Tarehe 7 Septemba, 2017
Total Page:16
File Type:pdf, Size:1020Kb
Load more
Recommended publications
-
1458124832-Hs-6-2-20
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA SITA Kikao cha Pili – Tarehe 1 Februari, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua MASWALI Na. 16 Ujenzi Usiokidhi Viwango Hospitali ya Wilaya ya Himo- Moshi Vijijini na Mawenzi MHE. BETTY E. MACHANGU aliuliza:- Kwa kawaida Mkandarasi anayejenga hospitali au jengo lolote lile hupewa ramani za michoro ya majengo husika lakini ni jambo la kushangaza kwamba majengo ya hospitali ya Wilaya inayojengwa Himo imeonesha upungufu mwingi, kwa mfano, vyumba vya maabara vilitakiwa kuwa saba (7) lakini vimejengwa vyumba viwili (2), idara ya macho vilitakiwa vyumba vitatu (3) lakini kimejengwa chumba kimoja (1) na katika hospitali ya Mkoa, Mawenzi jengo la operation la hospitali hiyo limejengwa katika viwango duni:- (a) Je, Serikali itafanya nini kwa ujenzi huo ulio chini ya viwango uliokwishajengwa kwenye hospitali hizo mbili? (b) Je, ni hatua gani zinazochukuliwa kwa wahusika wa matatizo haya? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU-TAMISEMI alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Betty Eliezer Machangu, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, hospitali ya Wilaya - Himo inatokana na kupandishwa hadhi kwa kilichokuwa Kituo cha Afya cha Himo. Ujenzi unaoendelea unalenga kuongeza majengo katika Hospitali hiyo kwa kuzingatia viwango vilivyowekwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii. Ujenzi unafanyika kwa awamu ambapo awamu ya kwanza imegharimu shilingi milioni 175. Awamu ya pili itagharimu shilingi milioni 319 ikihusisha ujenzi wa jengo la Utawala, Huduma ya Mama na Mtoto, jengo la X-Ray na uzio wa choo cha nje. -
Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1
Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA ISHIRINI Kikao cha Pili – Tarehe 13 Mei, 2015 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa tukae. Katibu! MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa, maswali tunaanza na ofisi ya Waziri Mkuu, anayeuliza swali la kwanza ni Mheshimiwa Josephine J. Genzabuke, kwa niaba yake Mheshimiwa Likokola! Na. 11 Fedha za Mfuko wa JK kwa Wajasiriamali Wadogo MHE. DEVOTHA M. LIKOKOLA (K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE) aliuliza:- Mfuko wa Wajasiriamali wadogowadogo maarufu kama mabilioni ya JK uliwavuta wengi sana lakini masharti ya kupata fedha hizo yamekuwa magumu:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kufanya mpango huo uwe endelevu kwa lengo la kuwanufaisha wanyonge? (b) Je, ni wananchi wangapi wa Mkoa wa Kigoma wamenufaika na mpango huo? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2006/2007, Serikali ilianzisha mpango wa uwezeshaji wananchi kiuchumi na kuongeza ajira kwa kutoa mikopo yenye masharti nafuu. Lengo la mpango huu ni kuwawezesha wananchi mijini na vijijini kupata mikopo ya kuanzisha au kuendeleza shughuli za kiuchumi ili kuongeza ajira na kipato. Masharti ya kupata mikopo hii si magumu sana ikilingalishwa na ile inayotolewa na mabenki, kwa sababu riba inayotozwa kwa mikopo hii ni asilimia 10, ikilinganishwa na riba inayotozwa na mabenki mengine, ambayo ni zaidi ya asilimia 20. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Mbili - Tarehe 22 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kwa masikitiko makubwa natoa taarifa kwamba Mheshimiwa Mussa Hamisi Silima, Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar, jana Jumapili, tarehe 21 Agosti, 2011 majira ya jioni kama saa mbili kasorobo hivi walipokuwa wakirejea kutoka Dar es Salaam, yeye na familia yake walipata ajali mbaya sana katika eneo la Nzuguni, Mjini Dodoma. Katika ajali hiyo, mke wa Mbunge huyo aitwaye Mwanaheri Twalib amefariki dunia na mwili wa Marehemu upo hospitali ya Mkoa hapa Dodoma ukiandaliwa kupelekwa Zanzibar leo hii Jumatatu, tarehe 22 August, 2011 kwa mazishi yatanayotarajiwa kufanyanyika alasili ya leo. Kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge tusimame dakika chache tumkumbuke. (Heshima ya Marehemu, dakika moja) (Hapa Waheshimiwa Wabunge walisimama kwa dakika moja) Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, amina. Ahsanteni sana, tukae. Kwa hiyo sasa hivi tunavyoongea Mheshimiwa Mbunge ambae nae pia ameumia vibaya na dereva wake wanaondoka na ndege sasa hivi kusudi waweze kupata yanayohusika kule Dar es Salaam na pia kule watakuwa na watu wa kuwaangalia zaidi. Lakini walikwenda Zanzibar kumzika kaka yake na Marehemu huyu mama. Kwa hiyo, wamemzika marehemu basi wakawa wanawahi Bunge la leo ndiyo jana usiku wamepata ajali. Kwa hiyo, watakaokwenda kusindikiza msiba, ndege itaondoka kama saa tano watakwenda wafuatao, watakwenda Wabunge nane pamoja na mfawidhi zanzibar yeye anaongozana na mgonjwa sasa hivi lakini ataungana na wale kwenye mazishi. -
20 MAY 2019.Pmd
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Thelathini na Moja – Tarehe 20 Mei, 2019 (Bunge Lilianza saa Tatu Asubuhi) DUA Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Mkutano wetu wa 15, leo kikao cha 31. Katibu! NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, nasikitika kuwatangazia kifo cha mwanasiasa mkongwe na kiongozi aliyepata kuhudumia kwa muda mrefu hasa kule kwenye Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Marehemu Ally Juma Shamhuna. Waheshimiwa Wabunge, katika uhai wake, marehemu Ally Juma Shamhuma amepata kushika nyadhifa mbalimbali zikiwemo hizi zifuatazo; amepata kuwa Mkurugenzi wa Mifugo, amewahi kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, amewahi kuwa Katibu Mkuu, Export Processing Zone Zanzibar, amewahi kuwa Waziri wa Mipango, amekuwa Waziri wa Nchi, Afisi ya Waziri Kiongozi, aliwahi kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo na wakati huo huo akiwa ni 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Naibu Waziri Kiongozi, katika uhai wake amekuwa Waziri wa Ardhi, Maji na Nishati na alipata kuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali. Aidha, Marehemu Mheshimiwa Shamhuna kwa muda mrefu alikuwa ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi kutokea Zanzibar na baadhi yenu humu Wabunge mtamkumbuka marehemu Mheshimiwa Shamhuna kama Mbunge wa Bunge la Katiba na alikuwa Mjumbe wa Kamati namba 8 kwenye Bunge la Katiba, Kamati ambayo nilikuwa Mwenyekiti wake. Kwa niaba yenu Waheshimiwa Wabunge, tunatoa pole kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Tunatoa pole kwa Wazanzibari wote na Watanzania wote kwa ujumla kufuatia kifo hicho na tunamuomba Mwenyezi Mungu aihifadhi roho yake mahali pema peponi, amina. -
Embaixada Do Brasil Em Dar Es Salaam Relatório De Gestão
EMBAIXADA DO BRASIL EM DAR ES SALAAM RELATÓRIO DE GESTÃO EMBAIXADOR CARLOS ALFONSO IGLESIAS PUENTE A presente versão simplificada e ostensiva do relatório de minha gestão como titular da Embaixada do Brasil em Dar es Salaam está estruturada da seguinte forma: I- Introdução II- Relações Políticas – política interna, externa e relações bilaterais; III- Relações Econômicas – panorama econômico-comercial e promoção comercial e de investimentos; IV- Cooperação Técnica e educacional – panorama, projeto Cotton Victoria e outros de cooperação técnica; cooperação educacional e promoção de língua portuguesa; V- Difusão cultural; VI – Cumulatividades – Comores, Seicheles e EAC 2. Algumas das maiores mudanças empreendidas pela minha gestão à frente do posto ocorreram nos setores de administração e consular. A fim de contornar as graves deficiências no controle patrimonial, decorrentes de problemas do programa de inventário, o posto conseguiu desenvolver novo banco de dados em Microsoft Access, cujas licenças também serviram para que se informatizasse, num segundo momento, o setor de administração, em particular o de contabilidade, e de atendimento consular. O sistema informatizado pôde garantir um serviço ao consulente ainda mais rápido e eficaz, de forma a complementar medidas adotadas logo que assumi a embaixada, e destinadas a tornar o atendimento mais humanizado e empático, entre as quais destaco a bem-sucedida implementação de protocolo de atendimento consular, que tem contribuído para assegurar atendimento ao público sempre cortês, eficiente e consistente. Na área consular, cite-se, ainda, a abertura recente, por proposta minha, de consulado honorário em Zanzibar, que tem por objetivo atender o crescente afluxo de turistas brasileiros no arquipélago e facilitar a interlocução com o governo daquela região semiautônoma. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Moja – Tarehe 5 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda na Biashara kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. NAIBU WAZIRI WA KAZI NA AJIRA: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kazi na Ajira kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MHE. JENISTA J. MHAGAMA - MWENYEKITI WA KAMATI YA MAENDELEO YA JAMII: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Kazi na Ajira kwa Mwaka 2010/2011 Pamoja na Maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MHE. REGIA E. MTEMA - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KWA WIZARA YA KAZI NA AJIRA: Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani juu ya Wizara ya Kazi na Ajira kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012. MASWALI NA MAJIBU Na. 373 Kuboreshwa kwa Maslahi ya Madiwani MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:- Madiwani ni nguzo muhimu katika kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi na nia ya Serikali ni kuboresha maslahi ya Madiwani iil waweze kutimiza wajibu wao ipasavyo;- Je, ni lini maslahi ya Madiwani yataboreshwa? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Felister Bura, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba, Waheshimiwa Madiwani ni nguzo muhimu katika kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi. -
Tanzania Human Rights Report 2015 Tanzania Mainland Legal and Human Rights Centre (LHRC) Tanzania Human Rights Report 2015
Tanzania Human Rights Report 2015 Tanzania Mainland Legal and Human Rights Centre (LHRC) Tanzania Human Rights Report 2015 Publishers Legal and Human Rights Centre Justice Lugakingira House, Kijitonyama P.O. Box 75254, Dar es Salaam, Tanzania Tel: +255222773038/48, Fax: +255222773037 Email: [email protected] Website: www.humanrights.or.tz Partners - LHRC Accountability in Tanzania (AcT) The Embassy of Norway The Embassy of Sweden ISBN: 978-9987-740-25-3 © LHRC 2016 - ii - Tanzania Human Rights Report 2015 Editorial Board Dr. Helen Kijo-Bisimba Adv. Imelda Urrio Ms. Felista Mauya Adv. Anna Henga Mr. Castor Kalemera Researchers/Writers Mr. Paul Mikongoti Mr. Pasience Mlowe Mr. Fundikila Wazambi Design & Layout Mr. Rodrick Maro - iii - Tanzania Human Rights Report 2015 Acknowledgement Legal and Human Rights Centre (LHRC) has been producing the Tanzania Human Rights Report, documenting the situation in Tanzania Mainland since 2002. In the preparation and production of this report LHRC receives both material and financial support from different players, such as the media, academic institutions, other CSOs, researchers and community members as well as development partners. These players have made it possible for LHRC to continue preparing the report due to its high demand. In preparing the Tanzania Human Rights Report 2015, LHRC received cooperation from the Judiciary, the Legislature and the Executive arms of the State. Various reports from different government departments and research findings have greatly contributed to the finalization of this report. Hansards and judicial decisions form the basis of arguments and observations made by the LHRC. The information was gathered through official correspondences with the relevant authorities, while other information was obtained online through various websites. -
MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao Cha Nane – Tarehe 12 Aprili, 2
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Nane – Tarehe 12 Aprili, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. TAARIFA YA SPIKA SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba niwape taarifa. Kama mlivyoona leo tumeingia hapa Bungeni kwa utaratibu mpya tofauti na ilivyozoeleka. Kanuni ya 20(1)(c) ya Kanuni za Bunge inaeleza kwamba Spika ataingia na kutoka ndani ya ukumbi wa Bunge akiongozana na mpambe wa Bunge lakini haitoi maelezo ya mlango gani utumike wakati wa kuingia au kutoka Bungeni. (Makofi/Kicheko) Katika Mabunge mengi ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola (Commonwealth) na nchi nyingine, utamaduni uliozoeleka ni kwa Spika wa Bunge kuingia ndani ya ukumbi wa Bunge akitokea chumba maalum cha Spika (Speaker’s Lounge). Baadhi ya nchi zenye utamaduni huo ambazo mimi na misafara yangu mbalimbali tumewahi kushuhudia ni India na Uingereza, wana utaratibu kama huu tuliotumia leo. Kwa kuwa tumekuwa tukiboresha taratibu zetu kwa kuiga mifano bora ya wenzetu, kuanzia leo tutaanza kutumia utaratibu huu mpya tulioutumia asubuhi ya leo kwa misafara 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) ya Spika, Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge kuingia na kutoka Bungeni kwa kutumia mlango wa kuelekea Speakers Lounge, ni kuingia na kutoka kwa utaratibu huu hapa. Waheshimiwa Wabunge, mlango mkuu wa mbele utaendelea kutumiwa na Waheshimiwa Wabunge kama kawaida yenu na Spika na msafara wake watautumia mlango huu mkuu wakati wa matukio maalum ya Kibunge kama vile wakati wa kufunga au kufungua Bunge au tunapokuwa na ugeni wa Kitaifa kama Mheshimiwa Rais akitutembelea tutaingia kwa lango lile kuu, katika siku za kawaida zote tutafuata utaratibu huu mliouona hapa mbele. -
Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Hamsini na Nne - Tarehe 24 Agosti, 2011 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua NAIBU SPIKA:Waheshimiwa Wabunge, kufuatia kikao cha pamoja cha Kamati ya Uongozi na Tume ya Huduma za Bunge kilichofanyika jana mchana Wajumbe walikubaliana na kupanga utaratibu wa namna watakavyoshiriki katika mazishi ya Mheshimiwa Mussa Khamis Silima, yatakayofanyika leo tarehe 24 Mwezi wa Agosti 2011 Zanzibar. Walikubaliana kuwa mwili wa Marehemu uchukuliwe Dar es Salaam na kwenda Zanzibar moja kwa moja na Waheshimiwa Wabunge watasafirishwa kwa ndege itakayowachukua kutoka Dodoma hadi Zanzibar kwenye mazishi na kuwarudisha Dodoma baadaye leo hii. Vile vile, wajumbe walikubaliana kuwa makundi yafuatayo ndiyo yatakayokwenda kushiriki katika mazishi hayo. Kwanza Wajumbe wa Kamati ya Uongozi, pia Wajumbe wa Tume ya Huduma za Bunge, tatu wajumbe nane kutoka Zanzibar na nne ni baadhi ya Wabunge kutoka Kamati ya Nishati na Madini pamoja na Menejimenti ya Ofisi ya Bunge. Waheshimiwa Wabunge, kuhusu utaratibu wa usafiri ni kwamba Ofisi ya Katibu wa Bunge imepata ndege mbili, moja yenye uwezo wa kubeba abiria kumi na moja na nyingine yenye uwezo wa kubeba abiria 49 hivyo jumla ya watakaohudhuria mazishi ni 60. Ndege ya kwanza itakayoondoka itabeba abiria 11 kama nilivyosema na itaondoka Dodoma saa Nne asubuhi hii. Ndege ya pili itakayobeba abiria 49 itaondoka saa nne na nusu asubuhi ya leo. Wote wanaosafiri wanaombwa kufika uwanja wa ndege wa Dodoma kuanzia saa tatu na nusu asubuhi hii. Waheshimiwa Wabunge, shughuli za ibada na mazishi zitaanza saa sita na nusu mchana huko Zanzibar na mazishi yatafanyika saa saba mchana mara baada ya mazishi ndege zitaanza kuondoka kurudi Dodoma, Ndege inayobeba abiria 49 itaondoka Zanzibar kurudi Dodoma saa tisa alasiri. -
A Study of Tanzania's Non-Compliance with Its
A STUDY OF TANZANIA’S NON-COMPLIANCE WITH ITS OBLIGATION TO DOMESTICATE INTERNATIONAL JUVENILE JUSTICE STANDARDS IN COMPARISON WITH SOUTH AFRICA JULIUS CLEMENT MASHAMBA A THESIS SUBMITTED IN FULFILLMENT OF THE REQUIREMENTS FOR THE DEGREE OF DOCTOR OF PHILOSOPHY (Ph.D.) OF THE OPEN UNIVERSITY OF TANZANIA 2013 ii CERTIFICATION We, the undersigned, hereby certify that we have supervised and thoroughly read the thesis and we have found it to be in the form acceptable for submission as it is an original work of the author. Main Supervisor’s Signature: _____________________________ PROF. MOHAMMED S. HUSSAIN DATED at Dar es Salaam this……. day of …………….., 2013 Co-Supervisor’s Signature: _____________________________ DR. PAUL KIHWELO DATED at Dar es Salaam this……. day of …………….., 2013 iii STATEMENT OF COPYRIGHT This Thesis is a copyright material protected under the Berne Convention, the Copyrights and Neighbouring Act (1999), and other international and national enactments; thus, an intellectual property. No part of this thesis may be reproduced, stored in any retrieval system, or transmitted in any form by any means, electronic, mechanical, photocopying, recording or otherwise without prior written permission of the author or the Open University of Tanzania in that behalf. iv DECLARATION I, JULIUS CLEMENT MASHAMBA, do hereby declare that, this thesis is my work, and that it has not been presented to any university for a similar or any other degree award. Signature: ___________________________ JULIUS CLEMENT MASHAMBA DATED at Dar es Salaam this……. day of …................... 2013 v DEDICATION To all African children who suffer unnoticed behind bars. vi ACKNOWLEDGMENT This research work is a result of contributions and efforts harnessed from many people and institutions. -
Uongozi Kuanzia 1961
UONGOZI KATIKA SEKTA YA MAJI TANZANIA BARA KUANZIA UHURU MWAKA 1961 HADI LEO Utangulizi: Orodha ya Uongozi katika Sekta ya Maji Tanzania bara kuanzia mwaka 1961 mpaka sasa. Kuanzia mwaka 1961 Tanzania ilipopata NA WAZIRI MWAKA NA KATIBU MKUU MWAKA uhuru wake, Sekta ya Maji imekuwa chini 1 Dereck Bryeson 1961 - 1964 1 Ibrahim Sapi Mkwawa 1962 - 1964 ya wizara mbalimbali. Jumla ya Wizara 2 Alhaji Tewa S. Tewa 1964 - 1966 2 Dickson A. Nkembo 1964 - 1965 3 Cleopa D. Msuya 1965 - 1967 20 ziliundwa kwa nyakati tofauti katika 3 Said A. Maswanya 1966 - 1968 4 Ernest A. Mulokozi 1967 - 1968 kipindi hicho ili kusimamia Sekta ya Maji. 5 David A. Mwakosya 1968 - 1968 Mwanzoni baada ya Uhuru, katika 4 Abdurahman Mohamed Babu 1968 - 1970 6 Awinia Mushi 1968 - 1969 muundo sekta ya maji ilikuwa ni Idara ya 7 Timothy Apiyo 1969 - 1970 Maji na Umwagiliaji ikiwa chini ya Wizara 5 Dkt. Wilbert Chagula 1971 - 1974 6 E. Elinawinga 1974 - 1975 8 Frederick Rwegarulila 1970 - 1978 ya Ardhi,Upimaji Ramani na Maji Dkt. Wilbert Chagula 1976 - 1978 (Ministry of Lands, Survey and Water) na E. Elinawinga 1978 - 1982 9 Harith B. Mwapachu 1978 - 1981 1981 - 1984 mwaka 1961 ilihamishiwa Wizara ya 7 Al Noor Kassum 1982 - 1986 10 Athumani Janguo 11 Fulgence M. Kazaura 1984 - 1985 Kilimo. 12 H. Z. Talawa 1985 - 1987 8 Dkt. Pius Yasebasi Ng’wandu 1986 - 1990 13 N. K. Nsimbira 1987 - 1990 Mwaka 1970 sekta ya maji iliweka 9 Christian Kisanji 1990 - 1990 14 Paul J. Mkanga 1990 - 1990 10 Jakaya Mrisho Kikwete 1990 - 1995 15 Prof. -
Majadiliano Ya Bunge ______
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Nane – Tarehe 6 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA UTARATIBU): Mheshimiwa Spika, Kabla sijawasilisha Hati Mezani ninapenda kutumia dakika yako moja kutoa shukrani za dhati kabisa kwako. Kwanza kwa kuwa wa kwanza kutangaza msiba wa Mama yangu na vilevile kuwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wote ambao wameniletea rambirambi kwa namna moja au nyingine kwa njia ya sms na kwa simu na hii imefanyika kwa wananchi wengi nchini kote. 1 Mheshimiwa Spika, ninawashukuru sana wote sina kitu cha kufanya isipokuwa kuwaambia kuwa asanteni sana, nimepata faraja na Mama yetu tumemwweka mahali pema katika nyumba yake ya milele. Kwa hiyo, baada ya maelezo hayo mafupi na kwa kuwapongeza na kuwashukuru wote naomba sasa kuwakilisha Hati Mezani. Taaarifa ya Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano, 2011/2012 - 2015/2016. NAIBU WAZIRI WA MAJI: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha, 2012/2013. MASWALI NA MAJIBU Na.143 Serikali Kujenga Nyumba za Walimu MHE. SULEIMAN M. N. SULEIMAN (K.n.y. MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA) aliuliza:- Shule nyingi za msingi zina upungufu mkubwa wa nyumba za walimu hivyo kusababisha walimu kuishi katika mazingira magumu na kutoripoti katika shule kama Nyamsebhi, Mnekezi, Shibela, Kageye, Ntono na Nyasalala katika Jimbo la Busanda. 2 Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za walimu katika shule hizo na nyingine ili kuboresha mazingira ya walimu kufanya kazi? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (ELIMU) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lolesia Bukwimba, Mbunge wa Busanda kwa kutoa maelezo yafuatayo.