HOTUBA YA WAZIRI WA MIUNDOMBINU, MHESHIMIWA DKT. SHUKURU JUMANNE KAWAMBWA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2010/2011

A: UTANGULIZI

1. Mheshimiwa Spika, baada ya Bunge lako Tukufu kupokea taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako tukufu likubali kupokea, kujadili na kupitisha Makadirio ya Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Miundombinu kwa mwaka wa fedha 2010/2011.

2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kuchukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kutujaalia uhai na afya njema na kutuwezesha sisi kushiriki katika Mkutano huu wa Bunge unaojadili Bajeti ya Serikali.

3. Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii pia kumshukuru na kumpongeza

1

Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa kwa kuendelea kuiongoza nchi yetu kwa uadilifu mkubwa na kudumisha umoja, amani na utulivu tangu amekabidhiwa madaraka ya kuliongoza Taifa letu. Kwa umahiri mkubwa ameendelea kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005 na kuendelea kutekeleza yale ambayo ameahidi kwa wananchi. Tunamuomba Mwenyezi Mungu amjalie afya njema, hekima na busara ili aendelee kuliongoza Taifa letu kwa amani na utulivu.

Aidha, napenda pia kumpongeza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein kwa kumsaidia na kumshauri Rais kwa hekima katika utekelezaji wa majukumu mazito aliyonayo.

4. Mheshimiwa Spika, naomba pia kumpongeza Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda, Mbunge wa Mpanda Mashariki, kwa kuendelea kuongoza vema shughuli za Serikali bungeni na kusimamia utekelezaji wa shughuli za Serikali.

5. Mheshimiwa Spika, naomba nikupongeze wewe mwenyewe binafsi kwa hekima, umahiri na busara

2

unazotumia katika kuliongoza Bunge hili Tukufu ambalo limefanya maamuzi mazito katika kipindi hiki cha miaka mitano. Maamuzi hayo yamethibitisha uwezo wa Bunge katika kusimamia demokrasia na utawala bora nchini.

6. Mheshimiwa Spika, kwa masikitiko makubwa napenda kuchukua fursa hii kutoa salamu za pole kwa msiba mkubwa uliolikumba Taifa letu kwa kuondokewa na Waziri Mkuu Mstaafu na muasisi wa TANU na CCM marehemu Mheshimiwa, Rashidi Mfaume Kawawa. Pole hizo ziifikie familia ya marehemu, ndugu, jamaa na watanzania wote. Aidha, napenda kutoa pole nyingi kwako wewe binafsi, Bunge lako tukufu, Kamati ya Bunge ya Miundombinu, familia ya marehemu na wananchi wa jimbo la Ruangwa kutokana na kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Mheshimiwa Sigifrid Selemani Ng’itu (Mb). Tutamkumbuka marehemu Mbunge kwa michango aliyoitoa katika vikao mbalimbali ndani na nje ya Bunge kwa lengo la kuleta maendeleo ya nchi yetu. Mungu azilaze roho za marehemu hao mahali pema peponi - Amen.

7. Mheshimiwa Spika, niruhusu niungane na waheshimiwa wabunge wenzangu kutoa pongezi zangu za dhati kwa Mheshimiwa Janeth Zebedayo Mbene (Mb.) wa CCM na Mheshimiwa Ismail Jussa Ladhu (Mb.) wa CUF walioteuliwa na Rais wa Jamhuri ya 3

Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Uteuzi wao ni ushahidi wa imani kubwa aliyonayo Mheshimiwa Rais kwao. Ni matarajio yetu kwamba michango yao itasaidia kuleta maendeleo ya nchi yetu. Aidha, napenda kuwashukuru kwa dhati wapiga kura wa jimbo la Bagamoyo kwa kunichagua kuwa mbunge wao na kuendelea kushirikiana nami katika kipindi chote cha utumishi wangu katika kuleta maendeleo ya Jimbo letu na Taifa kwa ujumla. Nitaendelea kuienzi fursa adhimu mliyonipa kuwa mwakilishi wenu. Ombi langu na mategemeo yangu kwa wananchi wangu wa jimbo la Bagamoyo ni kuwa mtanipa nafasi nyingine ya kushirikiana nanyi katika kipindi kijacho ili kuendelea kuliletea maendeleo jimbo letu.

8. Mheshimiwa Spika, kabla ya kutoa maelezo kuhusu hali ya kiutendaji ilivyokuwa kwenye sekta ya miundombinu kwa kipindi cha 2009/10, napenda kuishukuru Kamati ya Bunge ya Miundombinu chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa Alhaj Mohamed Hamisi Missanga, Mbunge wa Jimbo la Singida Kusini kwa kuendelea kunipa ushirikiano wa kutosha katika kuiongoza Sekta hii. Ushauri na maelekezo yao mazuri yaliiwezesha Wizara kusahihisha dosari mbalimbali katika mipango na utendaji, kwa lengo la kuongeza ubora wa huduma zitolewazo na sekta. Ushauri wao

4

utaendelea kuzingatiwa katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku ya sekta ya miundombinu.

9. Mheshimiwa Spika, napenda kuungana na Waheshimiwa Wabunge wenzangu, katika kuwapongeza na kuwashukuru Mawaziri waliotangulia kuwasilisha hoja zao, hususan Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda, Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mashariki na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mheshimiwa Mustafa Haidi Mkulo Mbunge wa Jimbo la Kilosa kwa hotuba zao ambazo zimetoa mwelekeo wa jumla katika masuala ya Mipango, Uchumi, Mapato na Matumizi kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2010/2011.

Naomba kuwashukuru Waheshimiwa wabunge waliochangia hotuba za Mawaziri waliotangulia. Maoni ya Waheshimiwa wabunge hao yamesaidia kuboresha mipango ya Serikali katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya Miundombinu.

10. Mheshimiwa Spika, tunapoingia katika kipindi cha mwaka 2010/2011, ni vyema tukatafakari utekelezaji wa maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya CCM ya mwaka 2005 na Ahadi za Viongozi Wakuu wa Serikali ili tuweze kupima kiwango cha utekelezaji wa Ilani na maendeleo tuliyopata pamoja na changamoto tulizokabiliana nazo.

5

11. Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo ya utangulizi, napenda sasa kuchukua nafasi hii kufanya mapitio ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005, majukumu ya kisera na kiutendaji na ahadi za Viongozi Wakuu wa Serikali. Aidha, nitaeleza utekelezaji wa mpango wa Wizara kwa mwaka wa fedha 2009/10, malengo na makadirio ya bajeti kwa mwaka 2010/2011.

B: MUHTASARI WA MAFANIKIO YA SERIKALI KATIKA UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM YA MWAKA 2005.

12. Mheshimiwa Spika, Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005 ilielekeza Wizara ya Miundombinu kutekeleza yafuatayo:

Ibara ya 44: Barabara

(a) Kuendelea kuimarisha Mfuko wa Barabara (Tanzania Road Fund)

13. Mheshimiwa Spika, ili kuendeleza na kuimarisha mfuko huu, Serikali imekuwa ikiongeza 6

kiasi cha tozo ya mafuta ambapo hadi mwaka 2007/08 imefikia shilingi 200 kwa lita. Katika kipindi cha mwaka 2009/10, Mfuko wa Barabara ulikusanya jumla ya Shilingi bilioni 284.1 ikilinganishwa na Shilingi bilioni 73.082 zilizokusanywa mwaka 2005/06. Ongezeko hili la fedha limeboresha hali ya barabara kutoka wastani wa asilimia 78 mwaka 2005 hadi asilimia 95 mwaka 2009.

Katika mwaka 2005/06 fedha za Mfuko wa Barabara zilizotolewa zilifanya matengenezo ya jumla ya Kilomita 39,532.9 ikilinganishwa na mwaka 2009/2010 ambapo Mfuko ulitoa fedha za matengenezo ya barabara ya jumla ya kilomita 58,230.1.

Hatua nyingine zilizochukuliwa na Wizara kupitia Bodi ya Mfuko wa Barabara ni kuunda kikosi kazi ili kubaini mianya ya uvujaji wa mapato na kufunga kifaa cha kusoma na kujua kiasi cha mafuta yanayoingizwa nchini kupitia bandari za Tanga na Dar es Salaam na taarifa zake kupelekwa moja kwa moja kwenye Bodi ya Mfuko wa Barabara ili kudhibiti mapato ya mafuta. Aidha, Wizara inaendelea na mchakato wa kuainisha vyanzo vingine vya mapato.

(b) Kukamilisha ukarabati wa barabara zote ambao unaendelea na ujenzi kwa kiwango 7

cha lami ambao umekwishaanza katika Barabara Kuu. Barabara hizo ni Dodoma – Manyoni, Manyoni – Singida, Singida – Shelui, Shelui – Igunga, Igunga – Nzega – Ilula; Muhutwe – Kagoma; Nangurukuru – Mbwemkulu – Mingoyo; Mkuranga – Kibiti; Pugu – Kisarawe; Chalinze – Morogoro – Melela; Tunduma – Songwe; Kiabakari – Butiama; Dodoma – Morogoro; Kagoma – Biharamulo – Lusahunga; Tabora – Kaliua – Malagarasi – Uvinza – Kigoma; Usagara – Chato – Biharamulo na Ndundu – Somanga

14. Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha jumla ya miradi 12 kati ya miradi 17 iliyopangwa kutekelezwa kwa kiwango cha lami. Hii ni sawa na asilimia 71 ya lengo. Miradi 12 iliyokamilika imejenga barabara za lami zenye jumla ya km 1,034.6 katika kipindi hiki cha kwanza cha Serikali ya Awamu ya 4. Miradi iliyokamilika ni kama ifuatavyo; Singida – Shelui (km 110), Shelui – Igunga – Nzega (km108), Nzega – Ilula (km 138), Muhutwe – Kagoma (km 24), Nangurukuru – Mbwemkuru – Mingoyo (km 190), Mkuranga – Kibiti (km 121), Pugu – Kisarawe (km 3.6), Chalinze – Morogoro – Melela (km 129), Tunduma – Songwe (km 71), Kyabakari – Butiama (km 11.4), Dodoma – Morogoro (256), Dodoma - Manyoni (km 127),

8

Buzirayombo - Kyamyorwa (km 120) na Buzirayombo – Geita (km 100).

15. Mheshimiwa Spika, miradi 5 iliyobaki ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji kama ifuatavyo: Ujenzi wa sehemu ya Manyoni - Isuna (Km 54) unaendelea ambapo jumla ya km 34 za barabara ya lami zimekamilika; Kuhusu mradi wa Kagoma-Lusahunga (Km 154): mkataba mpya ulitiwa saini mwezi Juni, 2009 na mpaka sasa kilometa 15 zimejengwa kwa kiwango cha lami; Mradi wa Tabora – Kaliua – Malagarasi – Uvinza – Kigoma (km 422): i) Sehemu ya Tabora-Urambo-Kaliua (km 126): zabuni za kazi za ujenzi zimetangazwa mwezi Aprili, 2010 kwa sehemu ya kutoka Tabora hadi Ndono (km 42) na Ndono hadi Urambo (km 48), ii) sehemu ya Kaliua-Malagarasi-Ilunde (km 156): Juhudi za kutafuta fedha za kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami zinaendelea, iii) Daraja la Malagarasi na Barabara zake (km 48): Taratibu za kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa Daraja zinaendelea chini ya ufadhili wa Serikali ya Korea Kusini. Fedha zilizopo zinatosheleza ujenzi wa daraja tu na sasa serikali inaendelea na mazungumzo ya kupata

9

fedha zaidi ili barabara za viungio nazo zijengwe. iv) Sehemu ya Ilunde-Uvinza-Kidahwe (km 104): Mkataba wa mkopo kutoka ABU DHABI kwa ajili ya kupata fedha za ujenzi wa km 77 umesainiwa Oktoba, 2009. Uchambuzi wa zabuni ili kupata mkandarasi uko kwenye hatua za mwisho na inatarajiwa kazi za ujenzi zitaanza katika mwaka wa fedha 2010/2011, v) sehemu ya Kidahwe – Kigoma (km 36): Mkandarasi amekamilisha kujenga jumla ya km 35 kwa kiwango cha lami.

Miradi mingine ni: (i) Usagara- Chato – Biharamulo (km 220): ambapo sehemu ya Usagara - Sengerema - Geita (km 92): Ujenzi unaendelea na kiasi cha kilometa 78 zimekamilika, sehemu ya barabara kutoka Geita – Bwanga (km70) zimejengwa na kukamilika kwa kiwango cha lami. Sehemu ya Bwanga - Biharamulo (km 69): Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami, na (ii) Ndundu – Somanga (Km 60): Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami unaendelea. Hivi sasa ujenzi wa makalvati na tuta umefikia asilimia 50.

(c) Kuendelea kuimarisha barabara nchini zitakazounganisha nchi yetu na nchi jirani

10

kwa barabara za lami; Makao Makuu ya Mikoa yote pia kwa barabara za lami na kuunganisha Makao Makuu ya Wilaya zote kwa barabara zinazopitika wakati wote.

16. Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuimarisha barabara zinazounganisha nchi yetu na nchi jirani kwa ajili ya ustawi wa uchumi wa nchi yetu na jamii kwa ujumla. Hadi sasa nchi jirani zilizokwisha unganishwa na nchi yetu kwa barabara za lami ni 7 kati ya 8 ambazo ni: Zambia na DRC eneo la Tunduma, Malawi eneo la Kasumulo, Uganda eneo la Mutukula, Kenya eneo la Sirari na Namanga, Burundi eneo la Kobero na Rwanda eneo la Rusumo. Jitihada za kuunganisha nchi yetu na Msumbiji kwa barabara ya lami kupitia Daraja la Umoja zinaendelea.

Pamoja na nchi yetu kuunganishwa kwa barabara za lami na nchi jirani, kuna miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa inayolenga kuboresha usafirishaji kwa njia ya barabara kati ya nchi yetu na nchi jirani. Miradi hiyo ni pamoja na barabara zifuatazo:- Arusha – Namanga (km105): ujenzi unaendelea kwa kiwango cha lami, Tanga – Horohoro (km 65). Mkataba wa ujenzi ulitiwa saini Disemba, 2009 na tayari kazi zimeanza, Mwandiga – Manyovu (km 60): ujenzi umeanza Disemba, 2008 11

na kiasi cha kilometa 20 zimekamilika na Masasi – Mangaka – Mtambaswala (km 119) itakayounganisha nchi yetu na Msumbiji upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Sehemu ya Masasi – Mangaka (km 54) inaendelea kujengwa kwa kiwango cha lami kwa msaada kutoka Serikali ya Japan na kiasi cha kilometa 32 zimekamilika. Aidha, usanifu wa Mangaka – Mtambaswala (km 65) umekamilika. Serikali ya Tanzania na Msumbiji zinaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara kwa sehemu ya Mtambaswala – Mueda (Msumbiji) kwa kiwango cha lami.

17. Mheshimiwa Spika, kwa kuwa nchi za jirani zimeunganishwa na barabara za lami, Serikali inaendelea kuhamasisha wananchi waishio kando kando ya barabara hizo kutumia fursa hiyo ili kuibua rasilimali zilizopo kwa kufanya shughuli za kiuchumi na kijamii katika maeneo hayo.

18. Mheshimiwa Spika, ili sekta ya miundombinu iendelee kuwa kichocheo cha ukuaji wa uchumi wa nchi, Serikali imeunganisha Makao Makuu ya Mikoa yote nchini kwa barabara za lami isipokuwa mikoa minne (4) tu ambayo ni Rukwa, Kigoma, Tabora na Manyara. Mipango ya kuunganisha Makao Makuu ya Mikoa hii ni kama ifuatavyo: 12

Mkoa wa Rukwa: Maandalizi ya kuanza ujenzi wa Barabara ya Tunduma – Sumbawanga itakayounganisha Makao makuu ya mkoa wa Rukwa na Mbeya kwa msaada wa fedha toka Serikali ya Marekani kupitia Shirika lake la Changamoto ya Milenia. Millenuim Challenge Corperation (MCC) yanaendelea. Kazi zinatarajiwa kuanza Julai, 2010. Kwa sehemu ya Laela – Sumbawanga. Sehemu kati ya Tunduma hadi Laela, mchakato wa kuwapata makandarasi upo hatua za mwisho.

Mkoa wa Kigoma: Ujenzi wa barabara ya Kigoma - Tabora utakaounganisha makao makuu ya mikoa ya Tabora na Kigoma upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji kama nilivyoeleza katika aya ya 12 ya hotuba yangu.

Mkoa wa Tabora: Ujenzi wa barabara ya Tabora - Itigi - Manyoni itakayounganisha mikoa ya Tabora na Singida upo katika hatua mbali mbali za utekelezaji. Mchakato wa kupata makandarasi wa kujenga kwa kiwango cha lami sehemu ya brabara kati ya Tabora – Nyahua na Manyoni- Itigi – Nyahua upo hatua za mwisho.

13

Mkoa wa Manyara; Ujenzi wa barabara ya Singida - Babati - Minjingu kwa kiwango cha lami itakayounganisha mikoa ya Manyara, Arusha na Singida unaendelea. Hivyo, makao makuu ya mkoa wa Manyara (Babati) yatakuwa yameunganishwa na mikoa ya Singida na Arusha.

Barabara zote zinazounganisha Makao Makuu ya Wilaya na Mikoa hivi sasa zinapitika majira yote ya mwaka isipokuwa Wilaya za Makete na Ludewa ambazo bado zinapitika kwa tabu wakati wa masika. Juhudi zinaendelea kufanywa ili kuhakikisha kwamba barabara za wilaya hizi zinaboreshwa ili ziweze kupitika majira yote ya mwaka. Wizara imeanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa kilometa 5 kwenye barabara ya Njombe – Makete kwa kuanzia Makete. Aidha, maeneo korofi yote kwenye barabara hii yanaendelea kuimarishwa kwa kiwango cha changarawe.

(d) Kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara zifuatazo; Tunduma – Sumbawanga; Marangu – Tarakea – Rongai; Minjingu – Babati – Singida; Rujewa – Madibira – Mafinga; Mbeya – Chunya – Makongorosi; Msimba – Ikokoto – Mafinga; Arusha – Namanga; Tanga – Horohoro na 14

ukarabati wa barabara ya Kilwa (Dar es Salaam), barabara ya Mandela (Dar es Salaam) na barabara ya Sam Nujoma (Dar es Salaam).

19. Mheshimiwa Spika, miradi mipya ya barabara iliyoanishwa kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami ni kumi na mmoja (11). Kazi ya ujenzi imeanza katika miradi yote isipokuwa mmoja tu. Kati ya miradi hiyo ambayo ujenzi wake umeanza katika kipindi cha mwaka 2005 - 2010, miradi miwili imekamilika ambayo ni barabara za Sam Nujoma na barabara ya Kilwa katika jiji la Dar es Salaam. Ujenzi wa barabara kwa miradi hii mipya imezalisha barabara za lami zenye urefu wa jumla ya km 161.1. Miradi iliyobaki ipo katika hatua mbalimbali za ujenzi kwa kiwango cha lami. Miradi hiyo ni pamoja na Tunduma – Sumbawanga; Marangu – Tarakea – Rongai; Minjingu – Babati – Singida; Rujewa – Madibira – Mafinga; Mbeya – Chunya – Makongorosi; Msimba – Ikokoto – Mafinga; Arusha – Namanga; Tanga – Horohoro na ukarabati wa barabara ya Mandela (Dar es Salaam).

Marangu – Tarakea – Rongai (km 98):

(i). Tarakea – Rongai – Kamwanga (km 32) - Kazi ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami imekamilika.

15

(ii). Rombo Mkuu - Tarakea (km 32) - Jumla ya km 25 za barabara zimekamilika kujengwa kwa kiwango cha lami,

(iii). Marangu - Rombo Mkuu - Mwika - Kilacha (34 km): Kazi ilianza Juni, 2008 baada ya kusitishwa kwa mkataba wa mkandarasi wa kwanza kutokana na kushindwa kutimiza majukumu yake ya kimkataba. Hivi sasa ujenzi wa barabara hii umekamilika kwa asilimia 70,

Nelson Mandela (km 15.6): Utekelezaji wa mradi huu umefikia asilimia 60,

Arusha – Namanga (km 105): Ujenzi kwa kiwango cha lami umefikia asilimia 25,

Mbeya – Chunya – Makongolosi (km112): Mkataba wa ujenzi wa barabara hii sehemu ya Mbeya – Lwanjilo (km 36) kwa kiwango cha lami umesitishwa tangu Mei, 2009 kutokana na utendaji usioridhisha wa Mkandarasi. Kazi zilizotekelezwa kabla ya kusitishwa mkataba ni kusafisha eneo la barabara asilimia 50 na ujenzi wa tuta la barabara asilimia 33. Mkandarasi mwingine atatafutwa baada ya kesi iliyoko mahakamani kukamilika.

Msimba – Ikokoto – Mafinga (km 124): Jumla ya km 45 zimekamilika kujengwa kwa kiwango cha lami. Kazi ya ujenzi inaendelea na inatarajiwa kukamilika Septemba, 2010,

16

Tunduma – Sumbawanga (km 224.5): Mhandisi Msimamizi wa barabara hii amepatikana Septemba, 2009. Barabara hii imegawanywa katika sehemu 3, sehemu hizo ni Tunduma – Ikana (km 63), Ikana – Laela (km 64) na Laela – Sumbawanga (km 98). Barabara hii inajengwa kwa fedha za MCC na tayari mkandarasi kwa sehemu ya Laela – Sumbawanga amepatikana na anajiandaa kuanza kazi.

Tanga – Horohoro (km 65): Mkataba wa ujenzi ulitiwa saini Disemba, 2009 na ujenzi rasmi ulianza Aprili 2010,

Minjingu – Babati – Singida (km 224): Mkataba wa kuanza kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami ulisainiwa Januari, 2009. Kazi za ujenzi zinaendelea vizuri,

Rujewa – Madibira – Mafinga (km 151): Kazi ya usanifu na uandaaji wa michoro ya madaraja pamoja na kuandaa vitabu vya zabuni imekamilika, Hatua inayofuata sasa ni ya kupata mkandarasi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami.

(e) Kuzifanyia upembuzi yakinifu na usanifu barabara zifuatazo kwa ajili ya kujengwa kwa kiwango cha lami: Maganzo – Maswa –

17

Bariadi – Mkula – Lamadi; Babati – Dodoma – Iringa; Sumbawanga – Kigoma – Nyakanazi; Musoma – Fort Ikoma; Korogwe – Handeni – Kilosa – Mikumi; Nzega – Tabora – Sikonge – Chunya; Mtwara – Masasi – Songea – Mbamba Bay; Manyoni – Itigi – Tabora; Ipole – Mpanda – Kigoma na Bagamoyo – Saadani.

20. Mheshimiwa Spika, miradi iliyoianishwa kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu ni kumi (10). Miradi yote iliyoainishwa imefanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu isipokuwa miradi miwili tu ambayo kazi ya upembuzi na usanifu inaendelea. Kati ya miradi hiyo ujenzi umeanza katika miradi mitatu (3). Maelezo ya kina ya miradi hiyo ya barabara ni kama ifuatavyo:

(i) Barabara ya Maganzo – Maswa – Bariadi – Mkula – Lamadi (km 171): Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika. Mkataba wa ujenzi wa sehemu ya Bariadi – Lamadi katika barabara hii ulisainiwa Septemba, 2009. Mkandarasi yupo katika kipindi cha matayarisho ya kuanza kazi.

(ii) Barabara ya Babati – Dodoma – Iringa (km 530), sehemu ya:

18

Babati – Dodoma (km 265): Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika. Mkataba wa ujenzi wa barabara hii sehemu ya Dodoma - Mayamaya (km 43.65) umesainiwa Mei 2010 na hivi sasa mkandarasi amekusanya vifaa vya kazi tayari kuanza kazi. Sehemu ya Babato – Bongea (km 19.2) pamoja na Daraja la Kolo mikataba ya ujenzi pia imesainiwa. Aidha, sehemu iliyobaki (km 188.5) Serikali ya Japan imeonyesha nia ya kusaidia ujenzi kwa kiwango cha lami.

Dodoma – Iringa (km 265): Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika. Mkopo wa fedha kwa kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Serikali ya Japan kupitia Shirika lake la Maendeleo (JICA) kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiii ulisainiwa Oktoba, 2009. Kazi za ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami zitaanza katika mwaka wa fedha 2010/2011.

(iii) Barabara ya Sumbawanga – Kigoma – Nyakanazi (km 800): Kazi ya kufanya usanifu wa kina na maandalizi ya nyaraka za zabuni kwa ajili ya ujenzi wa barabara sehemu ya Mpanda – Kigoma – Nyakanazi (km 562) imekamilika. Aidha, Mkataba wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami sehemu ya Sumbawanga – Kanazi (km 75) na Kanazi - Chizi – Kibaoni (km 19

76.6) umesainiwa Juni, 2009. Kazi za ujenzi kwa sehemu ya barabara zimeanza.

(iv) Barabara ya Musoma – Fort Ikoma Gate (km 140): Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii umekamilika Mei, 2006. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi.

(v) Barabara ya Korogwe – Handeni – Kilosa – Mikumi (km 363): Usanifu wa kina na matayarisho ya nyaraka za zabuni kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii umekamilika. Aidha, mikataba ya ujenzi kwa ajili wa barabara hii sehemu ya Korogwe – Handeni (km 65), Handeni – Mkata (km 54), Dumila – Rudewa (km.45) na Magole –Turiani (km 49) ilisainiwa Juni, 2009. Makandarasi wameanza kazi za ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami.

(vi) Barabara ya Nzega – Tabora – Sikonge – Rungwa - Chunya (km 679): Usanifu wa kina na matayarisho ya nyaraka za zabuni kwa ajili ya ujenzi yalikamilika Januari, 2010. Aidha, sehemu ya Nzega - Tabora (km 116) mchakato wa kumpata mkandarasi upo hatua za mwisho na hivyo kazi za ujenzi rasmi zinatarajiwa kuanza Agosti 2010.

20

(vii) Barabara ya Mtwara – Masasi – Songea – Mbamba Bay (km 826):

Masasi – Mangaka (km 54): Ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Masasi – Matumbushi – Nangalamo (km 32.5) umekamilika. Kazi zimeanza katika sehemu iliyobaki ya kilometa 22 kutoka Nangalamo hadi Mangaka.

Mangaka – Tunduru - Namtumbo (km 331): Serikali kwa kutumia fedha za ndani itafanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa sehemu ya Mangaka – Tunduru (km 146) kuanzia mwaka wa fedha 2010/11. Kuhusu sehemu ya Tunduru – Namtumbo (km 194), usanifu wa kina umekamilika na maandalizi ya kupata mkandarasi wa kujenga sehemu hii ya barabara yameanza kwa fedha za mkopo wa ADB na mkopo toka Serikali ya Japan kupitia shirika lake la JICA.

Namtumbo - Songea – Mbamba Bay (km 235): Usanifu wa kina na uandaaji wa nyaraka za Zabuni umekamilika. Mhandisi Msimamizi wa barabara hii amepatikana Septemba, 2009. Mkataba kwa ajili ya ujenzi kwa sehemu ya Namtumbo – Songea (km 67) umesainiwa mwezi Mei 2010 na Peramiho – Mbinga (km 78) mkataba wa ujenzi unatarajiwa kusainiwa mwezi Julai 2010. Ujenzi unatumia fedha za MCC

21

(viii) Barabara ya Manyoni – Itigi – Tabora (km 264): Mchakato wa kupata makandarasi kwa ajili ya ujenzi kwa sehemu ya Tabora – Nyahua (km 80) na Manyoni – Itigi – Chaya (km 85) upo katika hatua za mwisho.

(ix) Barabara ya Ipole – Tabora - Mpanda (km 338): Mkataba wa kufanya usanifu wa kina na maandalizi ya nyaraka za zabuni za barabara hii sehemu ya Mpanda - Ipole – Tabora (km 359) umesainiwa Juni, 2009. Mkataba huu ni wa miezi 20 na hivyo kazi itakamilisha mwezi Aprili, 2011.

(x) Barabara ya Bagamoyo – Saadani - Tanga (km 118): Kazi ya usanifu wa kina na maandalizi ya nyaraka za zabuni ya barabara hii yanaendelea.

(f) Kuhimiza maandalizi na ujenzi wa Daraja la Kigamboni chini ya uongozi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ili kuunganisha Kigamboni na Jiji la Dar es Salaam.

22

21. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kusimamia maandalizi ya ujenzi wa daraja la Kigamboni ambalo utekelezaji wake upo chini ya Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF). Mtaalam Mshauri aliyeajiriwa na NSSF kuandaa nyaraka za zabuni na kumpata Mbia mwenza kutoka sekta binafsi atakamilisha nyaraka za zabuni hizo mwezi Agosti, 2010. Nyaraka hizo zitasambazwa kwa wabia sita (6) waliopatikana ili waonyeshe uwezo wao kifedha na hatimaye ateuliwe mbia mmoja atashirikiana na NSSF kugharamia ujenzi wa daraja la Kigamboni.

(g). Kuhakikisha upatikanaji wa kivuko kipya cha Kigongo – Busisi (Mwanza):

22. Mheshimiwa Spika, Kivuko kipya cha Kigongo - Busisi kinachoitwa M.V. Misungwi chenye uwezo wa kubeba tani 250 kimepatikana na kinafanya kazi tangu Mei 2008.

(h). Kukamilisha ujenzi wa daraja jipya la Mpiji ambalo litawezesha njia mbadala ya Dar es Salaam – Tanga:

23

23. Mheshimiwa Spika, Ujenzi wa daraja hili umekamilika.

(i). Kufanya upembuzi yakinifu, usanifu na ujenzi wa daraja la mto Kilombero na kukamilisha ujenzi wa daraja la mto Mwatisi katika mkoa wa Morogoro.

24. Mheshimiwa Spika, kazi ya upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na utayarishaji wa Nyaraka za zabuni kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Kilombero zimekamilika Desemba, 2009. Ujenzi wa daraja hili utaanza katika mwaka 2010/11. Kuhusu daraja la Mto Mwatisi, ujenzi wa Daraja umeanza Agosti, 2009 na umefikia kiwango cha asilimia 25 na kazi zinaendelea.

(j). Kufanya usanifu wa daraja jipya la Ruvu:

25. Mheshimiwa Spika, usanifu na ujenzi wa daraja la mto Ruvu umekamilika Septemba,

24

2008 na kufunguliwa rasmi na Makamu wa Rais, Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein mwaka 2009.

(k). Kuendelea kuandaa mazingira mazuri ya kuishirikisha sekta binafsi katika ujenzi na matengenezo ya barabara kwa kutumia mfumo wa Jenga, Endesha na Kabidhi (BOT).

26. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya kushirikisha Sekta binafsi. Baadhi ya mikakati hiyo ni pamoja na kukamilisha Sera ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta binafsi na kupitishwa kwa sheria inayohusiana na masuala haya. Aidha, Serikali itatumia mwongozo na kanuni hizi kuhakikisha kuwa Sekta binafsi inashirikishwa kikamilifu katika ujenzi na matengenezo ya Miundombinu ya uchukuzi kwa mfumo wa Jenga, Endesha na Kabidhi (BOT).

(l). Kuanza ujenzi wa daraja la Umoja kati ya Tanzania na Msumbiji.

27. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Daraja la Umoja lenye urefu wa meta 720 ambao unajumuisha ujenzi wa barabara yenye urefu wa km 5 pande zote za daraja, ulikamilika na kufunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa

25

Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Armando Emilio Guebuza katika kijiji cha Mtambaswala, Mtwara. Ufunguzi huu ulifanyika tarehe 12 Mei, 2010.

Daraja hili linategemewa kuongeza fursa za kibiashara kati ya nchi hizi mbili pamoja na kukuza ukanda wa maendeleo wa Mtwara.

(m) Kuanzishwa programu ya Taifa ya Usafiri Vijijini.

28. Mheshimiwa Spika, suala la uboreshaji wa huduma za usafiri vijijini ni muhimu kwa kutambua kwamba asilimia 80 ya watanzania wanaishi maeneo ya vijijini ambapo sehemu kubwa ya shughuli za kilimo hufanyika. Kutokana na gharama kubwa za ujenzi wa miundombinu ya barabara, Wizara kwa kushirikiana na ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeendelea kuhimiza matumizi ya teknolojia stahili ya nguvu kazi ambayo inatumia gharama nafuu.

Aidha, Wizara kupitia Chuo cha Matumizi Stahili ya Nguvu Kazi imeendelea kutoa mafunzo kwa Makandasi wa Nguvu kazi pamoja na Wahandisi kutoka Halmashauri mbalimbali na sekta binafsi. Mafunzo hayo yametolewa pia kwa wanawake

26

wanaofanya kazi kwa kutumia teknolojia ya nguvu kazi na wanaotarajia kuanzisha kampuni za Ukandarasi kwa kutumia teknolojia Stahili ya Nguvu kazi.

Ibara ya 45: Usafiri na Uchukuzi

29. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha huduma za Usafiri na Uchukuzi kwa kushirikisha sekta binafsi na kuboresha miundombinu ya uchukuzi. Maboresho haya yanaenda sambamba na maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005 ambayo ilielekeza sekta hii kuchukua hatua zifuatazo:

(a) Kuendelea kuliimarisha Shirika la Reli Tanzania (TRC) kwa lengo la kulipa uwezo wa kutoa huduma bora kwa bidhaa na abiria wa ndani na wa nchi jirani. Pia, Shirika litaendelezwa kama mhimili wa mpango wa maendeleo wa eneo la Ukanda wa Kati.

30. Mheshimiwa Spika. kutokana na utendaji usioridhisha wa menejimenti ya TRL,

27

mwezi Machi, 2010 Serikali ilifanya uamuzi wa kusitisha mkataba wa uendeshaji wa TRL kwa kununua hisa asilimia 51 za RITES. Hatua zinazoendelea ni Serikali kufanya mazungumzo na RITES ili kuweza kuzinunua hisa hizo. Baada ya kukamilisha ununuzi wa hisa za RITES, Serikali itaendesha shughuli zote za reli ya kati mpaka hapo atakapopatikana Mbia mwingine.

Serikali inaendelea kufanya matengenezo na ukarabati wa njia ya reli baada ya kuharibiwa na mvua nyingi zilizonyesha mwezi Disemba, 2009 na Januari, 2010 na hasa maeneo ya Kilosa.

(b) Kuendelea kuliimarisha Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) ili liweze kuhimili kwa uwezo mkubwa zaidi majukumu ya kuboresha huduma kwa bidhaa na abiria na kusaidia shughuli za uendelezaji wa mpango wa eneo la Ukanda wa Mtwara.

31. Mheshimiwa Spika, Serikali za Tanzania na Zambia kwa pamoja zimeendelea kuchukua hatua mbalimbali zenye lengo la kuimarisha TAZARA. Disemba, 2009, Mawaziri wenye dhamana ya reli ya TAZARA kutoka Tanzania na Zambia 28

walifanya ziara ya kikazi nchini China kwa lengo la kuwasilisha maombi ya msaada wa fedha na ufundi kwa ajili ya kuendesha shughuli za TAZARA. Aidha, Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China ilikubali maombi hayo kimsingi na kutoa mapendekezo ambayo yanafanyiwa kazi.

32. Mheshimiwa Spika, katika ziara hiyo, Itifaki ya 14 ya mkopo nafuu wa jumla ya Dola za kimarekani millioni 39.3 kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China ilisainiwa tarehe 19 Disemba, 2009. Mkopo huu ni kwa ajili ya kuimarisha TAZARA kwa kuiongezea uwezo wa injini, mabehewa, nyenzo mbalimbali za uendeshaji na mafunzo kwa wafanyakazi. Katika makubaliano hayo Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China pia imefuta nusu ya deni la ujenzi wa reli ya TAZARA, na imeahidi kutuma wataalam kuja kutathimini matatizo na mahitaji ya TAZARA kwa nia ya kuboresha huduma za shirika. Serikali za Tanzania na Zambia kwa upande wao zinaendelea kuandaa mikakati inayofaa kuchukuliwa ili kuimarisha utendaji wa TAZARA. Kuimarika kwa reli ya TAZARA kutachochea maendeleo ya miradi iliyoko katika ukanda wa maendeleo ya kiuchumi wa Mtwara.

(c) Kuendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa reli mpya za Arusha – Musoma, 29

Isaka – Kigali na eneo la Ukanda wa Mtwara, ambayo itaunganisha Bandari ya Mtwara, Songea, Mbamba Bay, Mchuchuma na Liganga.

33. Mheshimiwa Spika, kutokana na umuhimu wa reli hizi katika kukuza uchumi wa nchi yetu, Serikali imeweka miradi hii katika vipaumbele vya miradi ya maendeleo. Aidha, reli hizi ni kati ya miradi iliyo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kupitia Mpango Kabambe wa Reli (East African Railway Master Plan) wenye lengo la kuboresha huduma za uchukuzi za Afrika Mashariki.

Katika ujenzi wa reli ya Arusha – Musoma, Serikali za Tanzania na Uganda zinaandaa mkakati wa pamoja kutekeleza ujenzi wa reli hii ili isaidie kusafirisha mizigo ya Uganda na ukanda wa Kaskazini kupitia bandari ya Tanga. Mradi huo unajumuisha ujenzi wa reli mpya kati ya Musoma na Arusha, ujenzi wa reli mpya kati ya Kange na Bandari mpya ya Mwambani (Tanga), ujenzi wa bandari mpya ya Mwambani, uboreshaji wa reli kati ya Tanga na Arusha na upanuzi wa bandari ya Musoma.

30

Kuhusu reli ya Isaka – Kigali, kazi ya kufanya upembuzi yakinifu wa mradi wa ujenzi wa reli ya Isaka – Kigali/Keza – Gitega – Musongati ilikamilika Septemba 2009. Kazi inayoendelea ni kufanya maandalizi ya usanifu wa kina wa reli hii. Aidha, Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) imekubali kutoa fedha jumla ya “units of accounts” milioni 1.66 sawa na Shilingi za Kitanzania bilioni 3.9 kwa ajili ya kufanya usanifu huo. Kamati ya wataalam inaendelea na mchakato wa kumpata Mtaalam Mshauri wa kufanya usanifu wa mradi huu.

Ujenzi wa reli itakayounganisha Bandari ya Mtwara, Songea, Mbamba Bay, Mchuchuma na Liganga ni sehemu ya Mpango Kabambe wa Uendelezaji wa Ukanda wa Maendeleo wa Mtwara. Juhudi za kuwatafuta wawekezaji katika maeneo ya Mchuchuma na Liganga pamoja na ujenzi wa reli hii muhimu zimeanza chini ya uratibu wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC).

(d) Kuimarisha bandari za Kigoma na Kasanga.

34. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha Bandari za Kigoma na Kasanga ili ziweze kuhudumia vyema wakazi wa maeneo yanayozunguka Ziwa Tanganyika. Kazi 31

zinazoendelea ni ujenzi wa gati mbili katika Bandari ya Kasanga ili kuwezesha meli mbili kutia nanga kwa wakati mmoja na ukarabati wa barabara za kuingia bandarini. Kazi hizi zinatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2010.

Katika bandari ya Kigoma, kazi ya kuondoa mchanga na kuongeza kina cha maji (dredging) imekamilika. Kazi ya kujenga cherezo (docking yard) inatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka 2010.

(e) Kuvutia uwekezaji katika miundombinu ya usafiri na uchukuzi wa reli, barabara, maji na anga katika Kanda za Maendeleo ili kuimarisha biashara kati ya nchi yetu na nchi jirani na kuwafanya wawekezaji kuvutiwa na soko kubwa la bidhaa na huduma zitakazozalishwa. Aidha, uwekezaji katika kanda hizi utaiwezesha Tanzania kutumia nafasi yake ya kijiografia na kuendeleza wajibu wake wa kuzihudumia nchi jirani zisizo na bandari.

35. Mheshimiwa Spika, katika kutumia nafasi ya Tanzania Kijiografia, Serikali imechukua 32

hatua mbalimbali zenye lengo la kuwavutia wawekezaji katika sekta ya Miundombinu kwa lengo la kukuza uchumi wetu. Wizara inaendelea kutekeleza Mpango wa miaka kumi ya Uwekezaji katika Sekta ya Uchukuzi nchini, Mpango Kabambe wa Bandari (Port Master Plan) na Mpango Kabambe wa Kukuza Usafiri wa Anga (Civil Aviation Master Plan). Mipango hii imebainisha miradi mbali mbali ya kipaumbele inayolenga kuendeleza na kupanua huduma za uchukuzi.

Wizara kwa kupitia Wakala za Uwezeshaji wa Biashara na Uchukuzi katika Ukanda wa Kati (Central Corridor Transit Transport Facilitation Agency – TTFA) na Ukanda wa TANZAM (Dar es Salaam Corridor) inaweka mazingira mazuri ya biashara katika sekta ya uchukuzi na kuratibu huduma za usafirishaji. Aidha, Sekretariati ya Kudumu ya TTFA imeshaanza kazi kwa msaada wa fedha kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika na Sekretariati ya TANZAM (Dar es Salaam Corridor) kwa ufadhili wa fedha kutoka Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID) na fedha kutoka mashirika ya umma na binafsi kutoka nchi wanachama wa TANZAM. Hatua hii itawezesha kuongeza ufanisi wa shughuli za kibiashara kupitia nchini mwetu kwenda nchi jirani na hivyo, kuvutia wafanyabiashara wengi zaidi kutumia miundombinu yetu ya uchukuzi ikiwemo bandari ya Dar es Salaam kupitishia mizigo yao.

33

(f) Kuendelea kuutengenezea mazingira mazuri ya kibiashara Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam yatakayoweza kuundeleza kuwa kiungo (hub) cha usafiri wa anga kitaifa, kikanda na kimataifa.

36. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea na mkakati wa kuandaa mazingira mazuri ya kibiashara ya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha ili kiwe kiungo (hub) cha usafiri wa anga kitaifa, kikanda na kimataifa. Kazi zifuatazo zinaendelea kufanyika hivi sasa; kukamilisha utekelezaji wa awamu ya pili ya ukarabati na ujenzi wa barabara za viungio na maegesho, barabara ya kuruka na kutua ndege, kuweka taa za kuongozea ndege (Apron Ground Lights-AGL), ukarabati wa maegesho ya ndege ya Terminal I, maegesho ya ndege za mizigo (cargo apron) pamoja na kutunza mazingira.

Kazi ya ujenzi wa jengo jipya la watu mashuhuri (VIP lounge) eneo la Terminal II imekamilika Kazi zinazoendelea ni pamoja na usanifu wa ujenzi wa jengo jipya la abiria (Terminal III), usanifu wa ujenzi wa jengo jipya la mapokezi ya ugeni wa kitaifa (State Reception Building), kukamilisha uhamishaji wa

34

wananchi waliojenga ndani ya eneo la kiwanja ili kupisha upanuzi ambapo mpaka sasa wakazi 1,221 wa Kipawa wamehamishwa. Vile vile taratibu za kupata eneo la Kigilagila zimeanza zitakazowezesha ulipaji wa fidia wakazi wa eneo hili na kuwahamisha. Kazi nyingine ni kuweka mitambo ya kisasa ya ukaguzi wa abiria (check in system) na mitandao ya habari na mawasiliano. Aidha, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa mtandao wa habari na mawasiliano (ICT Network) imekamilika.

(g) Kukamilisha ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe na kuimarisha viwanja vya ndege vya Kigoma, Tabora na Shinyanga.

37. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa awamu ya tatu na ya mwisho ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Songwe unaendelea vizuri. Ujenzi wa kiwanja hiki unategemewa kukamilika mwezi Machi 2011. Kazi zinazofanyika ni pamoja na kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kuruka na kutua ndege, maegesho ya ndege na barabara za viungo (Taxi ways). Aidha, jengo la abiria na ununuzi wa vifaa vya ukaguzi (x- ray machines) ni sehemu ya mradi huu.

35

Kuhusu viwanja vya ndege vya Kigoma na Tabora, Serikali itakarabati viwanja hivyo katika mwaka wa fedha wa 2010/11 kwa kujenga barabara za kutua na kuruka ndege kwa kiwango cha lami na hivyo kuviwezesha kutumika majira yote ya mwaka. Kuhusu Kiwanja cha Ndege cha Shinyanga, Serikali kwa kushirikana na Benki ya Dunia imekamilisha kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa kiwanja hiki. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi.

(h) Kutekeleza Mradi wa Mabasi ya Usafiri wa Haraka Dar es Salaam.

38. Mheshimiwa Spika, Mradi wa Mabasi ya Usafiri wa haraka katika jiji la Dar es Salaam umeendelea kutekelezwa kwa awamu. Ili kuanza ujenzi wa miundombinu ya Mradi huu, tayari Mtaalam Mshauri atakayesimamia ujenzi wa miundombinu hiyo ameajiriwa na kuanza kazi. Mchakato wa kuwapata makandarasi wa ujenzi umeanza Oktoba, 2009 na inatarajiwa kuwa kazi za ujenzi wa miundombinu zitaanza mwaka 2011. Aidha, rasimu ya zabuni ya kampuni mbili kwa ajili ya kutoa huduma za uendeshaji, ukusanyaji nauli na menejimenti ya fedha kwa awamu ya kwanza ya DART zimekamilika.

36

Ibara ya 46: Mawasiliano

(f) Kuimarisha uwezo wa utabiri wa hali ya hewa nchini kwa kutumia vyombo vya kisasa.

39. Mheshimiwa Spika, suala la kuimarisha huduma za hali ya hewa nchini ni muhimu kwa usalama na maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla. Hivi sasa Serikali kupitia Wizara ya Miundombinu ipo katika mchakato wa kukamilisha uandaaji wa Sera ya Taifa ya Hali ya Hewa. Sera hii ndiyo itakayokuwa mwongozo katika uimarishaji, uboreshaji na utoaji wa huduma ya hali ya hewa nchini. Katika kipindi cha 2009/2010 Serikali imeendelea kuimarisha huduma za hali ya hewa na utoaji wa huduma za hali ya hewa ambazo ni pamoja na utabiri wa kila siku wa hali ya hewa, utabiri wa hali ya hewa wa msimu na tahadhari ya hali mbaya ya hewa hususan majanga ya asili kama ukame, mafuriko na vimbunga.

40. Mheshimiwa Spika, Serikali iliweza kuongeza vituo vikuu vya utabiri wa hali ya hewa (synoptic stations) kutoka 26 (2008/09) hadi 28 37

(2009/10) vikijumuisha vituo vya Kilwa Masoko na Mpanda, kuongeza vituo vya hali ya hewa na kilimo kutoka 11 hadi 13 vikijumuisha vituo vya Matangatuani (Pemba) na Mbozi mkoani Mbeya na kuongeza vituo vya mvua kutoka 600 hadi 1400. Serikali pia kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa imeendelea na ununuzi wa mitambo na vifaa mbalimbali vya hali ya hewa ikiwemo mitambo ya utabiri ‘Synergie system’ na ‘Hydrogen plant’ na mifumo ya utabiri ya “Weather Research Forecasting- WRF” na “High Resolution Model- HRM”.

41. Mheshimiwa Spika, mafanikio mengine ni pamoja na Serikali kununua ‘radar’ ya hali ya hewa. Kazi inayoendelea ni ukamilishaji wa ujenzi wa miundombinu katika eneo litakalotumika kama Kituo cha Radar cha Hali ya Hewa nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Taratibu za ununuzi wa radar hiyo zimekamilika na inatarajiwa kuwasili nchini Julai, 2010 na kuanza kufanya kazi Agosti, 2010 baada ya kufungwa. Matumizi ya radar za hali ya hewa katika utoaji wa huduma ni muhimu kwani huongeza usahihi wa taarifa za hali ya hewa.

Serikali kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa imeongeza miundombinu ya mawasiliano na uchambuzi wa taarifa za hali ya hewa katika Kituo Kikuu cha Taifa 38

cha Utabiri wa Hali ya Hewa ili kuhakikisha kwamba taarifa na tahadhari za matukio ya hali ya hewa mbaya yanapokelewa na kusambazwa kwa taasisi zinazohusika na wananchi kwa wakati.

42. Mheshimiwa Spika, mafanikio mengine yaliyopatikana yanajumuisha utekelezaji wa mradi wa mabadiliko ya hali ya hewa kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais, Idara ya Mazingira unaofadhiliwa na Serikali ya Denmark, uimarishaji wa studio za utabiri wa hali ya hewa kwa kununua vifaa vya kisasa, upatikanaji wa hati ya kiwanja cha kujenga Makao Makuu ya Mamlaka ya Hali ya Hewa na kuanza kwa maandalizi ya ujenzi huo. Serikali kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa imekamilisha ujenzi wa karakana kwa ajili ya kutengeneza baadhi ya vifaa vya hali ya hewa. Serikali pia imeanza utekelezaji wa mfumo wa menejimenti ya ubora inayohusu kuzingatia viwango vya kutoa huduma za hali ya hewa kwa usafiri wa anga (Quality Management System).

Ibara ya 35: Utalii

(f) Kulisaidia Shirika la Ndege la Tanzania ili lichukue nafasi yake ipasavyo ya kuwa Shirika la Ndege la Taifa (National Flag

39

Carrier) kwa lengo la kuliwezesha Taifa kufaidika zaidi na mapato yatokanayo na Utalii.

43. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/2010, Serikali imeendelea kuisaidia Kampuni ya Ndege ya Tanzania ili iweze kuchukua nafasi yake katika kujenga uchumi wa Taifa letu kwa kutoa fedha ili kuwezesha kulipia gharama mbalimbali ikiwemo mishahara na mafuta. Ili kuongeza ufanisi katika uendeshaji wa Kampuni, Novemba 2009, Serikali ilitoa shilingi bilioni 3.6 kwa ajili ya mafao ya wafanyakazi 155 waliopunguzwa kazi. Aidha Serikali imeendelea kuisadia Kampuni kwa kulipa madeni mbali mbali ya Kampuni. Kwa sasa Serikali inafanya mazungumzo na wawekezaji ambao wameonesha nia ya kuwekeza ndani ya Kampuni. Lengo ni kuliunda upya Shirika la Ndege la Taifa kwa kushirikisha sekta binafsi.

Ibara ya 68: Maendeleo ya Makazi

(i) Kujenga mwamko wa kuzingatia mahitaji maalum ya watu wenye ulemavu katika ujenzi na utengenezaji wa majengo yanayotumiwa na Umma.

40

44. Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Nne imeendelea na nia yake ya kutambua, kuthamini na kujali mahitaji mbalimbali ya watu wenye ulemavu. Wizara imekwisha elekeza kuwa majengo yote ya Serikali yanayobuniwa yazingatie mahitaji maalum ya watu wenye ulemavu. Utekelezaji wa agizo hili unaendelea kusimamiwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA). Aidha, Wizara iko katika mchakato wa kuandaa rasimu ya Sheria ya Kudhibiti na Kusimamia Majengo nchini ambayo itahimiza juu ya ujenzi wa majengo kwa kuzingatia usalama wa watumiaji na mahitaji ya watu wenye ulemavu. Hatua nyingine zinazochukuliwa ili kuboresha mazingira kwa ajili ya walemavu ni kuendelea kujenga mwamko kwa umma wa kuzingatia mahitaji ya watu wenye ulemamavu katika majengo ya Umma.

(k) Kuendelea kujenga nyumba za watumishi wa Serikali kwa ajili ya kuwauzia.

45. Mheshimiwa Spika, Serikali ina nia ya kuboresha mazingira ya kuishi kwa watumishi wake kwa kuwapatia nyumba bora. Wizara kupitia Wakala wa Majengo ya Serikali imeendelea kujenga nyumba za kuwauzia watumishi wa Umma. Katika

41

kipindi cha 2005 hadi 2010, Serikali kupitia Wizara ya Miundombinu imejenga jumla ya nyumba 527 kwa ajili ya kuwauzia watumishi wa Umma na nyumba 185 kwa ajili ya kuishi viongozi mbalimbali wa kitaifa katika Mikoa yote ya Tanzania Bara. Ujenzi wa nyumba kwa ajili ya kuwauzia watumishi wa Umma na matumizi ya Viongozi wa Kitaifa yanaendelea.

C. HALI YA UTENDAJI WA UJUMLA WA SEKTA YA MIUNDOMBINU KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2009/2010.

46. Mheshimiwa Spika, kulingana na malengo na mikakati tuliyojiwekea, utendaji wa sekta ya miundombinu katika maeneo ya uchukuzi, ujenzi na hali ya hewa umeendelea kuimarika. Mafanikio hayo yanatokana na uboreshaji wa miundombinu na huduma zinazotolewa na Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi. Utendaji wa sekta umeendelea kuzingatia Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005, Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, MKUKUTA, Mkakati wa Kushirikiana na Wahisani (JAST), Malengo ya Milenia (MDGs), Sera za kisekta, Mikataba tuliyoridhia, makubaliano na Mashirika mbalimbali ya Kimataifa yanayohusu sekta zetu pamoja na utekelezaji wa ahadi za Viongozi Wakuu wa Serikali. 42

47. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutekeleza miradi ya ujenzi wa barabara kulingana na Ilani ya Uchaguzi ya ya mwaka 2005. Jumla ya miradi ya barabara 26 yenye urefu wa km 2,237 ilitekelezwa, miradi ya ujenzi wa barabara 28 yenye jumla ya urefu wa km 2,208 inaendelea kutekelezwa, miradi 7 yenye urefu wa jumla ya km 1,562 inaendelea kufanyiwa upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na matayarisho ya nyaraka za zabuni kwa ajili ya ujenzi. Miradi iliyokamilika upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ni 11 yenye urefu wa jumla ya km 2,745.

48. Mheshimiwa Spika, kwa ujumla barabara nchini zimeendelea kufanyiwa matengenezo katika viwango vya lami na changarawe ili ziweze kupitika katika kipindi chote cha mwaka. Kuhusu ujenzi na ukarabati wa Barabara Kuu na za Mikoa, jumla ya km 218 za Barabara Kuu zilifanyiwa ukarabati katika kiwango cha lami na km 156 kujengwa katika kiwango cha lami. Aidha, jumla ya km 42 za barabara za Mikoa zilijengwa kwa kiwango cha lami na km 591 zilifanyiwa ukarabati kwa kiwango cha changarawe. Kuhusu ujenzi wa madaraja, Serikali ilikamilisha ujenzi wa madaraja 51 ikiwa ni pamoja na Daraja la Umoja linalounganisha nchi ya Tanzania na Msumbiji. 43

Kuhusu matengenezo ya madaraja, jumla ya madaraja 4,365 yalifanyiwa matengenezo ya kuzuia uharibifu (Preventive Maintenance) na madaraja 231 yalifanyiwa matengenezo makubwa katika Barabara Kuu. Katika barabara za Mikoa, jumla ya madaraja 4,020 yalifanyiwa matengenezo ya kuzuia uharibifu na madaraja 429 yalifanyiwa matengenezo makubwa.

49. Mheshimiwa Spika, katika jitihada za Serikali kutimiza azma yake, iliunda Kikosi Kazi cha kuandaa Mkakati wa makusudi wa kuendeleza Makandarasi Wazalendo. Rasimu ya Mkakati huo imekamilika Februari, 2010. Wizara inaendelea kufanyia kazi mapendekezo ya Mkakati huo. Lengo la Mkakati ni kukuza uwezo wa makandarasi wazalendo kwa kuwapa kazi kubwa ambazo kwa sasa wanapewa makandarasi wa kigeni. Makandarasi hao watasaidiwa kupata mitambo, wataalamu na amana za fedha na watafanya kazi chini ya uangalizi wa karibu wa wataalamu Washauri. Matarajio ya Serikali katika mradi huo wa miaka mitano ni kuwa na makandarasi wazalendo wanaoweza kushindana na makandarasi wa kigeni.

44

50. Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio yaliyopatikana, ubora wa baadhi ya barabara nchini umekuwa hafifu kutokana na changamoto zilizojitokeza ikiwa ni pamoja na uwezo mdogo wa Makandarasi. Ili kukabiliana na upungufu huo, Wizara kupitia Bodi ya Usajili wa Makandarasi, Baraza la Ujenzi la Taifa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi imeendelea kutoa mafunzo kwa Wahandisi Washauri na Makandarasi wa Kizalendo ili wasimamie na kutekeleza vizuri mikataba ya ujenzi na matengenezo ya barabara. Aidha, Wizara imekuwa ikihakikisha kuwa makandarasi wanakabidhi barabara baada ya ujenzi au ukarabati kukamilika na kwa kuzingatia viwango vilivyokubalika.

51. Mheshimiwa Spika, huduma za usafiri wa anga zimeendelea kutolewa kwa kiwango cha kuridhisha ingawa kulikuwa na changamoto zilizoikumba sekta hii. Changamoto hizo ni pamoja na mtikisiko wa uchumi duniani, kupanda kwa bei ya mafuta. Kampuni za ndege za ATCL na PrecisionAir ni wadau wakuu wa usafirishaji kwa njia ya anga ndani ya nchi, zikiunganisha miji mikubwa nchini na nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika. Pamoja na Kampuni hizi mbili, kuna Kampuni ndogo za ndani zinazotoa huduma ya usafiri wa anga kibiashara na kijamii kama vile Community Air Line, Zan Air na Coastal Travel

45

ambazo hutoa huduma hasa kwa sekta ya utalii. Aidha, mashirika ya nje yamekuwa yakitoa huduma za usafiri kati ya nchi yetu na nchi mbalimbali. Huduma hiyo ya usafiri wa anga imekuwa ikitolewa ndani na nje ya nchi.

52. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuingia mikataba mipya na kuipitia upya mikataba ya usafiri wa anga kati ya Tanzania na baadhi ya nchi. Lengo la mikataba hii ni kutoa fursa kwa kampuni za ndege nchini kutoa huduma za usafiri wa anga katika nchi hizo na kampuni za nchi hizo kutoa huduma nchini mwetu. Katika mwaka 2009/2010, mikataba mipya iliyotiwa saini ni kati ya Tanzania na Uturuki, Jordan na Bahrain. Mikataba iliyopitiwa upya kwa lengo la kuiimarisha ni ile ya Tanzani na Kenya, Afrika Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Wizara kupitia Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) iliendelea kusimamia na kudhibiti usalama wa usafiri wa anga nchini. Katika mwaka 2009/10, hakuna ajali iliyotokea inayohusu upotevu wa maisha ya binadamu. Mwezi Machi, 2010, ndege ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) aina ya Boeing 737-200 ilipata ajali ilipokuwa inatua kwenye kiwanja cha ndege cha Mwanza na kusababisha uharibifu mkubwa wa ndege. Aidha, kumekuwepo na matukio madogo ya kibinadamu yanayotokana

46

na uhafifu wa miundombinu katika viwanja vilivyo kwenye mbuga za wanyama.

53. Mheshimiwa Spika, huduma za uchukuzi kwa njia ya Reli zimeendelea kutolewa na Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) na Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA). Serikali imeendelea kuhakikisha kuwa miundombinu ya njia ya reli, vichwa vya treni, mabehewa ya mizigo na ya abiria na usalama wa usafiri wa njia ya reli vinaboreshwa. Serikali ya Tanzania na Zambia zimefanikiwa kupata msaada wa fedha na ufundi kwa ajili ya kuboresha miundombinu na uendeshaji wa reli ya TAZARA. Serikali za Tanzania na Zambia zinaendelea kutafuta mwekezaji au mwendeshaji binafsi kwa ajili ya uendeshaji wa shughuli za TAZARA.

54. Mheshimiwa Spika, utendaji wa TRL, katika kipindi cha 2009/2010 haukuwa wa kuridhisha kutokana na utendaji hafifu wa Menejimenti ya TRL, uchakavu na ubovu wa miundombinu ya njia ya reli pamoja na mabehewa ya mizigo na abiria. Utendaji wake uliendelea kuathiriwa zaidi na uharibifu wa njia ya reli uliotokana na mvua nyingi zilizonyesha kati ya Disemba, 2009 na Januari, 2010. Mvua hizi ziliathiri miundombinu ya reli na barabara. Katika 47

harakati za kurudisha miundombinu katika hali yake ya kawaida, Serikali ilitoa jumla ya shilingi bilioni 15.6 kwa ajili ya ukarabati wa reli. Ukarabati wa miundombinu umefikia hatua ya kuridhisha na kazi iliyobaki ni uimarishaji wa maeneo yaliyokarabatiwa hususan tuta na kingo za mto Mkondoa.

Aidha, napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru wataalam wa Wizara ya Miundombinu, Jeshi la Wananchi wa Tanzania, RAHCO, TRL na Uongozi wa Mikoa ya Morogoro na Dodoma kwa kufanikisha ukarabati wa eneo lililoathirika na mafuriko.

55. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa usafiri majini, Serikali iliendelea kutoa huduma za uchukuzi katika maeneo ya pwani ya bahari ya Hindi na maziwa makuu. Lengo ni kuhakikisha kwamba huduma zinazotolewa na bandari zetu zinakidhi matakwa sio tu ya nchi yetu, bali pia ya nchi jirani. Njia hii ya uchukuzi inasaidia kukuza huduma za biashara katika nchi yetu na nchi za Rwanda, Burundi, DR Congo, Uganda, Zambia na Malawi. Kwa ujumla utendaji wa sekta hii ulikuwa wa kuridhisha kutokana na ukuaji kasi wa uchumi wetu na wa nchi jirani.

48

Ufanisi wa utoaji huduma katika Bandari ya Dar es Salaam uliongezeka kutokana na uboreshaji wa miundombinu ya bandari, mfumo wa upokeaji na utoaji mizigo bandarini pamoja na kuongezeka kwa eneo la kuhifadhi makasha ndani na nje ya bandari baada ya kujengwa ICDs za makampuni na watu binafsi, kupunguza muda wa makasha kukaa bandarini na kupungua msongamano wa meli na mlundikano wa makasha katika bandari ya Dar es Salaam. Mafanikio mengine yanatokana na utendaji mzuri katika utoaji wa huduma wa bandari za Ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa pamoja na bandari za Tanga na Mtwara.

Changamoto katika sekta hii ni uchakavu wa miundombinu ya bandari na kupungua kwa huduma za reli ambazo zimechangia kuchelewa kwa utoaji wa mizigo bandarini, hasa inayosafirishwa kwa njia ya reli na barabara.

56. Mheshimiwa Spika, kuhusu huduma za hali ya hewa, Serikali kupitia Wakala wa Hali ya Hewa imeendelea kutoa huduma hizo pamoja na tahadhari dhidi ya hali mbaya ya hewa katika kiwango cha kuridhisha. Taarifa za hali ya hewa zimekuwa zikitolewa katika baadhi ya vyombo vya habari na magazeti kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kujua hali halisi na kutumia taarifa hizo kupanga mipango yao ya kilimo, ujenzi, usafiri na

49

shughuli mbalimbali. Pamoja na huduma nzuri zilizotolewa, sekta hii ilikabiliwa na changamoto za ufinyu wa bajeti na ongezeko la watumiaji wa huduma za hali ya hewa linalotokana na kukua kwa sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii. Pia wamejitokeza watoaji huduma za hali ya hewa ambao hawafuati taaluma, miongozo na viwango vinavyotakiwa. Serikali iko kwenye mchakato wa kutengeneza Sera ya Taifa ya Hali ya Hewa itakayosimamia na kudhibiti sekta ndogo ya hali ya hewa.

57. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Wakala wa majengo nchini imeendelea kujenga nyumba za Serikali kwa lengo la kuwauzia watumishi wake. Hata hiyo kumekuwa na changamoto kadhaa zinazotokana na zoezi zima la kuboresha makazi ya watumishi wa serikali. Moja ya changomoto hizi ni uuzwaji wa nyumba katika maeneo ambayo nyumba hizo hazikutakiwa kuuzwa. Wizara imeendelea kusimamia mchakato wa kulimaliza tatizo hili kama alivyooagiza Mheshimiwa Rais.

50

D. MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA SEKTA KWA MWAKA 2009/2010 NA MALENGO YA MWAKA 2010/2011.

58. Mheshimiwa Spika, maelezo yaliyotangulia yanaonesha hali ya utendaji wa jumla wa sekta za ujenzi, uchukuzi na hali ya hewa kwa kipindi cha 2009/2010. Wizara ya Miundombinu kwa upande wake imeendelea na jukumu lake la kusimamia Sera, kuendeleza miundombinu na utoaji huduma katika sekta za uchukuzi, ujenzi na hali ya hewa.

Katika mwaka 2010/11, vipaumbele vimetolewa kwa kuzingatia miradi inayoendelea; miradi ambayo Serikali imeingia mikataba ya ujenzi; utekelezaji wa Sera za kitaifa na kimataifa, ahadi za Viongozi Wakuu wa nchi, ahadi za Serikali Bungeni na miradi inayofadhiliwa kwa pamoja kati ya Serikali na Washirika wa maendeleo. Orodha ya miradi itakayotekelezwa kwa mwaka wa fedha 2010/2011 imeoneshwa katika Kiambatanisho Na.1.

59. Mheshimiwa Spika, napenda nichukue fursa hii kueleza kwa kina kuhusu utendaji wa 51

sekta katika kipindi cha mwaka 2009/10 na malengo kwa mwaka 2010/11.

Ubunifu na utekelezaji wa Sera za Sekta

60. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Sera za kisekta. Sera hizo ni Sera ya Taifa ya Uchukuzi (2003), Sera ya Taifa ya Ujenzi (2003) na Sera ya Taifa ya Usalama Barabarani (2009). Aidha, Wizara imeendelea kukamilisha Sera ya Taifa ya Hali ya Hewa pamoja na kuifanyia mapitio Sera ya Taifa ya Uchukuzi (2003) na Sera ya Ujenzi (2003). Sera hizi zinatumika kama miongozo ya kusimamia maendeleo ya sekta pamoja na kutoa taratibu za uwekezaji katika kufikia malengo ya muda wa kati na muda mrefu. Malengo hayo ni pamoja na kuweka lami kwenye Barabara Kuu zote ifikapo mwaka 2018, kuhakikisha kuwa barabara za Mikoa zinakuwa angalau katika kiwango cha changarawe au lami nyepesi na zinazopitika wakati wote ifikapo mwaka 2015. Malengo mengine ni kuhakikisha kuwa bandari zetu kuu zinahudumia mizigo tani milioni kumi ifikapo mwaka 2015.

Kuhusu usafiri wa anga, malengo ya muda wa kati yanayotekelezwa ni pamoja na kuishirikisha sekta 52

binafsi ili iweze kutoa huduma kwa ufanisi zaidi; na kukifanya kiwanja cha ndege cha Mwalimu Julius Nyerere kuwa kiungo (hub) cha Usafiri wa anga katika Kanda. Kwa upande wa sekta ya reli, mkakati wa muda mfupi unaotekelezwa ni kuongeza uwezo wa reli kwa kuondoa reli yenye uzito mdogo (ratili 56.12 kwa yadi) na kuweka yenye uzito mkubwa (ratili 80 au zaidi kwa yadi).

Serikali ina mkakati wa muda mrefu wa kuiboresha reli ya kati kwa kuibadili njia yake toka kwenye muundo wa sasa wenye njia nyembamba na wenye uwezo mdogo (metre gauge) na kuifanya iwe pana (standard gauge) na yenye uwezo mkubwa.

Urekebishaji wa Taasisi za Wizara na Ushirikishwaji wa Sekta Binafsi

61. Mheshimiwa Spika, katika kuboresha huduma zitolewazo na Kitengo cha Makasha katika bandari ya Dar es Salaam na kuongeza ushindani, Serikali kupitia Wizara ya Miundombinu na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) kwa upande mmoja na Kampuni ya Hutchison Port Holdings Limited na Tanzania International Container Terminal Services (TICTS) kwa upande mwingine, walitiliana saini nyongeza ya Mkataba 53

(Addendum No. 3) katika Mkataba wa Ukodishaji wa Kitengo cha kontena katika Bandari ya Dar es Salaam. Nyongeza ya Mkataba huo ilihusu kuondoa kipengele kinachoipa TICTS ukiritimba wa kuhudumia meli zinazobeba Makasha. Kufuatia uamuzi huo, sasa Wawekezaji na Waendeshaji mbalimbali wanaruhusiwa kuhudumia meli zinazobeba makasha katika Bandari ya Dar es Salaam.

62. Mheshimiwa Spika, kufuatia utendaji usioridhisha wa Kampuni ya reli Tanzania (TRL), Februari, 2010, Serikali iliamua kununua hisa zote za RITES kiasi cha asilimia 51 ndani ya TRL. Ili kufikia azma hiyo, Serikali ilitoa ridhaa ya kujadiliana na RITES ili kununua hisa hizo. Kwa mantiki hiyo, mkataba kati ya Serikali na RITES utafutwa na hivyo Serikali itamiliki kampuni ya TRL kwa asilimia mia moja (100%) mpaka hapo atakapopatikana mwekezaji au mwendeshaji mwingine.

63. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa TAZARA, Disemba, 2009 Mawaziri wenye dhamana ya reli ya TAZARA walifanya ziara nchini China kwa madhumuni ya kusaini Itifaki ya 14 ya ushirikiano wa kiufundi na kiuchumi kuisaidia TAZARA. Aidha, Mawaziri walijadili mapendekezo ya Serikali za 54

Tanzania na Zambia ya kushirikisha sekta binafsi kutoka China kuendesha shughuli za TAZARA. Katika ziara hiyo, Serikali ya China ilikubali kutoa mkopo wenye masharti nafuu wa jumla ya RMBY milioni 270, sawa na USD milioni 39.3 kwa ajili ya kununua injini mpya za treni, mabehewa mapya ya mizigo, kufufua mabehewa ya mizigo na kukarabati injini za treni. Itifaki hii imeanza kutekelezwa Januari, 2010 na itakamilika baada ya miaka mitatu.

Kwa upande wa ushirikishwaji wa sekta binafsi kutoka China kuendesha shughuli za TAZARA, Serikali ya China itatuma vikundi viwili, kimoja cha wataalam wa kiufundi (Technical Team) na cha pili cha wataalam wa menejimenti (Operational and Management Team) kutoka Wizara ya Reli ya China kufanya tathmini ya hali halisi ya miundombinu ya reli na menejimenti ili kutoa uamuzi wa jinsi ya kurekebisha uendeshaji wa reli. Timu zote mbili zitaungana na wataalam kutoka Zambia na Tanzania kufanya kazi hiyo kwa pamoja.

64. Mheshimiwa Spika, kuhusu Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kuiwezesha UDA kuwa na mtaji wa kujiendesha yenyewe. Wawekezaji mbalimbali wamekuwa wakijitokeza ili kuendesha 55

UDA. Hata hivyo, wawekezaji hao wamekuwa hawakidhi viwango vinavyotakiwa na hivyo kushindwa kukabidhiwa uendeshaji wa Shirika. Serikali ilimwajiri Mtaalam Mwelekezi wa kuandaa nyaraka muhimu kama vile thamani ya mali na kutafuta thamani ya hisa ili kukamilisha zoezi la uuzaji wa hisa za serikali katika shirika la UDA.

65. Mheshimiwa Spika, kuhusu Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), Serikali imeendelea kuchukua hatua mbali mbali za kuiwezesha UDA kuwa na mtaji wa kujiendesha yenyewe, hii ikiwa ni pamoja na kuwasilisha mapendekezo Serikalini ya kufuta madeni ya muda mrefu ya UDA yenye thami ya shilingi milioni 612.189 kwa lengo la kuboresha mezania ya Shirika ili iweze kupata fedha kutoka taasisi mbali mbali za kifedha. Aidha, kutokana na mapendekezo ya Bodi ya UDA kuhusu hatma ya shirika, Serikali iko katika majadiliano na mwekezaji ambaye amejitokeza kununua hisa za Serikali za aslimia 49. Kupatikana kwa mwekezaji kutawezesha UDA kuongeza uwezo wake wakutoa huduma za usafiri jijini Dar es salaam na kushiriki katika mradi wa mabasi yaendayo kasi.

56

66. Mheshimiwa Spika, Wizara imechukua hatua mbalimbali ili kuboresha huduma za Kampuni ya Ndege (ATCL). Hatua hizo ni pamoja na Serikali kufanya uthamini wa kina wa mali za Kampuni ili kujua thamani yake, Serikali kutoa fedha kwa ajili ya kulipa madeni ya ATCL na kufanya mazungumzo na Kampuni ya China SONANGOL International Limited (CSIL) ambayo ilionyesha nia ya kununua asilimia 49 ya hisa za Serikali katika shirika jipya la Ndege la Taifa badala ya kuwekeza kwenye ATCL ya sasa. Mazungumzo kati ya pande mbili hizi hayajakamilika. Aidha, kwa kuwa majadiliano na CSIL yamechukuwa muda mrefu, Serikali inajipanga kuanza mchakato wa kumpta mwekezaji au mbia mwingine.

67. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kufanya mapitio ya sheria mbalimbali pamoja na kanuni zake ili kuimairisha usimamizi na utendaji na hivyo kuleta ufanisi katika sekta. Bunge lako tukufu katika Mkutano wake wa 18 lilipitisha Sheria ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi 2010 (The Architects and Quantity Surveyors Registration Act, 2010) kwa lengo la kusimamia na kuratibu mienendo na ubora wa shughuli na taaluma za wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi nchini. Aidha, kanuni 12 chini ya sheria mbalimbali zimewasilishwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa ajili

57

kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali kama ifuatavyo:

1. The Engineers Registration Regulations 2009; 2. The Engineers bylaws 2009; 3. The Procurement and Supplies Professionals and Technicians Code of Ethic and Conduct 2009; 4. SUMATRA Tariff Regulations 2009; 5. SUMATRA (Inquiry Procedures) Rules 2009; 6. SUMATRA (Procedures for Settling Claims for Late Delivery of Cargo) Rules 2009; 7. The Transport Licensing (Motorcycle and Tricycles) Regulations 2009; 8. TCAA (Rates and Charges) Rules 2009; 9. The Roads Use Regulations 2009; 10. The Civil Aviation (Procedures for Complaint Handling) Rules 2009; 11. The Road Reclassification Order, 2009 12. The Road Sector (Environmental Protection) Regulations 2009

68. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/11, Wizara imepanga kuwasilisha katika Bunge lako Tukufu Miswada mitatu. Miswada hiyo ni kama ifuatavyo: (i) Mswada wa sheria ya Majengo ambayo imelenga kudhibiti ujenzi wa majengo ili kuzuia ujenzi holela na hivyo kupunguza ama kuondoa kabisa madhara yatokanayo na nyumba

58

zilizojengwa bila kuzingatia ubora, (ii) Muswada wa sheria ya Utafutaji na Uokoaji wenye dhumuni la kuweka utaratibu wa kuratibu masuala ya utafutaji na uokoaji wakati wa ajali na dharura na (iii) muswada wa sheria ya Usalama Barabarani.

Utekelezaji wa Programu ya Uwekezaji Katika Sekta ya Uchukuzi (Transport Sector Investment Programme - TSIP)

69. Mheshimiwa Spika, Programu ya miaka 10 ya Uwekezaji katika Sekta ya Uchukuzi (Transport Sector Investment Programme – TSIP) imeendelea kutekelezwa kikamilifu kupitia bajeti ya Serikali pamoja na fedha za nje. Utekelezaji wa awamu ya kwanza ya miaka mitano ya Programu hii imeendelea kufuata mpango wa kuoanisha miradi iliyopewa kipaumbele na mpango wa muda wa kati wa Matumizi ya Serikali (Mid Term Expenditure Review Framework - MTEF). Katika mwaka 2009/10, Wizara ilifanya tathmini ya utekelezaji wa Programu hii kwa lengo la kufahamu hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wake. Matokeo ya tathmini hiyo yameonesha kwamba, hadi kufikia Juni 2009 karibu asilimia 40 ya miradi ya TSIP ndiyo iliyokuwa tayari imetekelezwa. Matokeo haya yanaonyesha changamoto tuliyo nayo katika utekelezaji wa Programu hii hasa ufinyu wa bajeti ya 59

Serikali pamoja na mchango mdogo wa sekta binafsi katika kuchangia utekelezaji wa Programu hii. Lengo la Serikali katika Programu hii ni kuona kwamba sekta binafsi inapewa fursa ya kutosha kushiriki katika utekelezaji wa TSIP hususan miradi inayoweza kutekelezwa kupitia mpango wa ubia kati ya Serikali na sekta binafsi.

70. Mheshimiwa Spika, sekta ya miundombinu imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali. Ili kuziibua na kuzijadili changamoto hizo, Wizara imekuwa ikiandaa Kongamano la Sekta za Miundombinu (Joint Infrastructure Roundtable). Katika kipindi cha mwaka 2009/2010, Wizara iliandaa Kongamano la pili la Sekta za Miundombinu mwezi Oktoba, 2009 ambalo lilijumuisha sekta zinazojihusisha na miundombinu. Sekta hizo ni Uchukuzi, Ujenzi, Nishati, Maji na Mawasiliano.

Masuala yaliyojadiliwa katika Kongamano hilo ni pamoja na mpango wa kuifanya Tanzania kuwa kiungo cha usafirishaji (Logistic Hub) kati yake na nchi jirani za Uganda, Kenya, Burundi, Rwanda, DRC, Zambia, Msumbiji na Malawi na jinsi ya kuboresha usafiri wa jiji la Dar es Salaam kupitia Mpango kabambe wa mabasi yaendayo kasi wa mwaka 2008. 60

Mapitio ya Utendaji wa Sekta ya Miundombinu

71. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea na utaratibu wake wa kila mwaka wa kupima utendaji wa sekta ya Miundombinu kupitia Kongamano la pamoja kati ya Serikali na Wahisani (Joint Infrastructure Sector Review – JISR). Mwezi Oktoba 2009, Wizara iliandaa Kongamano la tatu lililopima utekelezaji wa shughuli za sekta kwa kipindi cha mwaka 2009/10. Masuala yaliyojadiliwa kwa kina katika Kongamano hilo ni pamoja na umuhimu wa kutekeleza kwa ufanisi Sera mpya ya Usalama Barabarani iliyopitishwa na Serikali mwezi Januari 2010 pamoja na kupitia upya Sera ya Uchukuzi kwa lengo la kutoa mwelekeo mpya wa Sekta ya Uchukuzi kulingana na wakati uliopo. Moja ya Mikakati ya Serikali katika utekelezaji wa Sera ya Usalama Barabarani ni kuunda Wakala wa Usalama Barabarani utakaokuwa na jukumu la kusimamia usalama barabarani kwa lengo la kupunguza vifo vinavyoongezeka kupitia ajali za barabarani.

72. Mheshimiwa Spika, changamoto iliyojitokeza kwa Serikali katika Kongamano hilo ni lile la kutafuta mbinu mpya za kutekeleza Programu ya Uwekezaji kwenye Sekta ya Uchukuzi (TSIP) hasa mpango wa kushirikisha sekta binafsi katika miradi 61

ya ubia kati ya Sekta ya umma na sekta binafsi (Public Private Partnerships- PPPs). Masuala yaliyoonekana kuwa na nafasi ya kutekelezwa kupitia mpango huo ni pamoja na upanuzi wa miundombinu ya reli, bandari, viwanja vya ndege na barabara kwa miradi iliyofanyiwa tathmini ya kuonekana kuleta faida kwa mwekezaji. Aidha, suala la ongezeko la gharama za ujenzi lilionekana kukwamisha mipango ya Serikali na Wahisani katika kufanikisha malengo ya kuimarisha na kupanua miundombinu ya uchukuzi na ile ya ujenzi hapa nchini. Wizara itaendelea kutumia Kongamano hili ili kupima utendaji wa sekta za ujenzi, uchukuzi na hali ya hewa kwa lengo la kutathmini ukuaji wa sekta hasa katika kutekeleza mkakati wa Serikali wa kukuza uchumi na kupunguza umaskini nchini.

Huduma za Usafiri na Uchukuzi wa Barabara Mikoani na Vijijini

73. Mheshimiwa Spika, utoaji wa huduma za usafiri na uchukuzi kwa njia ya barabara mikoani na vijijini, pamoja na uendelezaji wa miundombinu, zimeendelea kusimamiwa na Wizara ya Miundombinu kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI na sekta binafsi. Kwa ujumla huduma za uchukuzi na idadi ya watoa huduma katika maeneo ya barabara za mikoa umeendelea 62

kuimarika hasa baada ya miundombinu ya uchukuzi kuboreshwa. Hata hivyo huduma za usafiri vijijini zimeendelea kuwa za wastani kutokana na uhafifu wa miundombinu. Uhaba wa miundombinu bora ya uchukuzi unakwamisha maendeleo katika maeneo hayo na hivyo kuwa kero na kusababisha kikwazo katika upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii. Wizara kwa kushirikiana na wadau wengine imeendelea kuhakikisha kuwa Sera ya Uchukuzi, Sera za Ujenzi pamoja na mikakati iliyojiwekea inatekelezwa ipasavyo ili kuboresha miundombinu hiyo.

Katika mwaka 2009/10, Wizara kwa kiasi kikubwa, iliendelea kuishirikisha sekta binafsi kutoa huduma za usafiri na usafirishaji kwa njia ya barabara ili kuhakikisha kuwa wananchi wa vijijini na mijini wanapata huduma bora za usafiri. Aidha, shughuli nyingi za kiuchumi na kijamii zimeendelea kutegemea usafiri kwa njia ya barabara kutokana na matatizo yanayoikabili sekta ya reli.

Uimarishaji wa Usafiri kwa Njia ya Barabara

74. Mheshimiwa Spika, sekta binafsi imeendelea kutoa huduma ya usafiri katika miji yetu, na katika hali ya ushindani ambao umesaidia kuinua kiwango cha ubora wa huduma na

63

kurahisisha upatikanaji wake. Aidha, SUMATRA imeboresha utaratibu wa utoaji leseni kwa kusogeza huduma karibu zaidi kwa wateja na hivyo kuwapunguzia muda wa kusafiri kwenda katika ofisi za Mamlaka katika makao makuu ya Mikoa. Katika mwaka 2009/10, jumla ya leseni 13,047 na ratiba 1,739 za mabasi ya abiria zilitolewa ikilinganishwa na leseni 11,194 na ratiba 1,600 zilizotolewa katika mwaka 2008/09. Ongezeko hili linadhihirisha kuhamasika kwa wasafirishaji kutumia Sheria na Kanuni za uchukuzi na usafirishaji.

75. Mheshimiwa Spika, msongamano wa magari katika miji mikubwa nchini utapungua kwa kuimarisha usafiri wa Umma. Kuimarika kwa usafiri wa umma na hasa kutumia mabasi makubwa kutavutia watu wenye magari madogo ya binafsi kutumia usafiri wa umma, hatimaye kupunguza msongamano. Ili kupunguza msongamano wa magari kwa kuanzia na Jiji la Dar es Salaam, Wizara kwa kushirikiana na SUMATRA ilianza juhudi za kupunguza magari madogo ya abiria (vipanya) kwa kusimamisha utoaji wa leseni ya kuingia katikati ya Jiji. Hatua hii imesaidia kuingiza mabasi makubwa katika usafiri wa umma Jijini Dar es Salaam, hatimaye kuboresha huduma. Takwimu zinaonyesha kuwa tangu utaratibu huu uanze, mabasi madogo yamekuwa yakipungua. Katika mwaka 2006 kulikuwa na mabasi madogo (Vipanya)

64

3,382 na mabasi makubwa 1,273 ikilinganishwa na mwaka 2009/2010 ambapo kuna mabasi madogo (Vipanya) 2,086 na mabasi makubwa 3,488.

76. Mheshimiwa Spika, mpango wa muda mrefu umezingatiwa katika utekelezaji wa mradi wa mabasi yaendayo kasi jijini Dar es Salaam (BRT). Kazi ya ulipaji fidia ya majengo na rasilimali zitakazoathiriwa na upanuzi wa miundombinu ya mradi wa mabasi ya usafiri wa haraka katika Manispaa za Ilala na Kinondoni imekamilika isipokuwa kwenye maeneo machache yaliyokuwa na malipo ya fidia ya nyongeza kutokana na malalamiko yaliyowasilishwa. Ulipaji fidia kwa eneo la Gerezani Kota unasubiri amri ya mahakama.

Serikali imeanzisha Mradi wa kuboresha na kuongeza mtandao wa barabara za Jiji ili kupunguza msongamano wa magari. Kwa kuanzia barabara zilizo katika mradi huu maalum ni; Jet Corner – Vituka Devis Corner (km 12.0), Ubungo Bus Terminal – Maziwa – Kigogo Round About (Km 6.4), Kigogo Round about – Jangwani - Twiga (km 2.7), Mbezi (Morogoro Rd.) – Malambamawili – Kinyerezi – Banana (km14), Old Bagamoyo - TPDC (Garden) road (km 9.1), Tangi Bovu hadi Goba (km 9.0), Kimara Baruti – Msewe - Changanyikeni (km 2.6), Kimara – Kilungule – External (Mandela Road 65

(km 9) na ukarabati wa mtaro mkubwa wa maji kuanzia Barabara ya Nyerere hadi barabara ya Uhuru. Kazi za ujenzi zimeanza katika barabara 3 nazo ni Jet Corner – Vituka Devis Corner (km 12.0), Ubungo Bus Terminal – Maziwa – Kigogo Round About (Km 6.4), Kigogo Round about- Jangwani- Twiga (km 2.7).

77. Mheshimiwa Spika, pamoja na kuwa idadi ya magari ya kusafirisha abiria mijini imeongezeka, bado idadi hiyo haikidhi mahitaji ya miji yetu ambayo inapanuka siku hadi siku. Kwa kuwa magari hayatoshi, hivyo yanachukua abiria wengi kuliko uwezo wake na kusababisha ajali. Katika mwaka 2010/11, Wizara itaendelea kusimamia utekelezaji wa Sera ya Uchukuzi na Sera ya Usalama Barabarani kwa kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji ili kuongeza idadi ya wawekezaji katika sekta ndogo ya usafiri na kuzuia ajali za barabarani.

Usalama Katika Miundombinu ya Uchukuzi.

78. Mheshimiwa Spika, sote tumeshuhudia mara kadhaa taifa letu likikumbwa na simanzi zinazosababishwa na majanga mbalimbali yanayotokea kwenye miundombinu yetu 66

na kuleta hasara kubwa. Baadhi ya majanga ambayo taifa letu haliwezi kuyasahau ni: lile la kuzama kwa meli ya MV Bukoba iliyotokea mwaka 1996 ambapo watu wengi walipoteza maisha na mali zao, ajali ya Treni Reli ya kati iliyotokea mwaka 2002 ambapo watu wengi walifariki na mali nyingi kupotea, kuporomoka kwa baadhi ya majengo kwenye miji mbalimbali nchini na ajali za barabarani zinazotokea mara kwa mara.

Aidha, kwa kipindi kirefu sasa tumeshuhudia matumizi yasiyo stahiki ya miundombinu yetu yanayosababisha uharibifu na uchafuzi wa mazingira hususan kwenye mtandao wa barabara, reli, usafiri majini na usafiri wa anga. Uharibifu wa miundombinu na uchafuzi wa mazingira licha ya kuwa ni mojawapo ya vyanzo vya ajali lakini pia huzorotesha ustawi wa jamii na kukuwa kwa uchumi wa taifa letu.

Ili kukabiliana na chagamoto hizi, katika mwaka 2009/10 Wizara iliunda rasmi Idara ya Usalama na Mazingira mahsusi kutatua matatizo ya uchafuzi wa mazingira na ajali katika sekta ya miundombinu ikiwa ni pamoja na kusimamia sera, sheria na kanuni husika za kitaifa na kimataifa.

67

79. Mheshimiwa Spika, naomba sasa nieleze kwa kifupi ukubwa wa tatizo la ajali, uchafuzi wa mazingira na uharibifu wa rasilimali katika sekta ya uchukuzi, usafirishaji na ujenzi.

Kwa upande wa ajali za barabarani, ajali zimekuwa zikiongezeka mwaka hadi mwaka licha ya juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali na wadau mbalimbali kutoka Jumuiya za Kitaifa, Kimataifa na Sekta binafsi. Ajali hizi zimeleta athari kubwa za kiuchumi na kijamii katika nchi yetu. Kwa mfano, mwaka 2007 watu 2,224 walipoteza maisha na watu 16,308 walijeruhiwa katika ajali 17,753 zilizotokea. Mwaka 2008 watu 2,429 walipoteza maisha na 17,861 walijeruhiwa katika ajali 20,615 zilizotokea, Mwaka 2009 watu 3,223 walipoteza maisha na watu 19,263 walijeruhiwa katika ajali 30,836 zilizotokea. Kwa wastani taifa hupoteza takriban asilimia 3 ya pato (GDP) lake kila mwaka kutokana na ajali za barabarani na takribani asilimia 2 kutokana na uharibifu wa miundombinu ya barabara.

80. Mheshimiwa Spika, tatizo la ajali za barabarani hapa nchini linaongezeka kwa kasi kutokana na sababu kuu zifuatazo:-

i. Uendeshaji mbaya, mwendo kasi, elimu duni na ufahamu mdogo wa sheria za usalama barabarani kwa watumiaji hususani

68

madereva, waendeshaji na wapandaji pikipiki, baskeli na watembea kwa miguu. ii. Ubovu wa vyombo vya usafiri unaotokana na matengenezo hafifu na vipuli duni yakiwemo matairi yasiyo kidhi viwango. iii. Dosari katika usanifu ujenzi na matengenezo ya miundombinu yasiyozingatia vigezo vya usalama. iv. Mapungufu katika sheria zilizopo na usimamizi wake. v. Ushirikiano hafifu wa wadau wa masuala ya usalama barabarani vi. Kuwepo kwa mafunzo duni ya udereva na utoaji leseni kiholela. vii. Uharibifu wa barabara kutokana na magari kuzidisha uzito. viii. Ulevi, uchovu (fatigue) na matumizi ya simu kwa madereva wakati wa kuendesha.

81. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/10 Wizara ilifanya mambo yafuatayo katika kukabiliana na changamoto zilizopo.

(i) Kuwahamasisha watumiaji mbalimbali wa barabara kuanzisha vyama/vikundi kama chama cha madereva wa malori, mabasi, wapanda pikipiki, wapanda baiskeli, chama cha shule za udereva n.k. Lengo ni 69

kurahisisha utoaji elimu na mafunzo. Vilevile wizara iliendelea Kuendesha warsha za kuelimisha vikundi hivi 1,250 vya watumiaji wa miundombinu ya usafiri katika mikoa ya Mwanza, Morogoro, Pwani na Dar es Salaam. (ii) Kusimamia utekelezaji wa sera ya usalama barabarani kwa kuandaa mikakati “road safety strategy, kuanza mchakato wa kuunda wakala, kutunga sheria mpya ijulikanayo kama Road “Traffic and Safety act”. (iii) Kuandaa, kuchapisha na kusambaza mitaala ya mafunzo ya shule za udereva, kanuni za barabara “Highway code”, miongozo ya udereva wanafunzi, miongozo ya alama za barabarani “a guide to traffic sign”. (iv) Kutoa elimu kwa umma kutumia Redio, Magazeti na luninga. (v) Kuandaa mafunzo ya ukaguzi wa usalama barabarani (Road Safety Audit) na kufanya ukaguzi kwa baadhi ya barabara ilikubaini kasoro zilizopo.

82. Mheshimiwa Spika, ili kuboresha masuala ya usalama barabarani na kulinda miundombinu ya barabara zetu, katika mwaka wa fedha 2010/2011 wizara yangu itaendelea kusimamia kikamilifu uzingatiaji na utekelezaji wa

70

sera ya usalama barabarani, kukamilisha sheria mpya ya usalama barabarani na kwa kupitia wakala wa barabara (Tanroads), wizara itaimarisha utendaji kwenye vituo vya mizani ili kudhibiti uharibifu wa barabara. Wizara itaandaa mpango kabambe wa ujenzi wa vituo vya mapumziko kwa madereva na wasafiri kwenye mtandao wa barabara zetu na kufanya maandalizi ya kujenga vituo cha kutahini madereva.

83. Mheshimiwa Spika, kuhusu usafiri wa reli, katika mwaka 2007 watu 43 walipoteza maisha na watu 23 walijeruhiwa katika ajali 111 zilizotokea. Mwaka 2008 watu 25 walikufa na watu 21 walijeruhiwa katika ajali 177 zilizotokea. Mwaka 2009 watu 32 walipoteza maisha na watu 20 walijeruhiwa katika ajali 158 zilizotokea.

Ili kuboresha usalama wa usafiri wa reli, Wizara itaimarisha ukaguzi wa miundombinu ya reli ya kati na reli ya TAZARA na ukaguzi na usimamizi wa mazingira ya reli zetu. Vilevile wizara inaendelea na jitihada za kuhakikisha kuwa mawasiliano katika sekta hii ya usafirishaji yanaimarika.

84. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa huduma za usafiri wa majini ajali zilizotokea mwaka 2007, zilihusisha watu 18 walipoteza maisha katika 71

ajali 11 zilizotokea. Mwaka 2008 watu 71 walipoteza maisha katika ajali 12 zilizotokea, na mwaka 2009 watu 35 walipoteza maisha katika ajali 13 zilizotokea.

Ili kuboresha usalama wa usafiri na usafirishaji majini, wizara inaendelea na mipango ya kuimarisha ukaguzi na usimamizi wa taasisi husika zilizo chini yake na utekelezaji wa sheria ya usafiri majini ya mwaka 2003 na nyingine zinazo husiana na kupunguza matukio ya ajali yanayojitokeza mara kwa mara hususani kwenye bandari zisizo rasmi. Wizara pia itaendelea na maandalizi ya kanuni ya kuzuia uchafuzi wa mazingira unaotokana na shughuli za uchukuzi majini.

85. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2007 zilijitokeza ajali za ndege 14 na mtu mmoja (1) alipoteza maisha na watu 3 kujeruhiwa. Mwaka 2008, ajali 15 zilitokea ambapo watu 12 walipoteza maisha na watu 5 kujeruhiwa. Katika mwaka wa 2009 ajali za ndege 15 zilitokea lakini hakuna mtu aliyepoteza maisha wala aliyejeruhiwa.

Kwa upande wa ajali za Ndege, Wizara itaendelea kushirikiana na Mamlaka ya Usafiri wa Anga, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege na Wadau wengine 72

na kufanya ukaguzi wa viwanja vyetu ili vilingane na viwango vya kimataifa. Aidha, Wizara itaendela kuongeza uwezo wa utendaji kazi kwa kutoa mafunzo kwa wote wanaohusika kwenye sekta hii ndogo ya usalama na mazingira.

86. Mheshimiwa Spika, tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa vyanzo vikuu vya ajali za barabarani, reli, maji na zile za anga zinatokana na mapungufu ya kibinadamu (human error), uchakavu na ubovu wa vyombo vya usafiri na dosari katika usanifu na ujenzi wa miundombinu yenyewe. Kwa upande wa ajali za barabarani. Mapungufu ya kibinadamu huchangia takriban asilimia 76, Ubovu na uchakavu wa magari unachangia takribani asilimia 16 ya ajali zote za barabarani zinazotokea nchini, na ubovu wa miundombinu huchangia takribani asilimia 8. Kwa upande wa reli mapungufu ya kibinadamu huchangia asilimia 21, reli yenyewe huchangia asilimia 29 na “rolling stolk” huchangia asilimia 50. Wakati usafiri wa anga mapungufu ya kibinadamu huchangia asilimia 73 Ubovu wa viwanja huchangia asilimia 16, hitilafu za ndege huchangia asilimia 5 na utabibu wa hali ya hewa na mengineyo huchangia asilimia 6. kwa upande wa usafiri wa majini tatizo kubwa ni uchafuzi wa mazingira, ubovu wa vyombo na ukiukwaji wa sheria, taratibu na kanuni za usafiri majini .

73

Kwa ujumla usafiri wa kutumia barabara huchagia zaidi ya asilimia 80 ya ajali zote zinazotokea kwenye sekta ya uchukuzi.

Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo na Matengenezo ya Barabara Kuu na Barabara za Mikoa

87. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2009/10, Wizara ilipanga kujenga barabara Kuu zenye urefu wa km 261.3 kwa kiwango cha lami na ukarabati wa km 111.8 kwa kiwango cha lami. Hadi kufika mwezi Machi 2010, jumla ya km 373 zilijengwa kwa kiwango cha lami na kukarabati km 60.3 kwa kiwango cha changarawe.

Jumla ya km 9,552.7 za barabara kuu na madaraja 1,026 yalipangwa kufanyiwa matengenezo mbalimbali. Kati ya kilomita hizo km 5,147.4 ni za barabara za lami na km 4,505.3 za barabara za changarawe. Hadi kufikia Machi, 2010 jumla ya km 8,216.5 zimefanyiwa matengenezo na madaraja 966 yametengenezwa. Kati ya barabara zilizofanyiwa matengenezo, km 3,737.3 ni za kiwango cha lami na km 4,479.2 ni za kiwango cha changarawe.

74

88. Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara za Mikoa, Wizara ilipanga kujenga jumla ya km 60.3 za barabara kwa kiwango cha lami, ukarabati wa km 1,006 kwa kiwango cha changarawe na ujenzi wa madaraja 13. Hadi kufikia Machi, 2010 jumla ya km 41.17 za lami zimejengwa, km 515.59 za changarawe zimefanyiwa ukarabati na madaraja 8 yamejengwa.

Kuhusu matengenezo ya barabara za mikoa pamoja na madaraja, Wizara ilipanga kutengeneza jumla ya km 19,210 za barabara na madaraja 1,207. Kati ya hizo, km 18,434 ni za udongo/changarawe na km 776.1 ni za lami. Hadi kufikia Machi, 2010 jumla ya km12, 202.8 za barabara za udongo/changarawe na km 481.7 za barabara za lami zimefanyiwa matengenezo mbalimbali.

89. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/10, Wizara imekabiliana na changamoto mbalimbali za kiutendaji. Changamoto hizo ni pamoja na uharibifu wa miundombinu ya usafiri hususan barabara na reli uliosababishwa na mvua zilizonyesha kati ya Disemba, 2009 na Januari, 2010 na hivyo kusababisha ongezeko la mahitaji ya fedha za matengenezo. Changamoto nyingine ni ufinyu wa bajeti ambao ulisababisha kushindwa kulipa Makandarasi kwa wakati pamoja na 75

kuchelewa kufanya malipo ya awali kwa miradi mipya iliyosainiwa Juni 2009, hivyo kusababisha kuchelewa kuanza utekelezaji wake.

90. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2010/11, Wizara kupitia TANROADS itaendelea kuzifanyia matengenezo Barabara Kuu, Barabara za Mikoa na Madaraja. Lengo ni kuzifanyia matengenezo mbalimbali barabara Kuu zenye urefu wa kilomita 10,345.5. Aidha, jumla ya madaraja1,221 yatafanyiwa matengenezo makubwa na ya kuzuia uharibifu. Kuhusu barabara za Mikoa, jumla ya km 20,153 zitafanyiwa matengenezo mbalimbali na madaraja 1,211 yamepangwa kufanyiwa matengenezo makubwa na ya kuzuia uharibifu.

91. Mheshimiwa Spika, miradi ya maendeleo itakayotekelezwa katika mwaka 2010/11 inajumuisha ukarabati wa jumla ya km 268.5 na kujenga km 634.2 kwa kiwango cha lami katika barabara Kuu. Madaraja kumi (10) yatakayoanza kujengwa ni Nanganga, Nangoo, Sibiti, Maligisu, Kilombero, Kavuu, Kagera, Ruhekei, Mbutu na Malagalasi.

76

Kwa upande wa barabara za Mikoa, miradi ya maendeleo itakayotekelezwa itahusu ukarabati kwa kiwango cha changarawe jumla ya km 1,350.9 na kujengwa kwa kiwango cha lami jumla ya km 98.55 na kujenga Madaraja 17. Kati ya km 1,350.9 zitakazokarabatiwa kwa kiwango cha changarawe, km 1,023.1 zitatumia mfuko wa maendeleo na km 327.8 zitatumia Mfuko wa Barabara. Aidha, kati ya km 98.55 zitakazojengwa kwa kiwango cha lami, km 68.55 zitagharamiwa na Mfuko wa Maendeleo na km 30.0 Mfuko wa Barabara. Kiambatanisho Na. 2.

Ushirikishwaji wa Wanawake katika Kazi za Ujenzi wa Miundombinu

92. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuhamasisha wanawake kushiriki kwa wingi katika kazi za ujenzi wa miundombinu ya uchukuzi nchini. Katika mwaka 2009/10, Wizara iliendesha mafunzo kwa wanawake mjini Tanga kuhusu namna ya kusimamia kazi za ujenzi wa barabara kwa kutumia teknolojia ya Nguvu Kazi. Washiriki katika mafunzo hayo walikuwa wanawake makandarasi kutoka mikoa ya Tanga, Pwani, Dar es Salaam, Kilimanjaro, Arusha na Kagera. Lengo ni kuwawezesha wanawake kuanzisha na kuendeleza Kampuni za ukandarasi na kushiriki kazi za matengenezo na ujenzi wa barabara kwa kutumia teknolojia ya 77

nguvu kazi. Wizara imeendelea kufuatilia utekelezaji wa mpango huu na kuendelea kuhamasisha wanawake kushiriki katika kazi za ujenzi wa miundombinu ya uchukuzi ili kujiongezea kipato na hivyo kupunguza umaskini.

93. Mheshimiwa spika, katika mwaka 2010/11, Wizara ina mpango wa kutekeleza kazi mbalimbali zikiwa ni pamoja na; kuendesha mafunzo ya Ukandarasi kwa Kampuni za wanawake 15, kuandaa miongozo ya ushiriki wa wanawake katika kazi za ujenzi wa miundombinu, kuhamasisha na kufuatilia maendeleo ya miradi inayotekelezwa na Kampuni zinazoendeshwa na wanawake.

USAFIRI NA UCHUKUZI MAJINI

Usafiri na Uchukuzi katika Maziwa

94. Mheshimiwa Spika, Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) imeendelea kutoa huduma ya uchukuzi wa abiria na mizigo katika Maziwa Makuu ya Tanganyika, Victoria na Nyasa. Katika mwaka wa fedha 2009/2010, jumla ya tani 123,279

78

zilisafirishwa ikilinganishwa na tani 137,938 zilizosafirishwa mwaka wa fedha wa 2008/2009 ikiwa ni pungufu kwa asilimia 11. Aidha, abiria 474,252 walisafirishwa katika mwaka 2009/10 ikilinganishwa na abiria 487,201 waliosafirishwa mwaka 2008/2009 ikiwa ni pungufu kwa asilimia 2.

95. Mheshimiwa Spika, MSCL inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na meli nyingi kuwa chakavu na hivyo kuchukua sehemu kubwa ya mapato yapatikanayo kwa matengenezo ya mara kwa mara na kusababisha ongezeko la matumizi ya mafuta. Kusimamishwa mara kwa mara kwa meli ya MV Umoja kutokana na kukosa mzigo kunakosababishwa na kupungua kwa mizigo inayosafirishwa kwa reli ya kati kumeathiri kwa kiasi kikubwa mapato ya kampuni.

Katika mwaka 2010/2011, Kampuni ya MSCL inatarajia kusafirisha jumla ya abiria 475,715 na mizigo tani 118,662, kuzifanyia matengenezo makubwa meli za MV Umoja, MV Victoria, MV Iringa, MV Songea na kukamilisha matengenezo ya MV Mwongozo iliyosimamishwa tangu mwaka 2008. Mpango mwingine wa Kampuni ni kuboresha usalama wa abiria na mali zao na kuweka bima za meli, abiria, mizigo na wafanyakazi.

79

96. Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua na kuthamini mchango wa sekta binafsi katika kutoa huduma za uchukuzi katika maziwa. Aidha, Serikali inazidi kuhamasisha sekta binafsi waendelee kutoa huduma kwa kufuata Sheria, kanuni na taratibu.

Usafiri na Uchukuzi Baharini

97. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2008/09, Kampuni ya Meli inayomilikiwa kwa pamoja na Serikali ya Tanzania na Jamhuri ya Watu wa China ijulikanayo kama SINOTASHIP, ilikuwa na meli mbili zenye uwezo wa kubeba tani 31,000 kwa pamoja. Kusuasua kwa mwenendo wa uchumi duniani, pamoja na uchakavu mkubwa wa meli zake kulisababisha SINOTASHIP kuamua kuuza meli zake mbili ili kulinda mtaji na kupunguza hasara. Hivyo, katika kipindi cha kuanzia Juni hadi Novemba 2009, Kampuni ilikuwa haina meli baada ya meli mbili zilizokuwepo kuuzwa. Aidha, katika kipindi hicho, SINOTASHIP ilikuwa ikiendelea na mpango wake wa ujenzi wa meli moja mpya yenye uwezo wa kubeba tani 57,000. Ujenzi wa meli hiyo ulikamilika Oktoba 2009 na kuanza kufanya kazi Disemba, 2009.

80

Katika kipindi cha kuanzia Disemba 2009 hadi Juni 2010, Kampuni iliweza kusafirisha jumla ya tani 150,000 ikilinganishwa na tani 148,590 zilizosafirishwa mwaka 2008 kwa kutumia meli mbili zilizouzwa kutokana na kuchakaa.

98. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa meli mpya ya pili yenye uwezo wa kubeba tani 34,000 unatarajiwa kukamilika mwaka 2011. Aidha, ili kuongeza mapato, katika mwaka 2010/2011, Kampuni itaelekeza nguvu zake katika kutafuta shehena inayosafirishwa kwa gharama kubwa na yenye masafa mafupi.

Udhibiti na Usalama wa Vyombo vya Majini

99. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia SUMATRA imeendelea kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Usafiri Majini ya mwaka 2003 kwa kuboresha ulinzi na usalama wa vyombo vya majini. Katika mwaka wa fedha 2009/2010, jumla ya vyombo vidogo 43 na vyombo 435 vyenye uzito wa zaidi ya tani 50 vilikaguliwa katika mwambao wa Bahari ya Hindi ili kubaini ubora wake. Aidha, jumla ya vyombo 1,382 vilikaguliwa katika Ziwa Viktoria, Tanganyika, Nyasa na Rukwa. Vyombo ambavyo havikukidhi viwango vya ubora vilielekezwa 81

kufanyiwa marekebisho kabla ya kupewa vyeti vya ubora na vyombo visivyotimiza kabisa masharti ya viwango vilivyowekwa vilisimamishwa kutoa huduma.

100. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha kuanzia Machi 2009 hadi April 2010, Kituo cha kuratibu shughuli za utafutaji na uokoaji cha Dar es Salaam kilipokea taarifa za dharura za vyombo vya majini zipatazo 17 ambazo zilitokea eneo la Tanzania. Katika matukio yaliyotolewa taarifa, watu wapatao 278 waliookolewa na 12 kupoteza maisha. Aidha, maiti 28 waliopolewa kutokana na ajali ya ndege ya Shirika la Ndege la Yemen (Yemeair).

101. Mheshimiwa Spika, pamoja na kuendelea na uratibu wa usalama wa vyombo vya uchukuzi nchini, SUMATRA pia imeendelea kudhibiti huduma za Makampuni yanayohudumia mizigo bandarini pamoja na Wakala wa Meli. Katika mwaka 2009/2010, kampuni 520 zinazoshughulikia huduma za mizigo bandarini zilisajiliwa ikilinganishwa na kampuni 588 zilizosajiliwa mwaka 2008/2009. Jumla ya leseni 32 za Uwakala wa Meli zilitolewa mwaka 2009. Aidha, SUMATRA imeendelea kushirikiana na Wadau wa Bandari katika kuhakikisha kuwa huduma zinaboreshwa na ufanisi wa bandari unaongezeka. 82

102. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011, SUMATRA itaendelea kukabiliana na ajali za majini kwa kuimarisha usimamizi wa usalama wa vyombo vya usafiri majini kwa kuvifanyia ukaguzi, kutoa elimu ya usafiri salama kwa wamiliki wa vyombo, waendeshaji wa vyombo vya usafiri majini, abiria na wadau wote.

Huduma za Bandari

103. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/2010, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) iliendelea na utekelezaji wa miradi mipya ya ujenzi wa miundombinu ya bandari na kufanya ukarabati wa miundombinu iliyochakaa ikiwa ni pamoja na kuibadilisha kulingana na mahitaji ya bandari. Lengo la kuboresha miundombinu na huduma za bandari ni kuweza kuhudumia shehena ya Tanzania na ya nchi jirani za Zambia, Malawi, Burundi, Rwanda na Uganda kwa ufanisi zaidi. Sekta binafsi imeendelea kushirikishwa katika kutekeleza miradi mikubwa.

104. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/2010, Mamlaka ya Bandari ililenga 83

kuhudumia tani za mapato milioni 6.98. Hadi Machi, 2010 jumla ya tani za mapato milioni 5.76 zilihudumiwa ikilinganishwa na lengo la kuhudumia tani za mapato milioni 5.32 kwa kipindi cha mwaka 2008/2009, na hivyo kuvuka lengo kwa asilimia 7.6.

Hadi Machi, 2010, TPA kupitia kitengo cha makasha kinachoendeshwa na TICTS kilihudumia shehena ya makasha (TEUs) 224,511 ikiwa ni pungufu ya lengo la kuhudumia makasha (TEUs) 249,300, upungufu huu ni sawa na asilimia 9.9. Sababu zilizochangia kushuka utendaji ni mlundikano wa makasha na msongamano wa meli uliokuwepo kati ya mwezi Julai hadi Disemba, 2009. Katika kukabiliana na hali hii, hatua za muda mfupi zilizochukuliwa ni pamoja na kuongeza vifaa vya kuhudumia meli na mizigo na kupanua maeneo ya kuhudumia mizigo ndani na nje ya bandari.

105. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/2010, Serikali imeondoa kipengele cha ukiritimba katika mkataba wa TICTS na hivyo kuruhusu meli za makasha kuhudumiwa pia katika vitengo vingine. Hatua hii imepunguza msongamano wa meli zinazosubiri kufunga katika bandari ya Dar es Salaam kwani hivi sasa meli tano zinaweza kuhudumiwa kwa wakati mmoja ukilinganisha na meli tatu hapo awali. Aidha, Serikali imebuni mikakati yenye lengo la kutoa ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la msongamano wa mizigo bandarini. 84

Mipango hiyo ni pamoja na kupanua bandari ya Dar es Salaam, kujenga bandari mpya za Bagamoyo na Tanga na kupanua bandari ya Mtwara.

106. Mheshimiwa Spika, kazi ya ujenzi wa magati sita (Kalya, Karema, Lagosa, Kirando, Kagunga na Kibirizi) katika ziwa Tanganyika iliyoanza kutekelezwa Disemba, 2009 na kubadilisha bomba la kupakulia mafuta ya aina mbalimbali ( Single Point Mooring – SPM) lililopo ndani ya bahari eneo la Kigamboni zinaendelea. Kazi ya ujenzi wa SPM inatarajiwa kuanza Julai 2010. Kazi nyingine zilizotekelezwa katika mwaka 2009/10 ni pamoja na: uondoshaji mchanga (maintenance dredging) katika gati Na. 1-11 na Gati la mafuta (Kurasini Oil Jetty - KOJ) katika bandari ya Dar es Salaam, uondoshaji mchanga katika bandari ya Tanga, ujenzi na upanuzi wa eneo la kuhudumia mizigo katika bandari ya Tanga, kuongeza maeneo ya kuhudumia shehena ya kontena kwa kusafisha na kukarabati maeneo ya iliyokuwa eneo la AMI na maeneo yaliyokuwa yakitumika kutunzia shaba katika bandari ya Dar es Salaam, uondoshaji mchanga (maintenance dredging) katika bandari ya Kigoma na ujenzi wa ghala la kuhifadhia shehena bandari ya Kasanga.

85

107. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011, miradi itakayotekelezwa ni pamoja na: ujenzi wa kituo kipya cha kuhudumia shehena ya makasha (Gati 13 & 14) bandari ya Dar es Salaam, kupanua na kuongeza kina cha lango la bandari na kuongeza kina cha gati Na. 1 – 7 bandari ya Dar es Salaam, mradi wa eneo la kuhudumia mizigo (CFS) Kisarawe, ujenzi wa kituo cha kuhudumia shehena ya mafuta cha SPM, ujenzi wa jengo la kuweka magari bandari ya Dar es Salaam, mradi wa uendelezaji wa Fukwe, ujenzi wa gati katika bandari ya Mafia, matengenezo ya eneo iliyokuwa NASACO, uboreshwaji wa Bandari ya Kasanga, ujenzi wa jengo la Bandari (One stop center), ununuzi wa vifaa vya kuhudumia shehena na Meli, ujenzi wa Gati la Kiwira, na upembuzi yakinifu wa ujenzi wa bandari mpya ya Mwambani na Bagamoyo.

Miradi mingine ni pamoja na kupanua bandari ya Mtwara ili kuiwezesha kuhudumia mizigo ya kichele na kontena, kukarabati bandari ya Kigoma , kuendeleza Bandari ya Mwanza na kukamilisha ujenzi wa gati sita katika Ziwa Tanganyika na ujenzi wa mtandao wa mawasiliano kwa bandari kuu na maziwa. Aidha, TPA itaendelea kuhakikisha kuwa huduma na utendaji wa bandari unakuwa wenye ufanisi zaidi.

108. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2010/2011, Mamlaka inalenga kuhudumia jumla ya 86

tani za mapato milioni 7.5 ikiwa ni ongezeko la asilimia 8.2 ya lengo la mwaka 2009/2010. Kitengo cha makasha (TICTS) kitahudumia makasha (TEUs) 340,100 ikiwa ni ongezeko la asilimia 4.9 ikilinganishwa na lengo la mwaka 2009/2010.

Usafiri na Uchukuzi wa Reli

109. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2009/10, TRL imekuwa ikitoa huduma ya usafiri wa abiria na mizigo kwa kiwango cha wastani. Kwa mfano, mwaka 2008/09, Kampuni iliweza kusafirisha tani 476,000. Hadi kufikia Novemba 2009, TRL iliweza kusafirisha tani 420,601 tu. Aidha, jumla ya abiria 59,000 walisafirishwa. Hadi kufikia mwezi Novemba 2009, jumla ya abiria 339,434 walisafirishwa. Hata hivyo, huduma za treni kuanzia Dar es Salaam na Dodoma zilizositishwa mwezi Disemba 2009 kutokana na mafuriko yaliyosababisha uharibifu mkubwa wa njia ya reli katika stesheni kati ya stesheni za Kilosa na Gulwe. Kazi ya dharura ya kurejesha miundombinu hiyo ilikamilika katikati ya mwezi Mei 2010 na huduma za treni ya mizigo ilianza baada ya ukaguzi wa njia kukamilika. Huduma za abiria zinatarajia kuanza mwishoni mwa mwezi Juni, 2010 baada ya kukamilika kwa matengenezo madogo madogo ya mabehewa na kufanyiwa ukaguzi na SUMATRA. 87

110. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011, TRL imepanga kufanya ukarabati wa injini 11 na mabehewa 107 ya mizigo. Mpango mwingine ni kuboresha miundombinu ya mawasiliano, ununuzi wa vifaa mbalimbali vitakavyotumika katika shughuli za utunzaji na matengenezo ya njia ya reli, mabehewa na injini.

111. Mheshimiwa Spika, kazi ya kufanya upembuzi yakinifu wa kuboresha reli kati ya Dar es Salaam na Isaka ilikamilika Septemba, 2009. Reli za tani 12,000 zinazotosheleza kubadili km 150 za njia ya reli kati ya Dodoma na Tabora zimekwishapokelewa. Aidha, mataruma yanayotosheleza km. 80 yamewasili nchini. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kununua mataruma ya km 70 zilizosalia.

Ujenzi wa vituo vya kuhifadhi makasha (ICDs) vya Ilala, Shinyanga na Mwanza unaendelea na mashine za kupakia na kupakua makasha (Reach stackers) tatu (3) zimewasili nchini na kupelekwa katika vituo vya Ilala na Shinyanga. Mashine mbili (2) za kupakia na kupakua mizigo zinatarajiwa kuwasili nchini mwaka 2010/11 kwa ajili ya kituo cha Mwanza

88

112. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/11, RAHCO imepanga kufanya usanifu wa kina (detailed engineering design) wa kuboresha reli ya Dar es Salaam – Isaka na usanifu wa kina wa ujenzi wa reli mpya kati ya Isaka– Kigali/Keza - Gitega – Musongati kwa kiwango cha “Standard Gauge”. Kazi nyingine zitakazotekelezwa ni ubadilishaji wa kilometa 150 za reli kati ya Dodoma na Tabora, ukamilishaji wa ujenzi wa vituo vya kuhifadhi makasha vya Shinyanga na Mwanza, kutafuta mbia kwa ajili ya ujenzi wa mtandao wa mawasiliano (fibre optic cable network) kati ya Tabora na Kigoma na Tabora na Mwanza.

RAHCO pia ina mpango wa kuanzisha Mfuko wa Miundombinu ya Reli (Railway Infrastructure Fund) chini ya sheria ya Reli ya mwaka 2002 kwa ajili ya uendelezaji wa miundombinu ya reli nchini.

113. Mheshimiwa Spika, hali ya miundombinu ya reli ya TAZARA kwa mwaka 2009/2010 ilikuwa inaridhisha ingawa utekelezaji wa mpango wa matengenezo ya reli ulikuwa duni. Katika kipindi cha nusu mwaka cha 2009/2010, kulikuwa na maeneo 23 yaliyowekewa tahadhari ya kupunguza mwendo wa treni. Sehemu nyingi za maeneo hayo ni zile zilizoharibika kutokana na ajali na mmomonyoko wa udongo. Aidha, vifaa vingi vya kufanyia kazi havikuwa katika hali nzuri kutokana na ukosefu wa fedha. 89

Kwa upande wa mawasiliano na ishara, TAZARA imeimarisha huduma hii kwa kutumia teknolojia ya nyaya aina ya Microwave, optic fibre na High Frequency Radio. Mamlaka imeendelea kukarabati njia za reli, mabehewa na injini ili kuimarisha usalama wa abiria, mizigo na vyombo vyenyewe.

114. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/2010, Mamlaka Reli Tanzania na Zambia (TAZARA) ilipanga kusafirisha jumla ya tani 600,000 za mzigo. Hadi kufikia Mei, 2010, TAZARA ilisafirisha tani 474,832 za mizigo ambazo ni wastani wa tani 43,167 kwa mwezi sawa`na asilimia 79 ya lengo. Mamlaka ilisafirisha abiria 695,867 ambao ni wastani wa abiria 63,260 kwa mwezi. Kiwango cha kusafirisha abiria kimeshuka kwa asilimia 4 ya lengo kutokana na uhaba wa injini, mabehewa na fedha za uendeshaji.

115. Mheshimiwa Spika, changamoto zinazoikabili TAZARA ni pamoja na uhaba wa fedha za uendeshaji. Uhaba huu umeathiri utendaji kiasi cha kushindwa kufanya matengenezo ya injini za treni na mabehewa. Aidha, uhaba wa fedha umeathiri kwa kiasi kikubwa ukarabati wa miundombinu hususan upande wa Tanzania na hivyo, kusababisha kuwekwa kwa vidhibiti mwendo katika sehemu zilizoathirika. 90

Ili kutatua changamoto hizi, katika mwaka wa fedha 2010/11, Serikali za Tanzania na Zambia zitabeba jukumu la ukarabati wa miundombinu, injini na mabehewa kupitia bajeti za Wizara husika. Mpango mwingine ni kuirudishia TAZARA makato yanayofanywa na TRA kama kodi kutokana na ununuzi wa mafuta ya TAZARA, Serikali za Tanzania na Zambia kubeba madeni mbalimbali ya TAZARA hususan yale ya kisheria ili kuiwezesha kukopesheka na kufanya kazi kibiashara zaidi pamoja na kufanya tathmini ya kitaalam kwa ajili ya kushirikisha sekta binafsi kuendesha TAZARA.

116. Mheshimwa Spika, katika mwaka wa fedha 2010/11, TAZARA inatarajia kubadilisha mataruma mabovu ya mbao 10,158 na kufunga mengine katika madaraja 322, kurudishia vyuma vya madaraja vilivyoibwa kutokana na kukithiri kwa biashara ya vyuma chakavu, kupaka rangi na kuchomea jumla ya madaraja 276 kwa upande wa Tanzania kutokana na kutu na kukarabati ‘culverts’ zilizoharibiwa na mvua katika maeneo ya Kurasini na Yombo.

91

Udhibiti wa Huduma za Usafiri wa Reli

117. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2009/10, SUMATRA imeendelea kudhibiti na kusimamia usalama, ubora wa huduma na udhibiti wa kiuchumi wa usafiri wa reli nchini. Katika kipindi cha kuanzia mwaka 2005/06 hadi 2009/10, SUMATRA ilifanya ukaguzi wa mabehewa 23 ya abiria na injini 6 zilizoingizwa nchini na TRL kutoka India. Aidha, SUMATRA ilifanya ukaguzi wa miundombinu ya reli, vifaa na huduma kutoka Dar es Salaam, Mwanza na tawi la kuelekea Mpanda. Upungufu uliodhihirika katika ukaguzi huo ni matengenezo yasiyoridhisha ya njia ya reli, baadhi ya maeneo kutokuwa na mawasiliano, uchakavu wa mabehewa na TRL kushindwa kutekeleza mkakati wa usalama. TRL walipewa maelekezo ya kurekebisha upungufu huo na SUMATRA iliandaa semina ya mafunzo kuhusu namna ya kukabiliana na makosa ya kibinadamu.

Kwa upande wa TAZARA, SUMATRA ilikagua mabehewa 100 yaliyoingizwa nchini kutoka China na kufanya ukaguzi wa miundombinu, vifaa na huduma za TAZARA kuanzia Dar es Salaam hadi Tunduma. Upungufu uliojitokeza ni hali mbaya ya mabehewa, mawasiliano mabovu, upungufu wa wafanyakazi wenye ujuzi na vitendea kazi. TAZARA walipewa maelekezo ya kurekebisha upungufu uliojitokeza. 92

118. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/11, SUMATRA inatarajia kufanya ukaguzi na tathmini ya usafiri wa reli kwa ajili ya kuimarisha usalama na ubora wa huduma, kuendelea kudhibiti gharama za watoa huduma, kufanya tafiti kwa ajili ya kuboresha huduma, kutoa mafunzo ya udhibiti na usimamizi na kutoa elimu ya ukimwi kwa wafanyakazi wake.

Usafiri wa Anga

119. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/2010, Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kupitia idara yake ya Huduma ya Uongozaji Ndege (ANS) ilifanikiwa kupata cheti cha Kimataifa cha ubora cha ISO 9001:2008 na hivyo kuweka rekodi ya kuwa taasisi ya pili kusini mwa jangwa la Sahara baada ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Afrika Kusini.

120. Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza katika hotuba yangu ya mwaka 2009/2010, Mamlaka ya Usafiri wa Anga ilikuwa inaendelea na ujenzi wa jengo la Makao Makuu eneo la Ukonga. Napenda kulifahamisha Bunge lako tukufu kwamba 93

ujenzi wa jengo hilo unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2010 na ofisi za Makao Makuu ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga zilizokuwa katika majengo ya kukodisha katikati ya Jiji la Dar es Salaam zitahamia katika jengo hilo jipya.

121. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha nusu mwaka wa 2009/10, abiria wanaotumia usafiri wa anga wanatarajiwa kufikia 2,963,916, ikilinganishwa na abiria 2,791,381 waliotumia usafiri wa anga mwaka 2008/09, ikiwa ni ongezeko la asilimia 6.1. Aidha, usafiri wa mizigo kwa kipindi hicho unatarajiwa kupungua kutoka tani 29,919 hadi tani 27,279, ikiwa ni upungufu kwa asilimia 8.8 kutokana na mtikisiko wa uchumi Duniani.

Katika mwaka 2010/2011, sekta hii inatarajiwa kukua kidogo kutoka abiria 2, 963,916 hadi abiria 3,082,472, ikiwa ni ongezeko la asilimia 4. Aidha, safari za ndege (aircraft movements) zinarajiwa kukua kwa asilimia 5 kutoka safari 175,247 mwaka 2009/10 hadi 185,366 mwaka 2010/11. Kukua huku kunatokana na ahueni itakayopatikana kwa jinsi dunia inavyokabiliana na mtikisiko wa uchumi. Huduma ya mizigo, inakadiriwa kuongezeka kutoka tani 27,279 hadi 28,370, ikiwa ni ongezeko la asilimia 4. Hii inatokana na juhudi zinazofanywa za kuwahamasisha watoa huduma hizo kufanya safari za kuja nchini kwetu. Mizigo mingi, hasa maua na

94

samaki, bado husafirishwa kwa barabara kutoka Tanzania hadi Kenya, kabla ya kusafirishwa kwenye masoko ya Ulaya.

122. Mheshimiwa Spika, katika juhudi za kuimarisha usalama wa anga, mtambo unaosaidia Marubani kupata taarifa za mwelekeo na umbali wa ndege (VHF Omni-directional Radio Range and Distance Measuring Equipment) tayari umesimikwa katika Kiwanja cha Ndege cha Mwanza na umeanza kufanya kazi tangu Disemba 2009, na hivyo kuleta faraja kwa marubani wa ndege. Kuwepo kwa mtambo huu katika Kiwanja cha Ndege cha Mwanza, kumeimarisha kiwango cha hali ya usalama katika anga kwenye kanda ya Ziwa Viktoria, hata kwa ndege zipitazo bila kutua katika Kiwanja cha Mwanza (over fly) kwenda nchi za Burundi, Kenya, Rwanda, Uganda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Kongo (DRC), Afrika Kusini, Sudan na nyinginezo.

123. Mheshimiwa Spika, Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL) imeendelea kutoa huduma za usafiri wa anga kwa kutumia ndege zake mbili aina ya Dash 8-Q300 na kurudisha ndege aina ya Boeing 737-200 iliyokuwa kwenye matengenezo makubwa nchini Msumbiji. Aidha, ATCL bado imeendelea kukabiliwa na matatizo makubwa ya kifedha na kimenejimenti kiasi cha kuathiri huduma zake. 95

124. Mheshimiwa Spika, katika kipindi 2009/2010, Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) umeendelea kutoa huduma za usafiri kwa viongozi wakuu wa kitaifa na Serikali kwa ujumla. Wakala wa Ndege za Serikali umehakikisha kuwa Ndege zake zote nne, zinafanyiwa matengenezo makubwa na ya kawaida hapa nchini na nje ya nchi.

Katika kipindi cha Julai 2009 hadi Februari 2010, Wakala umeweza kukusanya madeni ya kiasi cha shilingi bilioni 2.8 ambacho ni kati ya madeni ya kiasi cha shilingi bilioni 7.9 inayodai. Wakala umeweza kufanya malipo mbalimbali yakiwemo ya vipuli vya ndege kwa asilimia 80 kulingana na fedha zilizotolewa kwa Wakala. Kwa mantiki hiyo wakala umekuwa na uwezo wa kukopeshwa (credit worth) kutoka kwa watoa huduma (Manufacturers and Suppliers). Katika kipindi cha kuanzia Julai, 2005 hadi Mei, 2010, Wakala umeweza kupata mapato ya shilingi billioni 22.0 yaliyotokana na ukodishaji wa ndege za Serikali ikilinganishwa na kiasi cha shilingi billioni 28.0 kilichokadiriwa kukusanywa.

125. Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio yaliyopatikana, Wakala ulikabiliwa na changamoto mbalimbali. Changamoto hizo ni

96

pamoja na ufinyu wa bajeti ukilinganisha na mahitaji na uhaba wa Marubani. Ili kukabiliana na changamoto hizo, Wakala uliendelea na mafunzo ya marubani na wahandisi pamoja na watumishi wengine.

Katika kipindi cha 2010/11, Wizara kupitia Wakala itaendelea kuboresha huduma za usafiri wa anga kwa Viongozi Wakuu wa Kitaifa na kuziandaa ndege zetu kuwa tayari kwa safari wakati wowote zitakapohitajika. Wakala utaendelea kudumisha na kuboresha usalama wa ubora wa huduma kwa kufuata taratibu zilizopo kwenye mkataba wa huduma kwa mteja. Wakala pia utaendelea kuwapeleka watumishi katika mafunzo ya ndani na nje ya nchi ili kuwaongezea uwezo wa kufanya kazi zao kwa tija na ufanisi zaidi.

126. Mheshimiwa Spika, katika Kiwanja cha Ndege cha Julius Nyerere Mamlaka ya Usafiri wa Anga imefunga mashine ya kisasa itwaayo “Multi- Channel Digital Voice and Data Logger’ ambayo husaidia kupata taarifa za uchunguzi wa kubaini kiini cha ajali za ndege mara zinapotokea. Katika mwaka 2010/11, vifaa kama hivi vitafungwa katika viwanja vya ndege vya Arusha, Mwanza na . Ufungaji wa mitambo ya mawasiliano ya VHF ili kuimarisha huduma za uongozaji ndege utafanyika 97

katika viwanja vya ndege vya Dodoma, Mbeya, Songea, Mtwara, Tabora na Arusha. Aidha, Mamlaka ya Usafiri wa Anga itatekeleza Mpango unaoratibiwa na Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga Duniani (ICAO) ujulikanao kama “safety management system’ wenye lengo la kudhibiti na kuondoa vitendo vinavyoweza kusababisha ajali.

127. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/2010, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) iliendelea kuhudumia viwanja vya ndege kwa kuzingatia sera ya Taifa ya Uchukuzi ambayo inasisitiza viwanja vya ndege kujiendesha kibiashara, kujitosheleza kwa mapato na kujitegemea. Miongoni mwa mambo muhimu ambayo Mamlaka iliendelea kuyafanya ni pamoja na matengenezo ya kawaida ya viwanja vya ndege ili kuwezesha ndege kutua na kuruka kwa usalama.

128. Mheshimiwa Spika, Mamlaka iliendelea na mkakati wa kuandaa mazingira mazuri ya kibiashara katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Julius Nyerere ili kiwe kiungo (hub) cha usafiri wa anga kitaifa, kikanda na kimataifa. Baadhi ya kazi zinazoendelea kufanyika ni pamoja na utekelezaji wa awamu ya pili ya ukarabati na ujenzi wa barabara za viungio na maegesho, barabara ya kuruka na kutua ndege, kuweka taa za kuongozea 98

ndege, ukarabati wa maegesho ya ndege ya Terminal I, maegesho ya ndege za mizigo (Cargo Apron) pamoja na kazi/huduma zinazohusiana na masuala ya mazingira, ujenzi wa Jengo jipya la watu mashuhuri (VIP Lounge) eneo la Terminal II na usanifu wa ujenzi wa jengo jipya la abiria (Terminal III), usanifu wa ujenzi wa jengo jipya la mapokezi ya ugeni wa kitaifa (State Reception Building).

129. Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kuimarisha na kuboresha huduma za viwanja vya ndege nchini, Serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini imeanza mchakato wa maandalizi ya awamu ya pili ya ukarabati na uboreshaji wa kiwanja cha Mafia kwa kiwango cha lami chini ya ufadhili wa “Millenium Challenge Corporation”. Kuhusu kiwanja cha Ndege cha Mwanza, Mamlaka inafanya mapitio ya mwisho ya usanifu wa uboreshaji wa miundombinu ya kiwanja hiki. Aidha, mchakato wa kutangaza zabuni umeanza.

130. Mheshimiwa Spika, kuhusu kiwanja cha ndege cha Arusha, Mamlaka imekamilisha ukarabati wa barabara ya kuruka na kutua ndege, maungio na maegesho kwa asilimia 95. Kazi ya ukarabati wa barabara ya kutua na kurukia itakamilika katika mwaka 2010/11. Serikali pia itakarabati barabara za kutua na kuruka kwa 99

kiwango cha lami katika viwanja vya ndege vya Mpanda, Bukoba, Kigoma na Tabora.

Katika kiwanja kipya cha Kimataifa cha Msalato Dodoma, Mamlaka imekamilisha kazi ya kuthamini mali, ulipaji wa fidia, upembuzi yakinifu na usanifu wa awali kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja pamoja na kusawazisha eneo la kiwanja na kuweka mipaka ya eneo la kiwanja.

131. Mheshimiwa Spika, kuhusu Ujenzi wa Kiwanja cha ndege cha Songwe, Mamlaka imeendelea na awamu ya tatu na ya mwisho ya kumalizia ujenzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege pamoja na viungio vyake kwa kiwango cha lami kujenga mfumo wa kuondoa maji ya mvua kiwanjani (drainage works), ujenzi wa jengo la abiria (badala ya lile la awali ambalo litatumika kwa matumizi ya ofisi), ununuzi na ufungaji wa: “X – ray machine” kwa ajili ya ukaguzi, Samani za jengo la abiria, Mifumo ya kurahisisha utoaji wa mizigo kutoka kwenye ndege (conveyor belts), mtambo wa umeme wa dharura (generator), mitambo ya hali ya hewa na “Public Address System’; na ujenzi wa miundombinu ya kuvuta na kusafisha maji ‘(Water Supply and Treatment works). Mamlaka inaendelea pia na juhudi za kupata hati (Title Deeds) kwa maeneo mapya kwa ajili ya viwanja vipya vya ndege. 100

Maeneo hayo ni Bagamoyo (Pwani), Omukajunguti (Kagera), Kisumba (Sumbawanga), Msalato (Dodoma) na Ngungungu (Manyara). Aidha, Wizara kupitia TAA itafanya tathmini ya maeneo mapya yaliyoainishwa katika mikoa ya Mara na Singida kwa ajili ya ujenzi wa viwanja vipya.

132. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2010/2011, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege itaendelea na ujenzi wa uzio wa viwanja vya ndege vya Mafia, Ziwa Manyara na Dodoma, kununua vifaa vya usalama, “X- ray machines” kwa viwanja vya JNIA (3), Mtwara, Dodoma, Mwanza na Arusha. Kununua “Walk Through Metal Detectors” kwa viwanja vya JNIA, Arusha, Mtwara, Tanga, Dodoma,Tabora, Kigoma, Mafia na Mwanza, kununua “Hand held metal detectors” pamoja na kutoa mafunzo mbalimbali ya namna ya kukabiliana na vitisho vya kigaidi kwa viwanja vyote vya ndege vyenye ratiba maalum. Viwanja vya ndege vilivyobaki vitaendelea kuboreshwa na Mamlaka ya viwanja vya ndege kwa kutumia vyanzo vyake vya mapato.

133. Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio niliyoyataja hapo juu, Mamlaka ilikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na uwezo mdogo wa kifedha (bajeti) ikilinganishwa na 101

mahitaji makubwa ya ukarabati na uendelezaji wa miundombinu ya viwanja. Kutokana na ufinyu wa bajeti ya Serikali, miradi mingi huchukua muda mrefu kukamilika na kwa gharama kubwa zaidi.

Changamoto nyingine ni vitisho vya matukio ya vitendo vya kigaidi na uhalifu dhidi ya usafiri wa anga duniani na hivyo kuhitaji umakini na gharama kubwa katika masuala ya ulinzi na usalama katika viwanja vya ndege. Kukosekana kwa elimu na mwamko wa usalama wa usafiri wa anga kwa watumiaji wa viwanja vya ndege huleta misuguano mingi ya kiutendaji. Kukua na mabadiliko ya kasi katika matumizi ya teknolojia mpya katika usafiri wa anga duniani ambayo yanahitaji uwezo mkubwa wa uwekezaji katika miundombinu na huduma za viwanja vya ndege.

134. Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na changamoto zilizotajwa hapo juu, Serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania inaendelea na juhudi za kushirikisha Sekta Binafsi (PPP) katika uendeshaji, uendelezaji, na upanuzi wa huduma za viwanja vya ndege. Viwanja vya ndege 16 vimepata kipaumbele katika Mpango wa Kitaifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Uchukuzi “Transport Sector Investment Programme”, Viwanja hivyo ni JNIA, Arusha, Mwanza, Lake Manyara, Mafia, Mtwara, 102

Tabora, Bukoba, Dodoma, Kigoma, Moshi, Shinyanga, Musoma, Tanga, Singida, na Songwe. Jitihada zinaendelea chini ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) pamoja na mashirika mengine ya kimataifa (WB, BADEA, ORET, OPEC, JICA, ADB, IFC) ili mpango huo uweze kupatiwa fedha za utekelezaji.

Huduma za Hali ya Hewa

135. Mheshimiwa Spika, huduma za hali ya hewa zimeendelea kuboreshwa ili zifikie matarajio ya watumiaji wa huduma hizo. Katika mwaka 2009/10, sekta zilizonufaika na huduma hizo ni pamoja na Uchukuzi, Kilimo, Maji, Mazingira, Ujenzi na tahadhari kwa Umma dhidi ya majanga yatokanayo na mabadiliko ya mwenendo wa hali ya hewa.

Katika mwaka wa fedha 2010/11, Mamlaka itaendelea kuboresha huduma za hali ya hewa ili kukidhi mahitaji ya wananchi na pia sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii. Ujenzi wa kituo cha Radar ya hali ya hewa ambacho kinajengwa Dar es Salaam kinatarajiwa kukamilika na kuanza kufanya kazi mwezi Agosti, 2010. Aidha, Mamlaka itanunua Radar ya pili ya hali ya hewa inayotarajiwa kufungwa mkoani Mwanza na hivyo kuongeza 103

usahihi wa taarifa za hali ya hewa pamoja na tahadhari juu ya matukio ya hali mbaya ya hewa.

Mamlaka pia itaendelea kuboresha vituo vyake kwa kununua vifaa vya kisasa vya hali ya hewa. Katika kuhakikisha taarifa za hali ya hewa hususani utabiri zinawafikia walengwa, Mamlaka inatarajia kuboresha studio zake za kutayarishia taarifa hizo.

Ili kufikia malengo ya utekelezaji wa mradi wa uhakiki wa ubora wa viwango vya kutoa huduma za hali ya hewa kwa usafiri wa anga (Quality Management System), Mamlaka itanunua mitambo ya hali ya hewa ikiwemo “pressure calibration unit”.

136. Mheshimiwa Spika, Mamlaka pamoja na kupata mafanikio hayo bado inakabiliwa na baadhi ya changamoto ikiwemo upungufu wa Bajeti, uchache wa vituo vya kupimia hali ya hewa, uhaba na uchakavu wa mitambo na vifaa, maslahi duni kwa wafanyakazi, ujenzi wa Makao Makuu ya Mamlaka na Kituo Kikuu cha Utabiri, kukosekana kwa sera na sheria ya utoaji wa huduma kwenye sekta ya hali ya hewa.

104

Ujenzi wa Nyumba za Viongozi na Watumishi wa Umma

137. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2009/10, Serikali kupitia Wakala wa Majengo (TBA), iliendelea kutoa huduma za ushauri na kusimamia ujenzi wa nyumba za Viongozi na watumishi wa umma, ujenzi na ukarabati wa majengo ya ofisi za Serikali, kuweka samani katika nyumba za viongozi pamoja na kushughulikia migogoro na shughuli mbalimbali zinazohusu majengo, hususan nyumba na majengo ya Serikali.

Nyumba zilizoanza kujengwa ni kama ifuatavyo: Jijini Dar es Salaam (2), Tabora (1), Mwanza (1), Iringa (1), Arusha (1), Mbeya (1), Songea (1), Urambo (1), Tanga (1) na Dodoma (1). Nyumba za viongozi zilizoanza kujengwa ni Arusha (2), Ukerewe (2), Bahi (2), Kigoma (1), Sumbawanga (1), Mafia (1) na Mvomero (1). Miradi hii ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Aidha, Wakala wa Majengo unaendelea na ukamilishaji wa majengo matatu ya ghorofa yanayojengwa kwa ubia jijini Dar es Salaam kwa ajili ya biashara.

138. Mheshimiwa Spika, kazi za ukarabati na uboreshaji wa makazi ya nyumba za viongozi 105

nchini imeendelea kufanyika. Katika mwaka 2009/10 uboreshaji na ukarabati wa nyumba 81 za viongozi zilizojengwa maeneo ya Mikocheni, Kijitonyama na Msasani Penninsular unaendelea kutekelezwa. Kazi nyingine za ukarabati zilizotekelezwa ni pamoja na ukarabati wa Ghorofa moja (Ngano Street) lenye makazi 3 jijini Dar es salaam. Nyingine ni majengo katika miji ya Iringa (1), Tabora (1), Dodoma (1), Lindi (3), Mwanza (3), Lushoto (1), Tanga (1), Mafia (1) na Musoma (2).

139. Mheshimiwa Spika, Wakala wa Majengo umeendelea pia na kazi ya ujenzi wa nyumba kwa ajili ya Watumishi wa Serikali nchini. Miradi iliyoainishwa kutekelezwa katika mwaka 2009/10, ilihusu ukamilishaji wa nyumba 60 za watumishi katika mikoa yote Tanzania Bara pamoja na ujenzi wa majengo ya iliyokuwa NMC Mbezi beach Dar es Salaam. Aidha, ujenzi wa Ofisi za TBA Makao Makuu, mkoa wa Manyara na Pwani, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Bariadi, ujenzi wa Zahanati katika nyumba za viongozi Mwangaza Dodoma, ukarabati na uhifadhi wa Jengo la Boma la kale Bagamoyo na ukarabati wa Ikulu ndogo Mafia – Pwani unaendelea.

140. Mheshimiwa Spika, Wakala pia ulikamilisha umiliki wa viwanja 429 vilivyopatikana 106

pamoja na eneo la eka 635 lililopatikana Mjini Dodoma litakalopimwa viwanja kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za Watumishi.

141. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/11, Serikali kupitia TBA itaendelea na ukamilishaji wa miradi ya ujenzi na ukarabati wa nyumba zilizokwisha anza kama zilivyoainishwa hapo juu pamoja na kuanza ujenzi wa nyumba mpya 16 kwa ajili ya viongozi nchini wakiwemo Waheshimiwa Majaji.

TBA inategemea kuanza ujenzi wa nyumba nyingine 5 katika kila mkoa Tanzania bara kwa ajili ya watumishi wa umma, ununuzi wa nyumba za iliyokuwa NASACO, NIC, ujenzi wa nyumba 25 za Watumishi Bunju Dar es Salaam pamoja na kukamilisha upatikanaji na umiliki wa viwanja katika sehemu mbalimbali nchini kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA)

142. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2009/10, TEMESA imeendelea na majukumu yake ya msingi ambayo ni kutengeneza magari na mitambo, ukaguzi na ukarabati wa mifumo ya 107

umeme katika nyumba za Serikali, elektroniki, viyoyozi na mabarafu. Wakala pia umeendelea kutekeleza miradi ya kutoa ushauri wa kitaalam (Consultancy services) katika usimikaji wa mifumo ya elekroniki, viyoyozi na mabarafu.

143. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea na mkakati wa kuimarisha vivuko katika maeneo mbalimbali yanayohitaji huduma hiyo. Katika mwaka wa fedha wa 2009/10, Wizara imekamilisha ununuzi wa Kivuko cha Mto Pangani (Tanga), ukarabati wa MV Kigamboni (Dar es Salaam) na MV Sengerema (Mwanza). Vivuko hivi vimekabidhiwa Serikalini na kuanza kutoa huduma chini ya uendeshaji wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA). Kukamilika kwa vivuko hivi ni hatua nzuri katika kuboresha huduma ya usafiri wa vivuko kwa wananchi katika maeneo husika hivyo kurahisisha utekelezaji wa shughuli zao za maendeleo. Aidha, vivuko vya Utete (Rufiji), Rugezi- Kisorya (Mwanza) na Musoma-Kinesi (Mara) vinaendelea kujengwa na vitakamilika Septemba 2010.

144. Mheshimiwa Spika, changamoto zilitojitokeza katika utekelezaji wa majukumu hayo ni pamoja na uchakavu wa karakana na ukosefu wa

108

vitendea kazi vya kisasa. Wakala unaendelea na juhudi za kupunguza matatizo haya kwa awamu.

145. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2010/11, Wizara kupitia TEMESA imepanga kutengeneza magari 9,144. Aidha, Wakala utaendelea na Mpango wake wa ukarabati wa karakana na kuzipatia vitendea kazi vya kisasa na kuendelea kusimamia uendeshaji na matengenezo ya mara kwa mara ya vivuko vyote nchini ili viendelee kutoa huduma bora na salama. Pia Wakala utaendelea kutoa ushauri wa kiufundi kwa miradi ya matengenezo ya mifumo ya umeme, mitambo, elektroniki, viyoyozi na mabarafu katika majengo ya Serikali ikiwa ni pamoja na ukodishaji wa mitambo na magari maalum kwa Viongozi.

146. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2010/11, Wizara imepanga kukamilisha ununuzi wa vivuko vipya vyenye uwezo wa tani 50 kila kimoja vya Msanga Mkuu (Mtwara), Rusumo (Kagera), Itungi Port (Kyela) na Kilambo (Mtwara) kitakachotoa huduma kati ya Tanzania na Msumbiji.

Wizara itaendelea kujenga maegesho (ramps) katika vivuko vya Nyakaliro-Kome, Msanga Mkuu na 109

Rusumo ili kuwezesha abiria na magari kupanda na kushuka kwenye vivuko kwa urahisi nyakati zote za mwaka. Pia Wizara itafunga mashine za kukatia na kutambua tiketi zitakazotumia mfumo wa kompyuta katika Kivuko cha Kigamboni ili kurahisisha upatikanaji wa tiketi na utunzaji sahihi wa takwimu za mapato.

Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC)

147. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/2010, Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) limeendelea kuratibu ushirikishwaji wa sekta binafsi ili iweze kushiriki kikamilifu katika masuala ya ujenzi nchini. Aidha, NCC imeendelea kutekeleza Sera ya Ujenzi kwa kupitia Sheria ya Manunuzi ya Umma ya 2004 ambayo inatoa upendeleo katika utoaji wa Kandarasi na huduma kwa Watanzania.

148. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2010/11, Baraza limepanga kutoa msukumo katika utekelezaji wa Sera ya Ujenzi, kubuni na kutekeleza mikakati ya ukuzaji ubora na tija, kuandaa kanuni za utekelezaji wa Sheria iliyoanzisha Baraza na kuboresha utendaji kazi wa sekta ya ujenzi isiyo rasmi. Aidha, Baraza limepanga kuratibu na kutoa mafunzo, kufanya ukaguzi wa 110

kiufundi (technical audit), kutoa ushauri wa kiufundi na kutatua migogoro katika sekta ya ujenzi na kufanya tafiti zitakazowezesha kubaini matatizo. Baraza pia litaendelea kutafuta kazi mbalimbali na kuendesha mafunzo na huduma za ushauri zitakazosaidia kuliongezea mapato.

149. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/11 Baraza litaendelea na ujenzi wa jengo la ghorofa 18 ambalo litatumika kwa shughuli za kiofisi na kibiashara kwa kushirikiana na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na mwekezaji binafsi, jijini Dar es Salaam.

Bodi ya Mfuko wa Barabara (RFB)

150. Mheshimiwa Spika, Bodi ya Mfuko wa Barabara kwa kipindi cha mwaka 2009/2010 ilikusanya kiasi cha shilingi bilioni 284.1 ikiwa ni ongezeko la asilimia 14 ikilinganishwa na shilingi bilioni 249.1 mwaka 2008/2009.

151. Mheshimiwa Spika, pamoja na ongezeko hilo la makusanyo, changamoto mbalimbali zilijitokeza ikiwa ni pamoja na kutokidhi

111

gharama za matengenezo ya barabara. Kwa mfano, mahitaji halisi ya matengenezo ya barabara nchini kwa mwaka 2009/2010 ukijumuisha na mahitaji ya malimbikizo ya matengenezo ni shilingi bilioni 480 wakati bajeti kwa ajili ya matengenezo kwa mwaka 2009/2010 yalikuwa shilingi billioni 284.1 tu ambayo ni asilimia 59 ya mahitaji. Upungufu huo wa fedha uliathiri zaidi matengenezo maalum ya barabara.

152. Mheshimiwa Spika, changamoto nyingine ni kuongezeka kwa gharama ya kufanya matengenezo ya barabara kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta, vifaa na mitambo ya ujenzi. Aidha, malimbikizo ya matengenezo ya mtandao wa barabara yamesababisha barabara nyingi kuwa kwenye hali mbaya. Inakadiriwa kuwa, hivi sasa malimbikizo ya matengenezo kwa mwaka ni shilingi bilioni 113.0 kwa Barabara Kuu na za Mikoa na shilingi bilioni 70.0 kwa barabara za wilaya, ujazio (feeder roads) na za mijini.

153. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011, Bodi inatarajia kukusanya jumla ya shilingi bilioni 286.9. Orodha ya miradi ya Barabara za Mikoa itakayotekelezwa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara imeoneshwa katika Kiambatanisho Na. 3 na orodha ya Miradi ya 112

Maendeleo itakayotekelezwa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara imeoneshwa katika Kiambatanisho Na.4. Aidha, mchanganuo wa fedha zilizotengwa kwa ajili ya kutekeleza Mpango wa Matengenezo ya Barabara Kuu na Barabara za Mikoa kwa mwaka wa fedha 2010/2011 ni kama unavyooneshwa katika Kiambatanisho Na. 5 (A-F).

Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB)

154. Mheshimiwa Spika, hadi Mei, 2010, Bodi iliweza kusajili wahandisi wazalendo 541 na wageni 61 na kampuni za ushauri wa kihandisi 9, ikilinganishwa na mwaka wa fedha 2008/09 ambapo ilisajili wahandisi wazalendo 461 na wageni 56. Haya ni mafanikio ya ongezeko la wahandisi la asilimia 17 kwa wahandisi wazalendo na asilimia 9 kwa wageni. Hadi kufikia Juni 2010, Bodi iliendelea kusimamia utekelezaji wa utaratibu wa mafunzo ya kujiendeleza kitaaluma kwa wahandisi wote ili waweze kwenda sambamba na mabadiliko ya kisayansi na kiteknolojia.

155. Mheshimiwa Spika, Bodi imeendelea pia kusimamia utekelezaji wa mpango wa mafunzo 113

kwa vitendo kwa wahandisi wahitimu. Katika kipindi cha Julai 2009 hadi Juni 2010, Bodi ilisimamia mafunzo kwa wahandisi wahitimu 998 na kufanya jumla ya wahandisi wahitimu 1,496. Aidha, katika kipindi hicho jumla ya wahandisi wahitimu 501 walihitimu na walisajiliwa kama Wahandisi wataalam (Professional Engineers), jumla ya miradi 285 ilikaguliwa, wahandisi wageni 61 walisajiliwa na 7 walikataliwa usajili kwa sababu hawakuwa na sifa za kutosha.

156. Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio hayo, katika kipindi cha 2009/2010, Bodi ilikabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo; ufinyu wa bajeti kwa ajili ya kutekeleza majukumu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusimamia mpango wa mafunzo kwa vitendo kwa wahandisi wahitimu, kufanya kaguzi za miradi nk, Wahandisi wengi kuikimbia taaluma kutokana na imani kwamba masilahi katika fani ya uhandisi ni madogo ukilinganisha na fani nyingine na ikizingatiwa kwamba mafunzo huchukua miaka mingi kuhitimu uhandisi pamoja na uhaba wa ofisi ambao unasababisha upungufu wa wafanyakazi. Jitihada za kupata eneo la kujenga ofisi bado zinaendelea.

157. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2010/2011, Bodi imepanga kusajili 114

wahandisi 725, Mafundi Sanifu 200 na kampuni za ushauri wa kihandisi 20, kusimamia utekelezaji wa mpango wa mafunzo ya vitendo kwa wahandisi wahitimu 1,220. Bodi itafanya ukaguzi wa shughuli za kihandisi katika Halmashauri zote na miradi yote mikubwa.

Malengo mengine ni kuendelea kuwashawishi wahandisi wataalamu ili waanzishe kampuni za ushauri wa kihandisi mikoani. Kutembelea mikoa yote kuhamasisha utekelezaji wa Sheria ya Usajili wa Wahandisi namba 24 ya mwaka 2007 pamoja na kanuni zake na kusimamia mafunzo ya kujiendeleza kitaaluma kwa wahandisi watalaamu wote.

Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB)

158. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/2010, Bodi ilisajili makandarasi wapya 930 na hivyo kufanya jumla ya makandarasi waliosajiliwa hadi Januari 2010 kufikia 5,698 ikilinganishwa na Makandarasi 5,125 mwaka 2008/2009. Hili ni ongezeko la Makandarasi 573. Aidha, jumla ya makandarasi 154 walipandishwa madaraja yao ya usajili baada ya kukuza uwezo wao na kukidhi 115

vigezo vya madaraja ya juu. Idadi ya Makandarasi waliopandishwa madaraja ya usajili yaliongezeka kutoka 142 mwaka 2008/2009 hadi kufikia makandarasi 154 katika mwaka 2009/2010.

159. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Januari - Disemba 2009 jumla ya miradi 1,765 ilikaguliwa. Miradi 1,235, ambayo ni sawa na asilimia 70 haikuwa na upungufu na miradi 530, sawa na asilimia 30 ilikutwa na mapungufu mbali mbali yakiwemo; kutokuzingatia afya na usalama kazini (11.6%), kutokusajili mradi (17%) na kufanya kazi zinazozidi daraja la usajili (2.6%). Makandarasi waliokutwa na upungufu walichukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria. Idadi ya miradi ya ujenzi iliyokaguliwa na Bodi na haikuwa na upungufu iliongezeka kutoka miradi 1,119 mwaka 2008/2009 hadi kufikia miradi 1,235 mwaka 2009/2010.

Katika mwaka 2009/2010, Bodi iliendesha kozi sita [6] kupitia mpango wake wa mafunzo endelevu kwa makandarasi (Sustainable Structured Training Program) katika mikoa ya Kagera, Dar es Salaam, Ruvuma, Moshi, Morogoro na Tabora ambapo jumla ya washiriki 373 walihudhuria ikilinganishwa na washiriki 285 katika mwaka 2008/2009.

116

160. Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio yaliyopatikana, Bodi ya Usajili wa Makandarasi ilikabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo kukuza uwezo wa makandarasi wazalendo, kwani, ingawa makandarasi wa kizalendo ni asilimia 96, gawio la soko (market share) bado ni dogo (34%). Hii inatokana na makandarasi kuwa na uwezo mdogo kiutendaji. Ili kukabiliana na changamoto hii, Bodi imebuni Mkakati wa Makusudi wa Kuendeleza Makandarasi Wazalendo ili waweze kufanya kazi zenye thamani kubwa.

Uwezo wa makandarasi wazalendo unaathiriwa na kutokuwa na mitambo ya ujenzi. Ili kukabiliana na changamoto hii, Bodi imekamilisha utafiti ambao una mapendekezo ya kuwezesha makandarasi wazalendo kupata miradi. Baadhi ya mapendekezo hayo ni kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika vituo vya kukodisha mitambo (plant hire pools) na pia kuhamasisha asasi za kifedha kuwawezesha makandarasi kutumia “Lease Financing” katika kununua mitambo.

161. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011, Bodi imepanga kusajili makandarasi wapya 803 na kukagua jumla ya miradi ya ujenzi 1,980. Aidha, Bodi inatarajia kuendesha kozi tano kwa ajili ya kujenga uwezo wa makandarasi ikiwa ni 117

pamoja na kuanza utekelezaji wa Mkakati wa Makusudi wa Kuendeleza Makandarasi Wazalendo.

Bodi ya Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB)

162. Mheshimiwa Spika, Bodi imeendelea kuwasajili Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi ambapo katika mwaka 2009/10, jumla ya wabunifu majengo 21 na wakadiriaji majenzi 15 walisajiliwa na hivyo kufanya jumla ya wataalamu waliosajiliwa na Bodi kufikia 460. Usajili huu ni ongezeko la wataalam 27 ikilinganishwa na jumla ya wataalam 433 waliosajiliwa hadi kufikia mwaka 2008/2009. Aidha, Kampuni 8 za wabunifu majengo na kampuni 11 za ukadiriaji majenzi zilisajiliwa na kufanya jumla ya kampuni zilizosajiliwa kufikia 222. Hili ni ongezeko la kampuni 19 ikilinganishwa na kampuni zilizosajiliwa mwaka 2008.

163. Mheshimiwa Spika, Bodi pia iliwasajili wataalam wa fani hizi wenye sifa za kati 25 na kufanya jumla ya wataalam wa sifa za kati waliosajiliwa na Bodi kufikia 62. Mafanikio haya katika usajili ni matokeo ya mpango unaogharimiwa na Serikali wa mafunzo kwa vitendo kwa Wahitimu wa taaluma katika fani hizi mbili. 118

164. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/10, ukaguzi wa majenzi ulifanyika katika mikoa yote 21 ya Tanzania Bara. Jumla ya sehemu za majenzi 999 zilikaguliwa ikilinganishwa na majenzi 610 yaliyokaguliwa mwaka 2008; hili ni ongezeko la sehemu za majenzi 389 zilizokaguliwa. Ukaguzi wa mwaka 2009 ulilenga katika kuhakikisha kwamba wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi wanahusishwa katika sehemu za majenzi na wanatoa huduma za kitaalamu zinazokidhi mahitaji ya jamii na mazingira. Aidha, Bodi ilihakikisha kwamba katika sehemu za majenzi kwa mujibu wa sheria kunakuwepo bango linaloonesha jina na anwani ya mradi, mwenye mradi, wataalam na mkandarasi wa mradi.

165. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/2010, jumla ya majenzi 59 yalisimamishwa kwa muda, wakati waendelezaji na wataalam 72 walichukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kulipa faini kwa mujibu wa sheria kutokana na kukiuka taratibu za ujenzi.

166. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011, Serikali kupitia Bodi itaendelea kutafuta namna bora ya kusimamia utekelezaji wa

119

Sheria ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi ya mwaka 2010. Ili kufanikisha lengo hilo msukumo mkubwa utakuwa kwenye kuimarisha raslimali watu na elimu kwa umma. Aidha, Bodi imepanga kuwasajili wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi wapya 50, kuwasajili Wataalam wenye sifa za kati 28 na Makampuni ya ubunifu majengo na ukadiriaji majenzi 28.

167. Mheshimiwa Spika, vile vile Bodi ina mpango wa kutembelea mikoa yote ya Tanzania Bara kuwaelimisha waendelezaji wa miradi ya ujenzi kuhusu umuhimu wa kutumia wataalam waliosajiliwa na Bodi katika miradi yao. Bodi pia itachukua hatua za kisheria kwa watakaokiuka taratibu za ujenzi.

Kituo cha Usambazaji wa Tekinolojia katika Sekta ya Uchukuzi (Tanzania Transportation Technology Transfer (TANT2 - Centre)

168. Mheshimiwa Spika, Kituo cha Usambazaji wa Tekinolojia katika Sekta ya Uchukuzi kilianzishwa mwaka 1997 kutokana na juhudi za Wizara yangu kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam pamoja na msaada wa Shirika la Barabara la Marekani (US FHWA). Madhumuni ya 120

Kituo hiki ni kuimarisha/kuboresha sekta ya uchukuzi kwa kutumia mbinu ya usambazaji wa tekinolojia katika sekta ya uchukuzi kwa wadau.

Kituo kilianza kwa kujihusisha na usambazaji wa tekinolojia katika sekta ya barabara tu. Hata hivyo kutokana na mapendekezo ya utafiti uliofanyika mwaka 2002 kuhusu uimarishaji wa Kituo na kuwezesha huduma zake kuwa zenye ufanisi mkubwa na endelevu, kuanzia mwaka wa fedha 2003/2004, Kituo hiki kilianza rasmi usambazaji wa tekinolojia katika sekta ya uchukuzi kwa ujumla. Aidha, katika mwaka wa fedha 2010/2011, Wizara ina mpango wa kuendelea kukiendeleza Kituo hiki ili kiweze kusambaza tekinolojia kwa ufanisi zaidi katika sekta ya uchukuzi

Kikosi Cha Ujenzi

169. Mheshimiwa Spika, Vikosi vya Ujenzi vilianzishwa kwa Sheria ya Vikosi vya Ujenzi Na. 23 ya mwaka 1974 ili kufanya kazi za ujenzi pamoja na kubuni miradi yoyote ya kibiashara yenye mahusiano na kazi za majenzi. Vikosi vya Ujenzi vimeendelea kutekeleza kazi za kandarasi mbalimbali zinazopatikana kwa maelekezo ya Serikali au kupatikana kwa njia ya ushindani. 121

Katika mwaka 2009/2010, Vikosi vya Ujenzi vimekuwa vikitekeleza miradi ya ukarabati na uhifadhi wa jengo la boma la kale Bagamoyo, ujenzi wa jengo la nane nane la Wizara ya Miundombinu Dodoma, ujenzi wa nyumba za viongozi Dar es Salaam na Mwanza, ujenzi wa kituo cha mabasi Mkata – Handeni, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Nyamagana, Ofisi ya Mtendaji Kata Enduimat Longido na ujenzi wa “Community Centres” za Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika vituo vya Mafia, Rufiji na Kilwa. Aidha, katika mwaka 2010/2011, Vikosi vya Ujenzi vinategemea kuendelea kukamilisha miradi iliyopo pamoja na miradi mipya itakayopatikana.

Kanda za Maendeleo (Development Corridors)

170. Mheshimiwa Spika, Tanzania ina kanda nne za maendeleo; kanda hizo ni: (i) Ukanda wa Maendeleo wa Mtwara, (ii) Ukanda wa Maendeleo wa Kati, (iii) Ukanda wa Maendeleo wa Tanga na (iv) Ukanda wa Maendeleo wa Dar es Salaam. Katika jitihada za kuendeleza Ukanda wa Maendeleo wa Mtwara, miradi kadhaa inaendelea kutekelezwa ikiwa ni pamoja na maandalizi ya ujenzi wa barabara kutoka Bandari ya Mtwara hadi Bandari ya Mbamba Bay kwa kiwango cha lami. Ili kuwezesha utekelezaji wa miradi ya makaa ya mawe 122

ya Mchuchuma na chuma cha Liganga, Serikali iko katika maadalizi ya ujenzi wa Barabara ya Itoni (Njombe) – Mchuchuma/Liganga – Manda (km 250) kwa kiwango cha lami. Aidha, Serikali inafikiria kujenga njia ya reli kati ya Makambako – Lindi – Mtwara kwa lengo la kufanikisha miradi hiyo.

171. Mheshimiwa Spika, kuhusu ukanda wa kati, Serikali imeendelea kuboresha miundombinu ya reli na bandari katika Ukanda huu. Upembuzi yakinifu wa mradi wa kujenga reli ya kutoka Dar es Salaam - Isaka – Kigali/Keza – Gitega – Musongati umekamilika. Utekelezaji wa mpango wa kupanua bandari ya Dar es Salaam na za Maziwa Makuu unaendelea ili kuhimili ongezeko la mahitaji ya matumizi ya bandari zetu na kurahisisha usafirishaji wa mizigo na abiria.

172. Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea na jitihada za kuimarisha Ukanda wa Maendeleo wa Tanga, ambapo miradi ya barabara, reli na bandari imependekezwa. Uendelezaji wa miradi iliyoainishwa utachochea ukuaji wa shughuli za maendeleo katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii katika Ukanda wa Tanga. Kwa upande wa barabara, Serikali inaendelea na jitihada za kuboresha barabara ya Tanga – Horohoro (km 65) kwa kiwango cha lami ambapo mkataba wa ujenzi ulisainiwa 123

Disemba, 2009. Sambamba na mchakato wa kuanzishwa mradi wa kuvuna magadi katika Ziwa Natron, imependekezwa ijengwe Barabara mpya kwa kiwango cha lami kutoka eneo la mradi hadi Longido (km 99), reli mpya kati ya eneo la mradi na Arusha (km 164), uboreshaji wa reli ya Tanga – Arusha (km 437). Imependekezwa pia ijengwe bandari mpya katika eneo la Mwambani Tanga, ambayo itaongeza ufanisi wa bandari ya Tanga. Jitihada mbalimbali zinaendelea ili kuhakikisha kuwa mapendekezo hayo yanafanyiwa kazi.

173. Mheshimiwa Spika, ukanda wa Maendeleo wa Dar es Salaam unaendelea kuimarishwa kwa kuboresha miundombinu ya reli ya TAZARA, barabara na bandari ya Dar es Salaam. Miradi inayoendelea katika ukanda huu kwa upande wa bandari ni ujenzi na maandalizi ya maegesho ya magari katika bandari ya Dar es Salaam ili kupunguza msongamano bandarini. Miradi mingine inayoendelea ni ukarabati wa barabara kutoka Iyovi – Kitonga na Ikokoto – Iringa, pamoja na uimarishaji wa njia ya reli ya TAZARA eneo la Kitete – Mpanga.

Ushiriki katika Jumuiya Mbalimbali

Ushirikiano kati ya Serikali ya Muungano (SMT) na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ)

124

174. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kufanya vikao vya mara kwa mara katika ngazi ya Mawaziri na Watendaji Wakuu wa Wizara ya Miundombinu (SMT) na Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi (SMZ). Kikao katika ngazi ya Mawaziri kilifanyika tarehe 16 Novemba, 2009 Pemba ambapo tulijadili masuala ya utendaji wa kisekta. Aidha, tulipata nafasi ya kukagua miradi ya ujenzi wa barabara kwa kutumia teknolojia mpya na nyepesi ya Ro – mix, bandari za Wete na Chake Chake pamoja na kujadiliana juu ya masuala mbalimbali yenye kero katika sekta zetu. Aidha, tumekuwa tukishiriki pamoja katika mikutano mbali mbali ya kitaifa, kikanda na kimataifa inayohusu sekta ya uchukuzi. Tutaendelea kukutana mara kwa mara ili kuondoa kero mbali mbali katika sekta ya Uchukuzi. Namshukuru sana Mhe. Machano O. Said Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi – SMZ kwa ushirikiano anaoendelea kunipa.

Ushiriki katika Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC)

175. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kushiriki kwenye mikutano mbalimbali ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuzungumzia masuala

125

yanayohusu usafiri wa barabara, maji, reli, anga na masuala ya hali ya hewa. Katika ushirikiano huu, miradi mbalimbali ya miundombinu imeibuliwa na kufanyiwa maamuzi ya pamoja. Mradi mkubwa ni ule wa Mtandao wa barabara katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (The East African Road Network Project – EARNP) pamoja na Mradi wa Uwezeshaji wa Kiuchukuzi na Kibiashara Afrika Mashariki (East Africa Trade and Transport Facilitation Project – EATTFP). Miradi hii inalenga katika kuhakikisha kuwa ujenzi wa barabara za kikanda kwa kiwango cha lami pamoja na kuoanisha sera na mikakati mbali mbali kuhusu miundombinu kama kiungo muhimu cha kiuchumi. Jumuiya inakamilisha Mkakati wa Kuendeleza Sekta ya Uchukuzi na programu ya Barabara.

176. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Tanzania, utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Arusha – Namanga – Athi River umekamilika kwa takriban kilometa 29. Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara za Arusha – Holili - Voi na Bagamoyo – Saadani - Tanga - Horohoro – Malindi inaendelea. Aidha, kituo cha pamoja cha Forodha cha Namanga (One Stop Border Post) kitajengwa chini ya mkataba wa ujenzi wa mradi wa barabara ya Arusha - Namanga – Athi River.

126

177. Mheshimiwa Spika, kuhusu usafiri wa reli, nchi wanachama wameandaa Mpango Kabambe wa uendelezaji wa reli (The East African Railway Master Plan) pamoja na Mpango Kabambe wa mapitio kuhusu reli (Revised Railways Master Plan) wenye lengo la kuendeleza usafiri wa reli itakayounganisha nchi hizi. Aidha, nchi wanachama wa EAC ziko katika mchakato wa maandalizi ya mwongozo wa kisheria na kiutendaji kuhusu Public Private Partnerships (PPPs) utakaosaidia pia kuendeleleza reli za kikanda.

178. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa usafirishaji majini, Tanzania imeendelea kushirikiana na nchi nyingine wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kupambana na vitendo vya kiharamia katika bahari ya Hindi kwa kushirikiana na IMO, African Union (AU), IGAD pamoja na kuandaa makubaliano ya ushirikiano wa kupambana na kuzuia vitendo vya kiharamia na ujambazi. Aidha, imekubaliwa kuwa Kituo cha Utafutaji na Uokoaji katika maziwa kijengwe Mwanza.

127

Ushiriki katika Jumuiya ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC)

179. Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza Makubaliano ya Itifaki ya Uchukuzi, Mawasiliano na Hali ya Hewa ya Nchi Wanachama wa SADC ya mwaka 1998 (The SADC Protocol on Transport, Communication and Meteorology of 1998), Wizara imeendelea kushiriki katika vikao mbalimbali vya SADC kuhusu masuala ya uoanishaji wa tozo za ushuru wa barabara na uoanishaji wa viwango vya uzito na ukubwa wa magari, uendelezaji wa Kanda za Uchukuzi na ulegezaji wa masharti katika usafiri wa anga. Lengo ni kufungua njia za mawasiliano ya uchukuzi wa barabara na anga ili kuwezesha kukuza biashara kwa nchi wanachama.

180. Mheshimiwa Spika, sambamba na utekelezaji wa masuala muhimu yaliyopo katika Itifaki ya Uchukuzi, Mawasiliano na Hali ya Hewa, Wizara bado ina jukumu la msingi katika uendelezaji wa miundombinu ya uchukuzi ili kuiunganisha nchi yetu na nchi wanachama wa SADC. Miongoni mwa miradi iliyopo katika Ukanda wa Maendeleo wa Mtwara ni pamoja na ujenzi wa barabara za Mtwara – Mbamba Bay na Tunduma – Sumbawanga – Kasulu – Nyakanazi zitakazoiunganisha nchi yetu na nchi za Msumbiji, 128

Malawi, Zambia na DRC pamoja na kukamilika kwa ujenzi wa Daraja la Umoja linaloiunganisha nchi yetu na Msumbiji. Uboreshaji wa usafiri wa reli ya TAZARA na huduma za usafiri katika bandari za Mtwara, Kasanga na Mbamba Bay utaendelea kupewa kipaumbele.

Maendeleo ya Watumishi

181. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/2010, Wizara imetekeleza muundo wake mpya na kujaza nafasi za Wakurugenzi na Wakurugenzi Wasaidizi kulingana na Muundo huo. Wizara imeendelea kuwahudumia watumishi wake katika nyanja za kitaaluma na kijamii. Katika kipindi hiki, Wizara ilipeleka watumishi 97 katika mafunzo ndani na nje ya nchi. Kati yao, watumishi 19 walipelekwa mafunzo ya muda mrefu na 65 mafunzo ya muda mfupi ndani ya nchi, na watumishi 13 walipelekwa mafunzo ya muda mfupi nje ya nchi.

182. Mheshimiwa Spika, Wizara iliwapandisha vyeo watumishi 14 wa kada mbalimbali na kuthibitisha kazini watumishi 23. Wizara ilipata vibali 59 vya ajira za wataalam wa kigeni ambapo wataalam 29 walipatiwa vibali vya 129

ajira mpya, na wataalam 30 waliongezewa muda wa kufanya kazi nchini. Wizara pia iliweza kuzindua Mkataba wa Huduma kwa Mteja.

183. Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa imeendelea kuwaelimisha wafanyakazi wote katika semina mbali mbali, kuhusu athari za Rushwa katika sekta yetu, makosa ya rushwa yanayoweza kutendeka na kuwahimiza kuepukana na makosa hayo. Aidha, Wizara iliendelea kuwasaidia watumishi waishio na virusi vya UKIMWI kwa kuwagharamia chakula chenye lishe bora kwa waliojitokeza.

184. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/11, hadhi za Wakuu wa sehemu katika Idara ya Utawala na Utumishi; na Idara ya Sera na Mipango zimepandishwa na kuwa na hadhi ya Wakurugenzi Wasaidizi. Aidha, utaratibu wa kupeleka watumishi mafunzoni utaendelea kwa awamu kwa lengo la kuwaongezea ujuzi, ufanisi, na tija katika kufanya kazi zao. Watumishi 183 wamepangiwa kupewa mafunzo. Kati yao, watumishi 142 watakwenda kwenye mafunzo ya muda mfupi na wengine 41 watakwenda kwenye mafunzo ya muda mrefu. Aidha, Wizara itajaza nafasi 14 zilizo 130

wazi baada ya kupata kibali kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

185. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011, Wizara itaendelea kuwasaidia watumishi waishio na virusi vya UKIMWI kwa kuwagharamia chakula chenye lishe bora kwa wataojitokeza na kuwahamasisha watumishi wengine kupima afya zao.

E. MASUALA MTAMBUKA

Utunzaji wa Mazingira

186. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuhakikisha kuwa miradi yote ya maendeleo ya miundombinu inatekelezwa kwa kuzingatia uhifadhi wa mazingira kwa kutumia Sera, Sheria, Kanuni na Mikataba ya kimataifa iliyoridhiwa na Serikali. Katika 2009/2010, Wizara iliendelea kusimamia utekelezaji na uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira Na. 20 ya Mwaka 2004 ikiwa ni pamoja na kupitia taarifa za Tathimini ya Athari kwa Mazingira (TAM)

131

za miradi ya barabara 16 na mradi wa ujenzi wa gati Na.1 katika bandari ya Mtwara.

Katika ukaguzi wa barabara uliofanyika, imegundulika kuwepo kwa uchafuzi wa mazingira unaosababishwa na vyombo vya usafiri. Kutokana na hali hii, Wizara kwa kuanzia inatarajia kujenga vituo vya kupumzikia katika maeneo ya Nangurukuru, barabara za Dar es Salaam – Lindi – Mtwara na Mkata katika barabara ya Dar es Salaam – Arusha. Aidha, Wizara iliandaa kanuni kwa ajili ya kuzingatia uhifadhi wa mazingira wakati wa ujenzi wa barabara. Kanuni hizo ni Mfumo wa Usimamizi wa Uhifadhi wa Mazingira, Mwongozo wa Kutathmini na Kusimamia Uhifadhi wa Mazingira ya Barabara na Kanuni za Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira ya Barabara.

187. Mheshimiwa Spika, Wizara pia ilifanya mafunzo kuhusu Tathmini ya Athari na Uhifadhi wa Mazingira ya barabara kwa Wahandisi 100 na Mafundi Sanifu 130 kutoka katika Halmashauri za Miji na Wakala wa Barabara (TANROADS). Kupitia Mradi wa utekelezaji wa Sheria ya Mazingira, Wizara ilishirikiana na wadau husika kutoa elimu ya kuhifadhi mazingira ya Bahari na Maziwa kwa Wadau wa vyombo vya Uchukuzi Majini katika Bandari za Mwanza, Mtwara, Ziwa Tanganyika na Dar es Salaam.

132

188. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2010/2011, Wizara itaendelea kuhakikisha kuwa miradi ya miundombinu inatekelezwa kwa kuzingatia maendeleo endelevu ya uhifadhi wa mazingira, kuandaa Kanuni za ujenzi na uendeshaji wa viwanja vya ndege na bandari.

Habari, Elimu na Mawasiliano

189. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuelimisha Umma kuhusu shughuli za Sekta ya ujenzi, uchukuzi na hali ya hewa kupitia njia mbali mbali za upashanaji habari. Aidha, tovuti za taasisi zilizo chini ya Wizara ya Miundombinu zimeunganishwa katika Tovuti ya Wizara ili kumwezesha mtumiaji kupata Rejea za taarifa mbalimbali kwa urahisi. Wizara pia imeendelea kuratibu na kuandaa vipindi maalum kwenye televisheni kwa lengo la kuelezea matukio mbalimbali ya sekta, mafanikio yaliyopatikana na matarajio ya utekelezaji wa shughuli mbali mbali zinazosimamiwa na Wizara ya Miundombinu.

190. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa fedha 2010/2011, Wizara itaendelea na kampeni za 133

upashaji habari na utoaji elimu kwa Umma kupitia vyombo vya habari, mabango, vipeperushi na majukwaa mbalimbali yakiwemo matamasha ya kitaifa na Kimataifa.

F. TAASISI ZA MAFUNZO

191. Mheshimiwa Spika, Wizara inathamini mchango unaotolewa na vyuo vyetu vya mafunzo katika kutoa Wataalam wa kada mbalimbali kuhusu masuala ya ujenzi, uchukuzi na hali ya hewa. Vyuo vilivyo chini ya Wizara ya Miundombinu ni pamoja na; Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma, Chuo cha Usafiri wa Anga Dar es Salaam, Chuo cha Ujenzi Morogoro na Chuo Cha Matumizi ya Teknolojia Stahili ya Nguvu Kazi (Appropriate Technology Training Institute – ATTI) Mbeya.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT)

134

192. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2009/10, Chuo kilidahili jumla ya wanafunzi 269 wa kozi ndefu ikilinganishwa na jumla ya wanafunzi 248 waliodahiliwa katika mwaka 2008/2009. Hili ni ongezeko la asilimia 8. Kwa upande wa kozi za muda mfupi za aina mbalimbali, Chuo kiliendesha kozi kwa wanafunzi 1,701. Aidha, Chuo kimeweza kuboresha mitaala yake na kutoa mafunzo ambayo yanakidhi mahitaji ya soko la ajira na kujiajiri baada ya kupata ithibati kutoka Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi. Mafunzo hayo yanatolewa katika mfumo wa “Competence Based Education and Training (CBET)” katika ngazi ya Stashahada na Shahada ya kwanza.

193. Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio hayo, Chuo kiliweza kutekeleza Mpango Mkakati wake ulioanza mwaka 2005 na kumalizika 2009 kwa asilimia 30 kutokana na ukosefu wa fedha pamoja na upungufu wa vitendea kazi kama vile maktaba, maabara za kufundishia, vifaa vya karakana, magari ya kufundishia, uhaba wa mabweni kwa wanafunzi na uhaba wa nyumba za wahadhiri.

194. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2010/11, Chuo kimepanga kuendelea kuipitia mitaala yake na kuongeza idadi ya programu, 135

kuimarisha uwezo wa wanataaluma wa Chuo, kuimarisha kozi za udereva wa kujihami, kuimarisha ukaguzi wa magari na utahini wa madereva, kuimarisha menejimenti ya Lojistiki ya Mizigo na kuongeza idadi ya wanafunzi wa kike kutoka asilimia 20 hadi asilimia 35 ya wanafunzi wote.

Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI)

195. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2009/2010, Chuo cha Bahari Dar es Salaam kimeendelea kutoa huduma za mafunzo, utafiti, ukarabati wa vifaa vya kuokolea maisha na uwakala wa ajira kwa Wafanyakazi melini. Mafunzo yaliyotolewa yalilenga katika kuendeleza rasilimali watu katika sekta ya usafiri majini. Katika kipindi hiki, Wanafunzi 378 wa kozi ndefu na 5,087 wa kozi fupi walijiunga na chuo ikijumuisha Wanafunzi wa ndani na nje ya nchi. Wanafunzi wa nje walitoka katika nchi za Kenya, Uganda, Comoro na Namibia. Aidha, udahili wa wanafunzi wa kozi ndefu umekuwa ukiongezeka baada ya wanafunzi wa stashahada ya juu kupata udhamini wa Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.

136

196. Mheshimiwa Spika, Chuo kimeendelea kukabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo uhaba wa vifaa vya kufundishia, miundombinu na ugumu wa kupata ajira kwa wahitimu wa chuo.

197. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2010/2011, Serikali ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China zina mpango wa kutatekeleza mradi wa maendeleo wa chuo cha Dar es Salaam kupitia ushirikiano kati ya Chuo cha Bahari cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Usafiri majini cha Dalian cha China; ambapo Chuo kikuu cha Dalian kitajenga tawi la chuo hicho ndani ya chuo cha Dar Es Salaam. Miundombinu itakayojengwa itakidhi mahitaji ya soko la elimu na mafunzo yanayohusu bahari. Aidha, Chuo kimepanga kununua “Engine Room Simulator” kwa ajili ya mafunzo ya vitendo ya wanafunzi Wahandisi wa meli.

Chuo kwa kushirikiana na SUMATRA, kitaelekeza nguvu zake katika kutafuta ajira kwa wahitimu wake katika meli za mataifa ambayo yatasaini mikataba ya ushirikiano na SUMATRA ya kutambua vyeti vya wahitimu kutoka chuo cha bahari. Aidha, Chuo kitaendelea kujitangaza ili kupata wanafunzi wengi zaidi wa ndani na nje ya nchi.

137

Chuo cha Usafiri wa Anga Dar es Salaam

198. Mheshimiwa Spika, Chuo cha Usafiri wa Anga (Tanzania Civil Aviation Training Centre) kimeendelea kutoa mafunzo yahusuyo shughuli za usafiri wa Anga na uendeshaji wa viwanja vya ndege. Mafunzo hayo hutolewa kwa wanafunzi wa ndani na nje ya nchi. Katika mwaka wa fedha 2009/10, idadi ya wahitimu kutoka chuo hicho ilikuwa 110 ikilinganishwa na wahitimu 269 katika kipindi cha mwaka 2008/09 ikiwa ni pungufu ya asilimia 59.

199. Mheshimiwa Spika, hatua zilizochukuliwa na Chuo katika kipindi cha mwaka 2009/10 ni pamoja na kuwaendeleza kitaaluma wakufunzi 20, Chuo kuendelea kupokea wanafunzi kutoka nchi za Botswana, Namibia, Uganda na Rwanda. Aidha, Chuo kilishinda na kupewa mkataba wa kuendesha mafunzo ya muda mfupi ya kitaaluma kwa ajili ya Mamlaka ya viwanja huko Msumbiji na hivyo kuendelea kuiingizia nchi fedha za kigeni na pia kutunukiwa cheti na Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Namibia cha kutambua ubora wake.

138

200. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2010/11, Chuo kimepanga kuongeza idadi ya kozi zinazotolewa na chuo ikiwa ni pamoja na kuwa na majengo yake.

Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma

201. Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) imeendelea kuboresha Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma kwa kujenga madarasa mawili. Jumla ya wanafunzi 227 walihitimu mafunzo ya awali na ya kati ya utabiri. Aidha, mafunzo ya muda mfupi na mrefu yamekuwa yakitolewa kwa wafanyakazi wa kada mbalimbali kulingana na mpango wa mafunzo wa Mamlaka. Katika mwaka wa 2010/2011, Chuo kinatarajia kuendelea kutoa mafunzo ya awali na ya kati katika fani ya hali ya hewa.

Chuo cha Ujenzi Morogoro

202. Mheshimiwa spika, Chuo cha Ujenzi Morogoro kilianzishwa mwaka 1962 kwa ajili ya kuendeleza taaluma za mafundi sanifu, stadi na Wahandisi wa Wizara za Miundombinu na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Aidha, Chuo kwa sasa 139

kinatoa mafunzo kwa mafundi sanifu na stadi wanaoshiriki kazi za ujenzi kwenye sekta zote za umma na binafsi.

Hadi kufikia Mei, 2010, Chuo kimetoa mafunzo kwa Wanafunzi 346 kwa ngazi ya Ufundi Sanifu kwa fani ya barabara na majengo, 106, kwa fani ya Ufundi, madereva bingwa wa umma 40, madereva waanzaji 116 na mafundi stadi waanzaji 84.

203. Mheshimiwa spika, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2010/11, Chuo kimepanga kuendeleza ujenzi wa jengo jipya la madarasa na karakana ya ufundi, kukarabati majengo 4, kununua samani, zana ndogo ndogo za kufundishia, kufundisha jumla ya wanafunzi 440 wa fani ya ufundi sanifu wa barabara, majengo na ufundi 120, madereva bingwa wa umma 50, madereva waanzaji 190, na mafundi stadi waanzaji toka fani za barabara, majengo na ufundi 80.

Chuo Cha Matumizi ya Teknolojia Stahili ya Nguvu Kazi katika ujenzi na matengenezo ya barabara (Appropriate Technology Training Institute – ATTI), Mbeya

140

204. Mheshmiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2009/10, Chuo Cha Matumizi ya Teknolojia Stahili ya Nguvu Kazi (ATTI) kimeendelea kutoa elimu ya matumizi ya teknolojia ya Nguvu kazi katika ukarabati na matengenezo ya barabara. Mafunzo hayo yametolewa kwa Makandasi wa Nguvu kazi, Wahandisi kutoka Halmashauri za Wilaya katika mikoa ya Tabora, Singida, Mbeya, Rukwa, Dodoma na sekta binafsi. Aidha, mafunzo yametolewa kwa wanawake wanaofanya kazi kwa kutumia teknolojia Stahili ya nguvu kazi na wanaotarajia kuanzisha kampuni za Ukandarasi kwa kutumia teknolojia Stahili ya Nguvu kazi.

Katika mwaka 2010/11, Chuo kitaendelea na usimamizi na utekelezaji wa mpango wa “Taking Labour Based Technology to Scale”, kutoa mafunzo ya teknolojia stahili ya Nguvu kazi kwa Makandarasi, Wahandisi toka Halmashauri za Wilaya na sekta binafsi. Aidha, mafunzo yatatolewa kwa Makandarasi wanaotumia teknolojia stahili ya Nguvu kazi na Wahandisi wa Halmashauri katika mikoa ya Iringa na Ruvuma kwa kugharimiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

G. SHUKURANI

141

205. Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Wizara ya Miundombinu, napenda kutoa shukurani za dhati kwa wadau wote wa sekta za ujenzi, uchukuzi na hali ya hewa ikiwemo sekta binafsi kwa ushirikiano wao katika kutimiza malengo yetu. Aidha, nawashukuru kwa dhati Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na wadau wengine kwa ushirikiano mkubwa waliouonesha wakati wa kipindi kigumu cha kukarabati na kurudisha katika hali ya kawaida miundombinu ya barabara na reli iliyoharibiwa na mvua kubwa zilizonyesha kati ya Disemba 2009 na Januari 2010. Shukurani zetu pia ziwaendee Washirika wetu wa maendeleo katika kutekeleza programu na mipango yetu ya Sekta. Washirika hao ni pamoja na mashirika ya kimataifa na taasisi za kimataifa zinazochangia katika kuboresha utoaji huduma na miundombinu ya sekta zetu. Nchi na mashirika hayo ni pamoja na Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Majini (IMO), Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO), Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), Benki ya Dunia (WB), Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Afrika (BADEA), Kuwait Fund, Jamhuri ya Korea, OPEC Fund, Umoja wa Nchi za Ulaya, “Third World Organization for Women in Science” (TWOWS), UNESCO, Urusi, Afrika Kusini, Uingereza, Marekani, Uholanzi, Japan, Korea, India, China, Denmark, Norway, Ubeligiji, Ujerumani na wengine wengi. Tungependa

142

waendelee kushirikiana nasi katika kuimarisha sekta yetu na kufanikisha malengo yetu.

206. Mheshimiwa Spika, napenda kuishukuru tena Kamati ya Bunge ya Miundombinu ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mheshimiwa Alhaj Mohamed Hamisi Missanga (Mb), Mbunge wa Jimbo la Singida Kusini na Waheshimiwa Wabunge wa Bunge lako Tukufu kwa michango na ushirikiano waliotupa katika kuimarisha huduma zitolewazo na Wizara.

207. Mheshimiwa Spika, shukurani zetu pia ziwafikie wadau mbalimbali hasa wa sekta binafsi kwa ushirikiano wao katika kutekeleza malengo ya sekta zetu. Nawapongeza waheshimiwa wabunge wenzangu kwa michango na ushirikiano mlionipa katika kuimarisha huduma zitolewazo na Wizara.

208. Mheshimiwa Spika, ninapofika mwisho wa hotuba hii sina budi kuwashukuru viongozi wenzangu katika Wizara nikianza na Naibu Waziri, Mheshimiwa Hezekiah Ndahani Chibulunje (Mb.), Katibu Mkuu Mhandisi Omar Abdallah Chambo, Wakuu wa Idara, Wakuu wa Vitengo, Viongozi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara pamoja na watumishi wote wa Wizara na Taasisi. Wote kwa pamoja 143

wamenipa ushirikiano mkubwa ambao umenisaidia kutekeleza majukumu niliyopewa ya kusimamia uendelezaji wa sekta za ujenzi, uchukuzi na hali ya hewa. Michango yao ya mawazo na utendaji wao mzuri yamewezesha kufanya kazi yetu kuwa rahisi na yenye mafanikio. Nawashukuru sana.

H. MAOMBI YA FEDHA

209. Mheshimiwa Spika, ili Wizara iweze kutekeleza majukumu na malengo yake ipasavyo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2010/2011, naomba bunge lako tukufu liidhinishe jumla ya shillingi 1,164,983,227,000 Kati ya fedha hizo, shillingi 293,429,311,000 ni kwa matumizi ya kawaida na shillingi 871,553,916,000 ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Fedha za matumizi ya kawaida inajumuisha shillingi 56,743,044,000 za mishahara ya watumishi na shillingi 236,686,267,000 ni fedha za Matumizi Mengineyo (OC). Fedha za Miradi ya Maendeleo inajumuisha shillingi 370,880,081,000 za ndani na shillingi 500,673,835,000 ni fedha za nje.

210. Mheshimiwa Spika, napenda kwa mara nyingine nitoe shukurani zangu za dhati kwako binafsi na kwa Waheshimiwa Wabunge kwa 144

kunisikiliza. Hotuba hii inapatikana pia katika tovuti ya Wizara kwa anuani ya: www.infrastructure.go.tz.

211. Mheshimiwa Spika, pamoja na hotuba hii nimeambatanisha majedwali ya miradi yote itakayotekelezwa katika mwaka 2010/2011 pamoja na kiasi cha fedha kilichotengwa kutekeleza miradi hiyo. Naomba viambatisho hivyo vichukuliwe kama sehemu ya vielelezo vya hoja hii.

212. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

145

KIAMBATISHO NA. 1

Mgawanyo wa fedha za Bajeti ya Maendeleo kwa mwaka 2010/11 MAKADIRIO 2010/11 (Tshs. mil) MFADHILI km Fedha za Fedha za Jumla ndani Nje SUBVOTE 1001: ADMINISTRATION 5492 Tanzania Multisectoral AIDS Project 31.51 31.51 WB 6284 Public Sector Reform Program - PSRP II 1,403.70 1,403.70 WB SUB TOTAL 1,435.21 1,435.21 SUBVOTE 1003: POLICY AND PLANNING 6251 Public Finance Management Programme(PFMRP) 259.53 259.53 WB 6267 Institutional Support 500 3,979.59 4,479.59 GOT/DFID/EU SUB TOTAL 500 4,239.12 4,739.12 SUB VOTE 2002: TECHCAL SERVICES 4125 Construction of ferry ramps and vending machines 751.94 - 751.94 GOT 4139 Procurement of Ferries 4No 1,304.25 - 1,304.25 GOT 4144 Rehabilitation of 2 ferries (Mv Alina & Mv Pangani) 471.96 471.96 GOT 6327 Construction of Government Houses 5,696.67 - 5,696.67 GOT SUB TOTAL 8,224.83 - 8,224.83 146

SUB VOTE 2005: TRANSPORT 4109 Wazo Hill - Bagamoyo - Msata 64 5,651.75 - 5,651.75 GOT Usagara - Geita-Bwanga -Buzirayombo - Kyamyorwa (424km) 422 - - - (i) Kyamyorwa - Buzirayombo (Construction) 120 1,304.25 - 1,304.25 GOT 4110 (ii) Buzirayombo - Geita (Construction) 100 1,043.40 - 1,043.40 GOT (iii) Geita - Usagara (Lot 1 & Lot 2) 90 5,043.10 - 5,043.10 GOT (iv) Uyovu-Bwanga-Biharamulo (Construction) 112 2,608.50 - 2,608.50 GOT Kigoma-Kidahwe - Uvinza-Kaliua-Tabora 443 - (i) Malagarasi Bridge and Associated approach roads 48 3,043.25 26,000.00 29,043.25 GOT/KOREA 4112 (ii) Kigoma - Kidahwe section 36km 36 5,651.75 - 5,651.75 GOT (iii) Kidahwe-Uvinza-Ilunde 76 2,608.50 45,000.00 47,608.50 Abu Dhabi/GOT (iv) Tabora - Ndono (42km) 42 4,347.50 0 4,347.50 GOT Marangu-Tarakea - Rongai - Kamwanga/Bomang'ombe - Sanya Juu (Const. & F/S) 173 4115 (i) Marangu - Rombo Mkuu incl. Mwika - Kilacha 34 3,738.85 - 3,738.85 GOT/NORAD (ii) Rombo Mkuu - Tarakea 32 1,739.00 10,500.00 12,239.00 GOT/BADEA (iii) Tarakea - Rongai - Kamwanga 32 3,478.00 - 3,478.00 GOT (iv) Bomang'ombe - Sanya Juu - Kamwanga 75 - - - GOT 147

4117 Nangurukuru - Mbwemkulu 95 869.5 - 869.5 GOT 4118 Dodoma - Manyoni 125 1,565.10 - 1,565.10 GOT 4120 Mbwemkulu - Mingoyo 95 1,043.40 - 1,043.40 GOT (iv) Construction of Maligisu bridge in Mwanza region 1No 347.8 - 347.8 GOT (v) Construction of Kilombero bridge Morogoro 1No 3,478.00 - 3,478.00 GOT (vi) Kavuu Bridge along Majimoto-Inyonga 1No 1,304.25 - 1,304.25 GOT 4126 (vii) Construction of Mbutu Bridge along Igunga- Manonga 1No 869.5 - 869.5 GOT (viii) Bailey bridge for 1No 260.85 260.85 GOT (ix) Ruhekei Bridge along Mbinga-Mbambabay 1No 695.6 - 695.6 GOT 4127 New Bagamoyo (Kawawa Jct - Tegeta) 17 4,347.50 14,000.00 18,347.50 GOT/JAPAN 4128 Kyaka - Bugene - Kasulo 58 4,347.50 - 4,347.50 GOT Isaka – Lusahunga (Rehab) 245 4129 Isaka - Ushirombo (Rehabilitaion) 245 4,347.50 4,347.50 GOT/EU Ushirombo- Lusahunga (Rehabilitaion) 245 1,739.00 1,739.00 GOT/EU Manyoni - Itigi - Tabora Road - GOT 4130 Tabora - Nyahua Sect. 85 4,347.50 - 4,347.50 GOT Manyoni- Itigi - Chaya Sect. 89.35 4,347.50 - 4,347.50 GOT 4131 Korogwe - Handeni 65 4,347.50 - 4,347.50 GOT 4132 Regional Roads Rehabilitation (21 regions) 1,825.60 36,709.25 10,231.00 46,940.25 GOT / DANIDA

148

4133 Mwanza - Shinyanga Border road Rehabilitation 10 347.8 - 347.8 GOT 4134 Handeni - Mkata Road (54km) 54 4,347.50 - 4,347.50 GOT 4135 Mwandiga - Manyovu (Construction) 60 4,347.50 - 4,347.50 GOT 4137 1No 695.6 - 695.6 GOT/MZQ De-congestion of DSM Roads 19.4 - (i) Kawawa R/about – Msimbazi – Twiga (Jangwani) 2.7 4,097.83 - 4,097.83 GOT 4138 (ii) Ubungo Terminal – Kigogo R/About 6.4 4,347.50 - 4,347.50 GOT (iii) Jet corner- Vituka-Devis corner 10.3 4,899.56 - 4,899.56 GOT (iv) Nyerere – Uhuru road drainage 1,000.00 - 1,000.00 GOT 4143 Ndundu - Somanga 60 4,782.25 22,000.00 26,782.25 GOT/OPEC 4147 Kidatu - Ifakara 30 695.6 695.6 GOT/SDC 4148 Tabora - Ipole - Koga - Mpanda road [ FS & DD ] 100 869.5 - 869.5 GOT Natta - Mugumu - Klein's Camp - Loliondo - Mto wa 4149 Mbu (DD & Construction) 452 1,739.00 - 1,739.00 GOT 4150 Ibanda - Itungi Port (5km) 26 173.9 - 173.9 GOT 4151 Tanga - Horohoro Road (Construction) 65 521.7 - 521.7 GOT/MCC 4152 Nzega - Tabora Road (Constr.) 116 6,521.25 - 6,521.25 GOT Sumbawanga - Nyakanazi Road (DD & Construction) 201.6 4154 (i) Sumbawanga-Kanazi Road 75 4,347.50 - 4,347.50 GOT (ii) Kanazi – Kizi - Kibaoni Road 76.6 4,347.50 - 4,347.50 GOT

149

Nyanguge - Musoma/Kisesa Bypass [Musoma – 4155 Mwanza Border (83km)] 202 869.5 - 869.5 GOT 4156 Construction of 712.8 12,315.50 13,028.30 GOT/IDA 4157 Construction of 2,427.50 - 2,427.50 GOT/MCC 4158 Construction of Mpanda Airport 7,892.98 - 7,892.98 GOT 4159 Construction of 612.5 10,083.00 10,695.50 GOT/IDA 4160 Magole - Mziha Road (Magole -Turiani section 48.6 3,478.00 - 3,478.00 GOT k) Road Flyovers and their Approach roads (i) TAZARA 1No 347.8 - 347.8 GOT 4161 (ii) Ubungo 1No 347.8 - 347.8 GOT 4162 Mwigumbi - Maswa - Bariadi - Lamadi (71.8km) 71.8 4,347.50 - 4,347.50 GOT 4163 Ipole-Rungwa ( FS& DD) 95 869.5 - 869.5 GOT 4164 Kidahwe- Kasulu 50 6,086.50 - 6,086.50 GOT 4165 Mafia Aiport Access road (14 km) (DD & Constr.) 14 3,478.00 - 3,478.00 GOT 4166 Dodoma University road 2,795.44 2,795.44 GOT 4171 Sam Nujoma Road Upgrading 4 260.85 - 260.85 GOT 4180 Tunduma - Sumbawanga Upgrading (Constr) 231 695.6 - 695.6 GOT/MCC 4181 Kagoma - Lusahunga (Construction) 154 6,086.50 - 6,086.50 GOT Arusha - Namanga section of Arusha Athi River road 4182 (Rehab.) 105 434.75 30,000.00 30,434.75 GOT/ADB/JICA 150

4183 Singida - Babati - Minjingu (Construction) 222 7,825.50 34,000.00 41,825.50 GOT/ADB Dar es Salaam - Mbagala Road Upgrading (Kilwa 4185 Road) 12 3,478.00 3,478.00 GOT/JICA Msimba - Ruaha Mbuyuni/Ikokoto - Mafinga (TANZAM) (Rehab.) 219 173.9 80,000.00 80,173.90 GOT/DANIDA 4186 Rujewa - Madibira - Mafinga 152 2,608.50 - 2,608.50 GOT 4187 Same - Mkumbara - Korogwe (Rehabilitation) 165 869.5 40,000.00 40,869.50 GOT/IDA Mbeya - Makongolosi (Construction) Lwanjilo - Chunya Sect. 115 5,217.00 - 5,217.00 GOT 4188 Mbeya - Lwanjilo Section (Construction) 5,217.00 5,217.00 GOT 4189 Chalinze - Segera - Tanga 248 6,521.25 18,000.00 24,521.25 GOT/DANIDA 4192 Ruvu Bridge Construction 1No. 434.75 - 434.75 GOT 4195 Dodoma - Iringa (Construction) 267 5,217.00 46,358.00 51,575.00 GOT/ADB/JICA 4196 Dodoma - Babati 261 9,564.50 - 9,564.50 GOT

Masasi - Songea - Mbambabay (649km) 608.5 (i) Masasi - Mangaka 54 695.6 13,667.00 14,362.60 GOT/JICA (ii) Mangaka - Tunduru (FS & DD) 146 434.75 - 434.75 GOT/ADB/JICA (iii) Tunduru - Namtumbo 194 1,739.00 19,142.00 20,881.00 ADB/JICA 4197 (iv) Namtumbo - Songea 70 521.7 - 521.7 GOT/MCC

151

(v) Peramiho - Mbinga 144.5 521.7 - 521.7 MCC/GOT 4206 Construction of 13,316.20 9,950.00 23,266.20 GOT/BADEA 4207 Construction of Singida Airport 100 - 100 GOT 4209 Construction of 753.6 23,200.00 23,953.60 GOT/BADEA 4210 Construction of 1,000.00 - 1,000.00 GOT 4211 Rail Rehabilitation - TAZARA (Kit-Mpanga) 6,000.00 - 6,000.00 GOT 4213 Relaying of 197kms of TRC with 80 Ibis/yards 10,000.00 - 10,000.00 GOT Rail Rehab (Manyoni/SGD -Kaliua/Mpanda) (i) Kaliua - Mpanda sect. 600 - 600 GOT 4215 (ii) Manyoni - Singida 200 - 200 GOT Rail Rehabilitation (Dsm - Dom) Track Repair and improvement of Drainage 4,000.00 - 4,000.00 GOT Track measuring Car (2Nos) 3,500.00 - 3,500.00 GOT 4216 Bridge strengthening ( Dsm - Morogoro) 2,521.00 - 2,521.00 GOT 4281 Isaka - Kigali rail (DD) 387.78 387.78 GOT 4282 Inland Container Depots. 3,000.00 - 3,000.00 GOT 4286 Construction of Msalato Airport 100 - 100 GOT/IDA 4287 Construction of 1,713.80 10,083.00 11,796.80 GOT/IDA 4289 Construction of Terminal III JNIA 15,000.00 - 15,000.00 GOT 6377 Construction of NIT library building 1,739.00 - 1,739.00 GOT 152

Construction of TANROADS HQ (Design & 6383 Construction) 1,739.00 - 1,739.00 GOT 6520 Dev. of 8 berths in L. Tanganyika & Victoria 3,288.80 3,288.80 GOT 6521 Construction of Jetty at Mafia Port 3,478.00 - 3,478.00 GOT SUB TOTAL 348,742.81 493,594.50 842,337.31 GOT

SUB VOTE 2006: TRANSPORT SERVICES 4290 TMA Radar and Equipment 4No 3,478.00 - 3,478.00 GOT 4291 Government Aircrafts maintenance 9,151.36 - 9,151.36 GOT SUB TOTAL 1No 12,629.36 - 12,629.36 SUB VOTE 5002: SAFETY AND 4136 Road Safety Activities 783.09 575 1,358.09 GOT/DANIDA 6221 Institution Support to safety Environment 650 650 DANIDA 6571 EMA Implementation Support Programme 180 180 DANIDA SUB TOTAL 783.09 1,405.00 2,188.09 DANIDA GRAND TOTAL 370,880.08 500,673.84 871,553.92

153

KIAMBATANISHO NA.2.

Miradi ya Maendeleo ya Barabara za Mikoa (Kasma 4132) kwa mwaka 2010/11

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje 1 ARUSHA REGION Upgrading of Mbauda - Losinyai to DSD 0.8 90.00 90.00 Rehab.Olokii - Losinyai road 5.0 60.00 60.00 Upgrading to DSD Monduli township roads 1.0 200.00 200.00 Rehab.Mto wa Mbu - Loliondo road 210km 4.0 50.00 50.00 Rehab. Karatu Jnct. - Mangola - Matala (150km) 8.0 100.00 100.00 Upgrading to DSD Usa river- Momela -Arusha National 0.5 100.00 - 100.00 Park Upgrading to DSD Arusha urban roads 1.0 250.00 Rehab.Monduli Juu - Kitumbeine 6.0 80.00 80.00 Upgrading to DSD Monduli - Monduli Juu 0.3 80.00 80.00

154

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Rehab. Noondoto Jnct- Kitumbeine Road (80.6km) 6.0 70.00 70.00 Rehab. Karatu - Arusha/ Manyara boarder towards 8.0 100.00 Mbulu. 100.00 F S & DD of Kijenge - USA (Nelson Mandela University - 9.0 150.00 9km) 150.00 2 COAST REGION Upgrading of Pugu - Kisarawe - Vikumburu road . 0.5 80.00 80.00 Rehabilitation of Mbuyuni - Saadan road 6.0 80.00 80.00 Rehabiltation of Kilindoni - Rasmkumbi road - 62km 6.0 80.00 80.00 Rehabilitation of Mkuranga - Kisiju road (Karole - Kisiju 6.0 80.00 sect.) 80.00 Upgrading to DSD Kwa Matias - Nyumbu - Msangani 4.0 400.00 400.00 road (9.5km) Rehab. TAMCO - Vikawe - Mapinga road (24km) 15.0 200.00

155

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Rehab. Nyamisati - Ruaruke - Kibiti road 8.0 100.00 Upgrading to DSD Kibaha town roads (4km) 1.0 200.00 Upgrading to DSD Bagamoyo town roads (2km) 1.0 200.00 Rehabiltation of Makofia - Mlandizi - Mzenga 35km 15.0 80.00 80.00 Rehabilitation of Mbwewe - Lugira road 6.0 80.00 80.00 Rehabilitation of Msoga - Msolwa road 6.0 80.00 80.00 Rehabilitation of Kibiti - Utete road 15.0 105.00 105.00 3 DAR ES SALAAM REGION Upgrading Chanika - Mbande road (Otta seal) 29.6km 1.0 105.00 105.00 Rehabilitation of Kimbiji - Tundwi Songani road 4.0 80.00 80.00 Rehabilitation of Ukonga Mombasa - Msongola road 15.0 105.00 105.00 Upgrading to DSD Mission - Kijichi - Zakhiem road 400.00 400.00 (6.7km)

156

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Up grading to DSD of UDSM Kijitonyama Hostel access 1.5 150.00 150.00 road Upgrading of Banana - Kitunda to DSD 0.5 80.00 80.00 4 DODOMA REGION Rehab. Kolo- Dalai (Mrojochini - Goima section) 6.0 80.00 80.00 Rehab. Mbande - Kongwa - Suguta (Ugogoni - Suguta 80.00 6.0 80.00 section) Rehab. Pandambili - Mlali - Ng'ambi (Mpwapwa - Suguta 80.00 6.0 80.00 section) Rehab. Zemahero - Kinyamshindo (Kwamtoro - 100.00 8.0 100.00 Kinyamshindo section) Upgrading to DSD Shabibu- Dodoma/Arusha round 430.00 2.0 430.00 about 6km Rehab. Mnenia - Itololo - Madege (85km) 6.0 80.00 80.00

157

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Rehab. Manchali Kongwa - Hogoro Jctn (Kongwa - 6.0 80.00 80.00 Hogoro Jctn) 5 IRINGA REGION Rehab. Paved section Iringa - Msembe 0.4 80.00 80.00 Rehab. Paved section Iringa - Pawaga 0.4 80.00 80.00 Rehab. Ndulamo - Nkenja - Kitulo - Mfumbi 95km 4.0 80.00 80.00 Rehab. Mhaji - Lusisi - Ibumila (15km) 6.0 80.00 80.00 Rehab. Igowole - Kasanga - Nyigo (54.8km) 6.0 80.00 80.00 Rehab. Izazi - Mbolimboli - Pawaga - Mlowa road 7.0 90.00 90.00 Rehab. Mkiu - Madaba (79.8km) 6.0 80.00 80.00 Rehab. Iringa - Idete rd (68kms) 6.0 80.00 80.00

Rehab Njombe - Ndulamo - Makete (109.4) 6.0 80.00 80.00

Rehab. Mbalamaziwa - Kwatwanga (50km) 6.0 80.00 80.00

158

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Upgrading Mafinga Township roads( Bomani - Ikulu (0.8 1.0 200.00 200.00 km) &Sokoni - Kiota - Bank road (1.2km) Upgrading to DSD Njombe - Makete road 2.0 1,300.00 1,300.00 Rehab. Lusisi - Kibodago (15kms) 6.0 80.00 80.00 Upgrading to DSD Njombe township roads(CCM and 1.0 400.00 400.00 Kongo Streets - 4km) Upgrading to DSD Makambako railway station acces 0.15 50.00 50.00 road 150m Opening up Lupembe - Madeke - Taveta road 6.0 80.00 80.00 6 KAGERA REGION Rehab. Muhutwe - Kamachumu - Muleba rd 6.0 80.00 80.00 Rehab. Katoma - Kanyigo 6.0 80.00 80.00 Rehab. Buseresere - Kibumba - Makumgusi road 6.0 80.00 80.00

159

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Otta Seal. Bugene - Kaisho - Murongo road (Rwabunuka 1.0 80.00 80.00 Escarpment) Sect.) Rehab. Bukoba - Kabango bay 6.0 80.00 80.00 7 KIGOMA REGION Upgrading to DSD Kibondo township roads (5km) 1.0 315.00 315.00 Upgrading to DSD Kasulu Township roads 1.0 170.00 170.00 Simbo - Ilagala - Kalya (Upgrading to gravel std from 7.0 100.00 100.00 Rugufu bridge) Upgrading of Mwanga - Airport road (3km) 1.0 150.00 150.00 8 KILIMANJARO REGION Upgrading to Otta Seals Mwanga - Kikweni road 2.0 450.00 450.00 Rehabilitation of Holili - Tarakea 8.0 80.00 80.00 Rehab. Arusha road - Umbwe - Kibosho road Kirema 6.0 80.00 80.00

160

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Upgrading to Otta Seal Uru (Rau) - Mlimani road (Remeni 1.0 100.00 100.00 - KNCU Sect.) Rehab. Kibororoni - Mbokumu road 6.0 80.00 80.00 Rehab.Sanya juu - Rongai - 80km 6.0 80.00 80.00 Upgrading to DSD Moshi - TPC Road (21km) 0.4 65.00 65.00 Upgrading to DSD of Kawawa - Pakula - Marangu Mtoni 3.0 2,000.00 2,000.00 Upgrading to DSD of Kibosho Shine- Kwa Raphael road 3.0 2,000.00 2,000.00 Upgrading to DSD Kwasadala-Masama 1.5 1,500.00 1,500.00 Upgrading to DSD of Uru Njari - Rau Madukani (9.5km) 1.0 1,000.00 1,000.00 9 LINDI REGION Rehab. Ngongo - Mandawa Road ( 45Km) 6.00 80.00 80.00 Rehab. Lukuledi II Bridge along Mtama - Nyangamala 1No. 80.00 80.00 Rehab. Nangurukuru - Liwale road 25.0 400.00 400.00 Rehab. Mtanda - Kawawa road to DSD 0.5 120.00 120.00

161

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Rehab. Tingi - Kipatimu(50Km) 9.0 100.00 - 100.00 Rehab. Nanganga - Mandawa(60Km) 15.0 200.00 - 200.00 Rehab. Nachingwea - Liwale(30Km) 20.0 300.00 - 300.00 Rehab. Mtupwa village access road 8.0 100.00 100.00 Rehab. Lindi Airport road (5km) 5.0 80.00 80.00 Rehab. Nachingwea - Kilimarondo(60Km) 12.0 150.00 - 150.00 10 MOROGORO REGION Rehab. Lusanga - Kibati road 6.0 80.00 - 80.00 Rehab. Mvomelo - Dole - Kibati (80km) 6.0 80.00 - 80.00 Protection works at Furua Bridge along Lupiro - Kilosa 1No. 90.00 90.00 Rehab. Mvuha - Kiganila 6.0 80.00 - 80.00 Constr. Magole - Tuliani - Mziha - Handeni (Magole - 0.0 0.00 0.00 Upgrading to otta seal Liwambanjuki hills along Lupiro - 3.0 300.00 300.00 FS & DD Ifakara - Kihansi road 130km 130.0 287.20 287.20

162

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Rehab.Ubena zamozi - Ngerengere road ( Sect. 26+00 - 15.0 100.00 - 100.00 Rehab. Lumemo - Kilosa (50km) 6.0 90.00 - 90.00 Opening up of Kilosa kwa Mpepo - Londo road 40.0 350.00 - 350.00 Construction of Mtibwa Bridge across along 1No. 400.00 - 400.00 11 MBEYA REGION Start of Constr. Of Mpona Bridge along Galula - 1No. 232.05 232.05 Rehab. Chapwa - Nomole - Msangano 6.0 80.00 80.00 Rehab. Ndalambo - Kapole - Ilonga road 6.0 80.00 80.00 Rehab. Mbalizi - Shigamba - Isongole ( Mbalizi - 8.0 100.00 Rehab. Saza - Kapalala 6.0 80.00 80.00 Rehabilitation of Ilongo - Usangu road 6.0 80.00 80.00 Rehabilitation of Kiwila - Isangati road 6.0 80.00 80.00 Rehab. Mlowo - Kamsamba road (Itumba - Kamsamba 6.0 80.00 80.00 Start construction of Mbaka & Mwalisi Bridge along 2No 600.00 600.00

163

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Construction of Mbala bridge along Itungi - Mbala road 1No. 80.00 80.00 Construction of Mbalizi - Makongorosi (Mbalizi - Utengule 150.00 150.00 8km) OTTA SEAL 2.0 12 MANYARA REGION Rehab. Losinyai - Njolo (306km) 6.0 80.00 80.00 Rehab. Kilimapunda - Kidarafa 6.0 80.00 80.00 Rehab. Babati - Orkesumet 15.0 330.00 330.00 Rehab. Handeni - Kibaya - Kongwa road 8.0 100.00 100.00 Start Construction of Magara Bridge along Mbuyu wa 1No. 450.00 450.00 Mjerumani - Mbulu road Start Constr. to DSD KIA - Mererani Road 2.0 2,000.00 2,000.00 Constr. Concrete slab Along Mbuyu wa Mjerumani - 3.0 400.00 400.00 Mbulu (Rift Valley Section) Rehab. Arusha/ Manyara boarder - Mbulu road 6.0 80.00 80.00

164

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Rehab. Mbuyu wa Mjerumani - Mbulu 12.0 150.00 150.00 13 MARA REGION Rehab. Nyamwaga - Mriba - Itiryo - Kegonda road 6.0 80.00 80.00 Rehab. Muriba - Kegonga 6.0 80.00 80.00 Rehab. Murangi - Bugwema 6.0 90.00 90.00 Reh. Bunda - Guta ((Nyamuswa - Bunda) 6.0 90.00 90.00 Rehab. Manyamamanyama - Nyambui 6.0 90.00 90.00 Rehab. Mwanza brd - Sirari (Kyabakari section) 6.0 90.00 90.00 Rehab. Musoma - Tarime jnct (Musoma round about - 6.0 80.00 80.00 Baruti)

Feasibility study of Nyamuswa - Bunda - Kisorya (Bunda 90.00 90.00 - Kisorya - Nansio) 7.0

Rehab.Nyankanga - Rung'abure road 7.0 90.00 90.00 Upgrading to DSD Musoma township roads 0.5 150.00 150.00

165

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje 14 MTWARA REGION Rehab. Mnongodi -Mdenganamadi - Kilimahewa - 8.0 100.00 100.00 Michenjele (boarder road) Construction of Lukwamba bridge along Mnongodi - 1No 150.00 150.00 Mdenganamadi - Kilimahewa - Michenjele (boarder road) Rehab. Magamba - Mitema - Upinde Rd.297km) 8.0 100.00 100.00 Rehab. Newala - Mkwiti - Mtama road ( Amkeni - Mkwiti 8.0 100.00 100.00 Section) Detailed design Mangaka - Mtambaswala 0.0 - 0.00 15 MWANZA REGION Rehab. Geita - Nyang'hwale road 55km 6.0 80.00 80.00 Rehab. Magu - Kabila - Mahaha road 6.0 80.00 80.00 Rehab. Nyashimo - Ngasamo road 6.0 80.00 80.00 Rehab. Busisi - Nyang'wale 6.0 80.00 80.00 Upgrading to DSD - Sengerema Township roads 1.0 200.00 200.00 166

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Rehab. Bugando - Nyanguge road 4.0 60.00 60.00 Rehab. Nyang'hwale - Nyanholongo road 6.0 80.00 80.00 Rehab. Geita - Nzera - Kome road - 54km 6.0 80.00 80.00 Rehab. Bukongo - Rubya - Bukongo - Masonga road 6.0 80.00 80.00 Rehab. Katoro - Ibondo- Busanda - Kamena road 12.0 150.00 150.00 Construction of by- pass Mwanza Airport - Kayenze road 12.0 150.00 150.00 (17km) Upgrading to DSD Mwanza urban roads 1.0 600.00 600.00 Rehab. Runele - Gatuli 7km 6.0 80.00 80.00 Rehab.Mwanangwa - Misasi - Salawe (49.7km) 6.0 80.00 80.00 Rehab. Lamadi - Mkula - Sapiwi (16km) 6.0 80.00 Rehab. Ngudu - Malya road 6.0 80.00 Rehab. Ngudu - Nyamilama - Hungumalwa (26km) 6.0 80.000 80.00 16 RUKWA REGION

167

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Rehab. Kagwira - Karema (112) 6.0 80.00 80.00 Rehabilitation Mamba - Kasanza - Muze 6.0 80.00 80.00 Rehab. Laela - Mwimbi - Kizombwe 6.0 80.00 80.00 Upgrading to DSD Sumbawanga township roads 1.0 200.00 200.00 Upgrading to DSD Mpanda township roads 1.0 200.00 200.00 Rehab. of Kalepula Junction - Mambwenkoswe 6.0 80.00 80.00 Rehab Nkundi - Kate - Namanyere 6.0 80.00 80.00 Rehab Sitalike - Kilyamatundu 6.0 80.00 80.00 Rehab. Inyonga - Ilunde road 6.0 80.00 80.00 Rehab Kaengesa - Mwimbi 7.0 90.00 90.00 17 RUVUMA REGION Construction relief culvert at Ruvuma Bridge at Mitomoni 1No. 100.00 100.00 Village

168

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Construction of box culverts at Londo and its approach 1No. 100.00 100.00 roads (Lumecha - Kitanda - Londo rd) Rehab. Nyoni - Kipapa -Chamani-Mkoha 15km 6.0 100.00 100.00 Rehab of Wino - Ifinga road 6.0 80.00 80.00 Rehab. Lumecha - Kitanda - Londo road (Kitanda - 8.0 100.00 100.00 Londo Section.) Ruvuma/ Morogoro Boarder Upgrading to DSD Songea airport road (2.2km) 1.2 500.00 500.00 Upgrading Hanga - Kitanda (Mhangazi sect.) ( otta Seal) 1.0 170.00 170.00 Rehab. Mbinga - Mbuji - Litembo - Mkili road (Mbinga - 6.0 80.00 80.00 Litembo Sect.) Rehab. Nangombo - Chiwindi road (Ng'ombo - Chiwindi 6.0 80.00 80.00 Sect) Rehab. of Songea (Likuyufusi) - Mitomoni road 0.5 150.00 150.00

169

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Realignment chainage 50+000 - 75+000 along 8.0 100.00 100.00 Mbababay - Lituhi road Detailed Design and Construction of Kalulu Bridge along 1No. 615.00 615.00 Matemanga - road Rehab. Liuli - Lituhi Road 8.0 100.000 100.00 FS & DD Ruhuhu bridge (Ruvuma/Iringa Border) at 1No 150.00 150.00 Lituhi Upgrading of Lumecha - Kitanda - Londo Road (Hanga 1.0 150.00 150.00 Section) to Otta Seal 18 SINGIDA REGION Rehab.Manyoni - Ikasi 6.0 80.00 80.00 Rehab.Ulemo - Gumanga - Sibiti 6.0 80.00 80.00 Rehab.Ikungi - Kilimatinde 6.0 80.00 80.00 Rehab. Chemchem - Sibiti 6.0 80.00 80.00

170

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Rehab.Mwamanoni - Mkalama - Haidom road 12.0 150.00 150.00 Rehab. Kititimo - Kinyamshindo road 6.0 80.00 80.00 Rehab. Singida - Mwangoko-Kinkandaa- Mtunduru- 6.0 80.00 80.00 Ighombwe - Mguigira road Rehab. Kisaga - Sepuka - Mlandala (Sepuka - Mlandala 8.0 100.00 100.00 Sect.) 19 SHINYANGA REGION Rehab Kahama - Chambo road 12.0 140.00 140.00 Rehab. Ushirombo - Buseresere road 6.0 80.00 80.00 Rehab. Sola - Bushashi road 6.0 80.00 80.00 Rehab. Bariadi - Nguliati - Mwamlapa road 6.0 80.00 80.00 Upgrading to DSD Kahama township roads (5.5km) 1.0 200.00 200.00 Construction of Gamaloha bridge 1No 200.00 200.00 Construction of Bukingwaminzi bridge 1No 200.00 200.00

171

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Design and Start Construction of Lubiga bridge along 1No. 250.00 250.00 Rehab. Old Shinyanga - Salawe road 8.0 100.000 100.000 20 TABORA REGION Rehab Puge - Ziba 6.0 80.00 80.00 Rehab. Usagali - Fuluma - Ndono road (38km) 6.0 80.00 80.00 Construction of the bridge along Lusu - Nzega road 1No. 80.00 80.00 Rehab. Kaliua - Uyowa - Makazi road road 8.0 100.00 100.00 Rehab. Mambali - Bukene 8.0 100.00 100.00 Rehab. Ibologero - Igurubi 8.0 100.00 100.00 Upgrading to DSD. Igunga District roads 8.0 150.00 150.00 Rehab. Sikonge - Usoke road 8.0 100.00 100.00 Rehab. Muungano- Jionee- Songambele - Uyogo Road 12.0 140.00 140.00 Rehab. Tabora - Kigwa - Tabora/Singida Brd 7.0 90.000 90.00 21 TANGA REGION

172

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje Rehab. Lushoto - Mlalo 6.0 80.00 80.00 Upgrading to DSD Mombo -Lushoto - Magamba 1.0 150.00 150.00 Upgrading Korogwe Township roads 0.5 150.00 150.00 Upgrading to DSD - Tanga - Pangani 0.5 150.00 150.00 Upgrading to DSD Handeni Township roads 0.5 150.00 150.00 Rehab. Handeni –Kiberashi - Songe 8.0 100.00 100.00 Rehab. Kwekivu - Kwalugalu Road 8.0 100.00 100.00 22 DONOR FUNDED PROJECTS RSPS -3 DANIDA - 9,870.00 9,870.00 WORKS/TANROADS 1,091.65 36,449.25 9,870.00 46,319.25 SUPERVISION TANROADS B: RSPS -3 DANIDA - 130.00 130.00 D: JICA (ATTI) - 231.60 231.60 23 MONITORING (MOID) 260.00 260.00

173

MAKADIRIO 2010/11 km/ JINA LA MRADI (sh. Mio) JUMLA madaraja Fedha za Fedha za

ndani nje TOTAL CONSOLIDATED (Sub - total 1) 1,091.65 36,709.25 10,231.60 46,940.85

& 16 brg

174

KIAMBATANISHO NA.3

Miradi ya Barabara za Mikoa inayotekelezwa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara 2010/11

MAKADIRIO 2010/11 (Sh. Mio) km/ JINA LA MRADI km/ madaraja madaraja Fedha za Fedha za ndani nje

ARUSHA REGION

Rehab. Longido - Kitumbeine - Lengai. 8.0 100.00 100.00 (Kitumbeine - Lengai Sect.) Rehab. Msitu wa Mbogo (Karangai) - Nelson 8.0 100.00 100.00 Madela Institute (10km) COAST REGION

Rehab. Kisarawe - Masaki - Msanga-Chole Road 6.0 80.00 80.00

175

MAKADIRIO 2010/11 (Sh. Mio) km/ JINA LA MRADI km/ madaraja madaraja Fedha za Fedha za ndani nje

Upgrading to DSD Kwa Matias - Nyumbu - 8.0 90.00 90.00 Msangani road (9.5km) Purchase of Mafia roads (Purchase of excavator 1 set 150.00 150.00 and W/bowser) DAR ES SALAAM REGION Rehab. Uhuru Road -1km 0.5 100.00 100.00 Upgrading Chanika - Mbande road DSD 29.6km 1.00 100.00 100.00 Upgrading to DSD Feri - Tungi Kibada road 1.00 150.00 150.00 Upgrading of Mzinga - Way to DSD 0.50 200.00 200.00 Upgrading Boko - Mbweni road to DSD (6.9km) 1.00 300.00 300.00 Upgrading of Banana - Kitunda to DSD 0.50 100.00 100.00 DODOMA REGION Rehab. Izava - Dosidosi road (15km) 8.0 100.00 100.00 IRINGA REGION

176

MAKADIRIO 2010/11 (Sh. Mio) km/ JINA LA MRADI km/ madaraja madaraja Fedha za Fedha za ndani nje

Rehab. Izazi - Mbolimboli - Pawaga - Mlowa road 8.0 100.00 100.00 KAGERA REGION Rehab. Kajai Swamp along Katoma - Bukwali road 1.0 100.00 100.00 KIGOMA REGION Upgrading Airport - Ujiji road to DSD (3.5km) 0.5 150.00 150.00 Upgrading to DSD Hospitali - Kitahana Centre 0.5 130.00 130.00 LINDI REGION Mbwemkuru - Nanjilinji - Kiranjeranje (134km) 8.0 100.00 100.00 Rehab. Nangurukuru - Liwale road 8.0 100.00 100.00 MANYARA REGION Construction of Babati - Orkesumet/Kibaya New 15.0 200.00 200.00 Rehab Kibaya - Kibereshi road 92 km 5.0 70.00 70.00 Rehab. Nangwa - Gisambang - Kondoa Brd. 12.0 150.0 150.0 Rehab Mogitu - Hydom 68 Km 5.0 70.00 70.00

177

MAKADIRIO 2010/11 (Sh. Mio) km/ JINA LA MRADI km/ madaraja madaraja Fedha za Fedha za ndani nje

MARA REGION Rehab. Musoma - Makojo road 5.0 70.00 70.00 Rehab. Balili - Mgeta - Manchimweli - Rimwani 5.0 70.00 70.00 road Upgrading to DSD Bunda - Kisorya - Nansio road 0.5 140.00 140.00 (Nansio - Kisorya sect.) Upgrading to DSD Mika - Utegi - Shirati road 0.5 120.00 120.00 (60km) Upgrading to DSD Tarime - Nyamwaga road - 1.0 120.00 120.00 25km (Tarime - Nyamigura Sect) Otta Seal - MBEYA REGION Rehab. of Gagula - Namkukwe road (57km) 12.0 150.00 150.00 Rehab. Mbalizi - Shigamba - Isongole (Mbalizi - 8.0 100.00 100.00 Shigamba Sect 52km)road

178

MAKADIRIO 2010/11 (Sh. Mio) km/ JINA LA MRADI km/ madaraja madaraja Fedha za Fedha za ndani nje

Upgrading to DSD Igawa - Rujewa - Ubaruku 0.5 140.00 140.00 Rehab. Rujewa - Madibira road 83.1km 6.0 80.00 80.00 Construction of Mbalizi - Makongorosi ( Mbalizi - 1.0 150.00 150.00 Utengule 8km) OTTA SEAL Rehab. Ilongo - Usangu road 6.0 80.00 80.00

Raising Embakment Msangano - Tindingoma 1.0 120.00 120.00 (6km section) road MOROGORO REGION

Rehab. Mahenge - Mwaya road ( 40km) 8.0 100.00 100.00

Upgrading "kilima Simba" (Otta Seal) along 0.5 150.00 150.00 Mahenge - Mwaya Road Rehab Ifakara - Taweta rd (206km) 7.0 90.00 90.00

179

MAKADIRIO 2010/11 (Sh. Mio) km/ JINA LA MRADI km/ madaraja madaraja Fedha za Fedha za ndani nje

MTWARA REGION

Upgrading to DSD Newala Township roads (5km) 0.5 150.00 150.00 Rehab.Tandahimba - Litehu Mkwiti Road 6.0 80.00 80.00 MWANZA REGION Rehab. Kayanze - Nyanguge road 5.0 70.00 70.00 Rehab. Chibingo - Bukondo road - 37km 5.0 70.00 70.00 Rehab. Kabaganga Ferry - Mugogo - Nyakabanga 3.0 50.00 50.00 Rehab. Magu - Ngudu - Jojiro road (64km) 6.0 80.00 80.00 Rehab. of Geita - Nkome Mchangani 5.0 70.00 70.00 Rehab. of Lumaji - Nyanshana (14km) 5.0 70.00 70.00 Rehab. of Geita - Nyarugusu - Bukoli 6.0 70.00 70.00 Construction of Sukuma( Simiyu II ) bridge along 1No. 100.00 100.00 Magu - Mahaha road Rehab Inonelwa - Kawekamo 5.0 70.00 70.00 180

MAKADIRIO 2010/11 (Sh. Mio) km/ JINA LA MRADI km/ madaraja madaraja Fedha za Fedha za ndani nje

Rehab Mwamhaya - Itongoitale 5.0 70.00 70.00 Rehab.Nyambiti - Fulo road 5.0 70.00 70.00 Rehab Misasi - Mbarika road (43km) 5.0 70.00 70.00 RUKWA REGION Rehab. Mamba - Kasanza - Muze 4.0 60.00 60.00 Rehab. Ntendo - Muze (39km)Kizungu hill section 0.5 90.00 90.00 to DSD Rehab. Miangalua - Kipeta road (km 52) 7.0 90.00 90.00 Rehab. Mpanda - Ugala road 7.0 90.00 90.00 Rehab. Inyonga - Majimoto (135km) 15.0 200.00 200.00 RUVUMA REGION Rehab. Azimio - Tulingane - Lukumbule road 12.0 150.00 150.00 Rehab.of Lilondo Quarry Plants. set 200.00 200.00

181

MAKADIRIO 2010/11 (Sh. Mio) km/ JINA LA MRADI km/ madaraja madaraja Fedha za Fedha za ndani nje

Opening up Londo - Kilosa Kwa Mpepo road 20.0 250.00 250.00 Section F.S and DD of Songea - Mitomoni road (120km) 120.0 300.00 300.00 Rehab. Chamani - Matuta - Mango - Kihagara road 2.8 51.00 51.00 Upgrading to DSD Kilimo Mseto - Makambi road 200.00 (2km) 1.0 200.00 Rehab. Nalasi - Sasawala road (26km) 7.0 90.00 90.00 Construction of Londo bridge approach road - Otta

Seal ( 1km ) along Kitanda - Londo (Ruvuma/ 160.00 160.00 1.0 Morogoro Brd) SHINYANGA REGION

Rehab. Kadoto -Kinamweli - Luguru Lagangabilili - 8.0 100.00 100.00 Bumera road 63km (Luguru Lagangabilili -

182

MAKADIRIO 2010/11 (Sh. Mio) km/ JINA LA MRADI km/ madaraja madaraja Fedha za Fedha za ndani nje

Upgrading to DSD Shinyanga - Old shinyanga road 0.5 150.00 150.00

Rehab. Maganzo - Maswa - Bariadi - Mkula - 5.0 70.00 70.00 Lamadi road Rehab. Maswa - Kadoto - Shishiyu - Jiju road 8.0 100.00 100.00 Rehab. Isagenye - Budekwa - Mabaraturu road 8.0 100.00 100.00 Rehab. Mkoma - Makao road 8.0 100.00 100.00 TABORA REGION Rehab. Tutuo - Izimbili - Usoke (70km) 4.0 61.00 61.00 Rehab. Nzega - Itobo - Bukooba (54.5km) 6.0 80.00 80.00 TANGA REGION

Rehab Mlalo - Mng'aro road (25km) 8.0 100.00 100.00 Rehab.Muheza - Maramba (41km) 8.0 100.00

183

MAKADIRIO 2010/11 (Sh. Mio) km/ JINA LA MRADI km/ madaraja madaraja Fedha za Fedha za ndani nje

Upgrading to OTTA Seal Korongwe - Kwengoma- 1.0 100.00 Sindeni (14km) 100.00 Rehab Mbaramo - Misozwe - Maramba - Kasera 7.0 90.00 90.00 road (90km) MOID ( Monitoring and Road Related Activities) 200.00 200.00 SPECIFIC ROAD RELATED PROJECTS: ATTI (Taking Labour Based Technology to Scale) 78.00 78.00 MWTI 105.00 105.00 WPU 45.87629 45.88 ROAD FUND ( Sub - Total 2 ) 357.80 9,020.87629 9,020.87629 & 1 brg

184

KIAMBATANISHO NA.4

Miradi ya Maendeleo inayotumia fedha za Mfuko wa Barabara, 2010/11

Na Kasma Jina la Mradi Makadirio (Tsh,Mio)

1 2326 Kirumi Bridge Study & Rehabilitation 100.00 2 2326 Bagamoyo ‐ Saadani ‐ Tanga (FS & DD) 200.00 3 2326 Sumbawanga ‐ Matai ‐ Kasesya Border(Matai‐Kasesya section DD) 200.00 4 2326 Nzega ‐ Tabora (Rehabilitation Gravel) 100.00 5 2326 Sumbawanga ‐ Mpanda ‐ Kanyani ‐ Nyakanazi ( FS & DD ) 200.00 6 2326 Training & Technical Assistance TANROADS 200.00 7 2326 Dar es Salaam Outer Ring Road (Acquisition) 300.00 8 2326 Mkuranga ‐ Kibiti 200.00 9 2326 Same ‐ Kisiwani ‐ Mkomazi 250.00 10 2326 Tabora ‐ Ipole ‐ Rungwa Road (Rehab to gravel) 200.00 11 2326 Ipole ‐ Koga (Rehabilitation Gravel) 200.00 185

12 2326 Mpanda ‐ Koga (Rehabilitation Gravel) 200.00 13 2326 Rungwa ‐ Itigi ‐ Mkiwa Road (Rehabilitation Gravel) 200.00 14 2326 Makongolosi ‐ Rungwa Road (Rehabilitation gravel) 200.00 15 2326 Magole ‐ Mziha ‐ upgrading (FS & DD) 200.00 16 2326 Tabora ‐ Koga ‐ Mpanda (FS & DD) 300.00 17 2326 Updating of Draft Design Manual (1989) & Economic Appraisal 300.00 18 2326 Arusha ‐ Moshi ‐ Voi & Arusha Bypass (Study) 930.00 19 2326 Nyamswa ‐ Bunda ‐ Kisorya ‐ Ukerewe road (FS & DD) 300.00 21 2326 Kyaka ‐ Bugene‐Kasulo/Benako (FS & DD) 620.00 22 2326 Makongolosi ‐ Rungwa ‐ Itigi ‐ Mkiwa Road (FS and DD) 700.00 23 2326 Handeni ‐ Kiberashi ‐ Kijungu ‐ Kibaya ‐ Njoro ‐ Olboloti ‐ Mrijo Chini ‐ 500.00 Dalai ‐ Bicha ‐ Chambalo ‐ Chemba ‐ Kwamtoro ‐ Singida (FS & DD)

24 2326 New Wami Bridge (Feasibility Study and Detailed Design) 400.00 25 2326 Kidatu ‐ Ifakara ‐ Lupilo ‐ Malinyi ‐ Londo ‐ Lumecha (Songea) (FS) 300.00 26 2326 CML‐Drilling Ring for Geotechnical Investigation 300.00 27 2326 Mafinga‐Igawa (FD & DD) 810.00 28 2326 Same ‐ Himo ‐ Marangu & Mombo‐Lushoto 680.00 29 2326 Makambako‐Songea 1330.00 186

30 2326 Mtwara‐Mingoyo‐Masasi 1070.00 31 2326 Kobero‐Nyakasanza & Lusahunga‐Rusumo 810.00 32 2326 Road Flyovers compesation 150.00 33 2326 Mtwara – Newala – Masasi including Mwiti Bridge (FS & DD) 300.00 34 2326 Shifting of Kibaha weigh bridge to Misugusugu 500.00 35 2326 Environmental Impact Assesment (EIA) of Rusumo Bridge in Kagera 150.00 36 2326 Environmental Impact Assesment (EIA) of Chalinze ‐ Segera road 350.00 37 2326 Monitoring and other road related activities (MOID) 200.00 38 2326 Roads Related Administrative Activities 1,011.70 39 2326 Procurement of Ferries 1,585.48 40 2326 Regional Roads Rehabilitation 9,020.87

JUMLA 19,717.957

187

KIAMBATANISHO 5A

SUMMARY OF ROADS FUND MAINTENANCE PROGRAMME FY 2010/11

TRUNK ROADS

ANNUAL PLAN

PHYSICAL FINANCIAL(Tshs. mio.) S/NO MAINTENANCE ACTIVITY

ROAD FOR UNIT QTY FUND EIGN TOTAL

Routine & Recurrent - km 4,313.77 8,240.190 - 8,240.190 1.0 Paved Routine & Recurrent - km 5,039.72 6,493.192 - 6,493.192 2.0 Unpaved Periodic Maintenance - km 319.35 32,361.520 - 32,361.520 3.0 Paved

188

Periodic Maintenance - km 516.57 9,319.010 - 9,319.010 4.0 Unpaved Spot Improvement - km 8.43 651.221 - 651.221 5.0 Paved Spot Improvement - km 64.02 917.597 - 917.597 6.0 Unpaved Bridges Preventive Nos. 1,168 1,308.381 - 1,308.381 7.0 Mtce 8.0 Bridges Major Repairs Nos. 53 2,812.799 - 2,812.799 Contribution to Donors km - - - 10.0 Programmes (PMMR) SUB-TOTAL Routine & Kms Recurrent 9,353.49 14,733.382 - 14,733.382 SUB-TOTAL Periodic & Kms Spot Maintenance 908.37 43,249.348 - 43,249.348 SUB-TOTAL Bridges Nos. TOTAL TRUNK ROAD BUDGET 62,103.910

189

REGIONAL ROADS

ANNUAL PLAN S/NO MAINTENANCE ACTIVITY PHYSICAL FINANCIAL (Tshs. mio.) UNIT QTY ROAD FOR TOTAL FUND EIGN Routine & Recurrent - 1.0 km Paved 730.18 913.743 - 913.743 Routine & Recurrent - 2.0 km Unpaved 17,093.06 18,988.806 - 18,988.806 Periodic Maintenance - 3.0 km Paved 67.76 16,222.100 - 16,222.100 Periodic Maintenance - 4.0 km Unpaved 1,767.73 24,914.605 - 24,914.605 Spot Improvement - 5.0 Paved km 8.80 431.000 - 431.000

Spot Improvement - 6.0 km Unpaved 387.24 5,907.072 - 5,907.072

190

Bridges Preventive 7.0 Nos. 1,132 Mtce 1,684.188 - 1,684.188 8.0 Bridges Major Repairs Nos. 79 Contribution to Donors 10.0 km Programmes 1,076.00 10,267.464 - 10,267.464 SUB-TOTAL Routine & Kms Recurrent 17,823.24 19,902.549 - 19,902.549 SUB-TOTAL Periodic & Kms Spot Maintenance 2,231.53 47,474.777 - 47,474.777 SUB-TOTAL Bridges Nos. TOTAL REGIONAL ROAD BUDGET Routine & Kms Recurrent 27,176.73 GRAND TOTAL TRUNK & Periodic & Kms REGIONAL ROADS(Works) Spot 3,139.90 149,835.176 - 149,835.176 Bridges Bridg es 2,432

191

EMERGENCY

1.0 Emergency and Urgent Works 3,054.248 - 3,054.248 2.0 Contingencies 1,000.000 - 1,000.000 SUB-TOTAL 4,054.248 - 4,054.248

HQ BASED MAINTENANCE ACTIVITIES

1.0 Road Mtce Manag. 300.000 - 300.000 Systems 2.0 Road Data Collection 300.000 - 300.000 Bridge Mtce 3.0 200.000 - 200.000 Management System 4.0 Road Safety 1,400.000 - 1,400.000 5.0 Road Act Enforcement 600.000 - 600.000 SUB-TOTAL 2,800.000 - 2,800.000

192

ADMINISTRATION AND SUPERVISION

1.0 Administration Cost 6,116.862 - 6,116.862 2.0 Supervision Cost 9,855.327 - 9,855.327 SUB-TOTAL 15,972.189 - 15,972.189

WEIGHBRIDGE OPERATIONS

1.0 Mechanical and Electronic Repairs 1,000.000 - 1,000.000 2.0 Weighbridge Operations 3,800.000 - 3,800.000 SUB-TOTAL 4,800.000 - 4,800.000 TOTAL ROADS FUND 177,461.613 - 177,461.613

193

TRUNK ROADS: Routine/Recurrent Maintenance for FY 2010/11 5B(i) Estimated Expenditure in 0.941 Tshs mio. Paved Trunk Roads FY 2010/11 Target Total Estimate Routine and Recurrent (km) Maintenance Roads Fund Foreign Arusha 219.37 495.352 - 495.352 Coast 312.60 631.398 - 631.398 Dar es Salaam 120.40 404.630 - 404.630 Dodoma 202.04 284.904 - 284.904 Iringa 369.30 614.485 - 614.485 Kagera 225.60 595.907 - 595.907 Kigoma 1.07 0.036 - 0.036 Kilimanjaro 231.61 506.523 - 506.523 Lindi 333.30 370.754 - 370.754 Manyara 10.14 11.330 - 11.330 Mara 170.72 306.982 - 306.982

194

Mbeya 359.42 884.537 - 884.537 Morogoro 403.00 880.625 - 880.625 Mtwara 147.50 137.414 - 137.414 Mwanza 282.14 504.048 - 504.048 Rukwa 1.90 5.006 - 5.006 Ruvuma 185.23 531.134 - 531.134 Shinyanga 141.01 202.150 - 202.150 Singida 192.30 251.190 - 251.190 Tabora 148.50 140.510 - 140.510 Tanga 256.62 481.274 - 481.274 Sub-Total 4,313.77 8,240.190 - 8,240.190

195

5B(ii)

Estimated Expenditure in Tshs mio.

Unpaved Trunk Roads Target FY 2010/11 Total Routine and Recurrent (km) Maintenance Roads Fund Foreign Estimate Arusha 37.00 58.060 - 58.060 Coast 1.00 0.805 - 0.805 Dar es Salaam - - - - Dodoma 355.00 423.653 - 423.653 Iringa 382.90 464.433 - 464.433 Kagera 323.20 221.880 - 221.880 Kigoma 567.22 747.259 - 747.259 Kilimanjaro - - - - Lindi - - - - Manyara 31.04 38.346 - 38.346 Mara 241.55 289.828 - 289.828 Mbeya 271.55 436.962 - 436.962 Morogoro 276.90 189.291 - 189.291 196

Mtwara 113.13 81.796 - 81.796 Mwanza 17.44 14.496 - 14.496 Rukwa 392.84 852.072 - 852.072 Ruvuma 629.20 723.177 - 723.177 Shinyanga 275.85 470.497 - 470.497 Singida 308.70 392.035 - 392.035 Tabora 815.20 1,088.601 - 1,088.601 Tanga - - - - Sub-Total 5,039.72 6,493.192 - 6,493.192 Total Trunk Roads Routine/Recurrent Maintenance (TShs. Mio.): Target Roads Fund Foreign Total 9,353.49 14,733.382 - 14,733.382

197

REGIONAL ROADS: Routine/Recurrent Maintenance for FY 2010/11 KIAMBATANISHO 5B(iii) Estimated Expenditure in Tshs mio.

Paved Regional Roads Target FY 2010/11 Total Routine and Recurrent (km) Maintenance Roads Fund Foreign Estimate Arusha 19.46 26.348 - 26.348 Coast 15.70 17.504 - 17.504 Dar es Salaam 129.03 175.967 - 175.967 Dodoma 11.95 25.473 - 25.473 Iringa 21.00 92.905 - 92.905 Kagera 172.44 71.648 - 71.648 Kigoma - - - - Kilimanjaro 109.72 242.622 - 242.622 Lindi 30.22 33.876 - 33.876 Manyara 7.32 6.841 - 6.841 Mara 22.67 44.674 - 44.674 Mbeya 21.76 6.695 - 6.695 198

Morogoro 38.49 44.846 - 44.846 Mtwara 37.56 31.339 - 31.339 Mwanza 15.56 14.198 14.198 Rukwa 1.50 3.95 - 3.952 Ruvuma 13.60 1.900 - 1.900 Shinyanga 6.00 3.156 - 3.156 Singida 10.60 8.587 - 8.587 Tabora 6.30 5.760 - 5.760 Tanga 39.30 55.452 - 55.452 Sub-Total 730.18 913.743 - 913.743

199

5B(iv)

Estimated Expenditure in Tshs mio.

Unpaved Regional Roads Target FY 2010/11 Routine and Recurrent (km) Maintenance Roads Fund Foreign Total Estimate Arusha 548.03 459.223 - 459.223 Coast 728.30 798.457 - 798.457 Dar es Salaam 333.60 381.105 - 381.105 Dodoma 978.33 661.914 - 661.914 Iringa 1,148.50 1,131.097 - 1,131.097 Kagera 822.82 1,066.774 - 1,066.774 Kigoma 328.88 371.371 - 371.371 Kilimanjaro 490.89 498.786 - 498.786 Lindi 913.92 802.673 - 802.673 Manyara 1,354.44 1,425.239 - 1,425.239 Mara 775.95 1,040.231 - 1,040.231 Mbeya 1,409.34 1,379.506 - 1,379.506 Morogoro 893.80 1,340.555 - 1,340.555 200

Mtwara 741.89 781.163 - 781.163 Mwanza 688.19 691.599 - 691.599 Rukwa 1,028.80 1,540.514 - 1,540.514 Ruvuma 978.88 990.722 - 990.722 Shinyanga 934.30 1,486.780 - 1,486.780 Singida 758.90 654.500 - 654.500 Tabora 558.10 463.215 - 463.215 Tanga 677.20 1,023.381 - 1,023.381

Sub-Total 17,093.06 18,988.806 - 18,988.806 Total Regional Roads Routine/Recurrent Maintenance (Tshs mio.):

Target Roads Fund Foreign Total 17,823.24 19,902.549 - 19,902.549 Total Trunk & Regional Roads Routine/Recurrent Maintenance (Tshs mio.): Target Roads Fund Foreign Total 27,176.73 34,635.931 - 34,635.931

201

DETAILS OF PERIODIC MAINTENANCE KIAMBATANISHO 5C(i) PAVED TRUNK ROADS

Region Road Name Length (km) Estimate (Tshs mio) ARUSHA KIA JCT - TCA JCT 9.00 900.000 TCA JCT - Minjingu 13.00 1,301.170 Makuyuni - Ngorongoro Gate 2.00 200.000 Sub-total 24.00 2,401.170 COAST Kongowe - Mkuranga - Kibiti 10.60 581.900 Mlandizi-Chalinze - Ngerengere 5.30 1,174.800 Kibiti - Nyamwage 8.00 702.200 Bunju - Bagamoyo 6.00 455.000 Sub-total 29.90 2,913.900 DAR ES SALAAM Nyerere road 2.00 1,500.000 Morogoro Road 1.00 500.000 Kilwa Road 5.00 300.000 Road Safety Measures 202

Street Light 503.000 Road Markings and signs 200.000 Traffic Signals 350.000 Sub-total 8.00 3,353.000 DODOMA Gairo - Dodoma - Kintinku 5.00 963.600 Mtera - Dodoma - Bereko 1.20 443.200 Sub-total 6.20 1,406.800 IRINGA Tanzam Highway 12.00 1,200.000 Makambako - Lukumburu 10.00 254.000 Sub-total 22.00 1,454.000

KAGERA Mutukula-Bukoba-Kagoma-Kalebezo 31.00 617.000 Rusumo - Lusahunga 7.80 867.000 Kobero - Ngara - Nyakasanza 19.60 346.000 Bukoba - Bukoba Port 2.00 50.000 Sub-total 60.40 1,880.000 KIGOMA Urban trunk road 3.00 450.000 KILIMANJARO Same - Himo Jct 3.00 250.000

203

Himo Jct - Kia Jct 6.00 600.000 Himo - Marangu 2.00 120.000 KIA Jct - KIA 0.80 120.000 Sub-total 11.80 1,090.000 LINDI Malendego - Nangurukuru 18.20 835.000 Mingoyo - Mtegu 20.70 607.000 Mingoyo - Mkungu 6.40 190.000 Sub-total 45.30 1,632.000

MARA Musoma town - Makutano (Sirari Jnct) 2.00 240.000

Makutano - Sirai (overlay) 13.00 2,600.000

Sub-total 15.00 2,840.000 Uyole - Ibanda - Kasumulu (Tanz/Malawi MBEYA brd) 2.00 600.000

Ibanda - Itungi Port 5.60 221.000

204

TANZAM (Iyayi - Tunduma ) 6.00 624.000 Mbeya - Rungwa 1.90 243.000 Sub-total 15.50 1,688.000 MOROGORO Tanzam Highway 10.30 1,541.000 Morogoro - Dodoma (Parking, Shoulders & Walkway) 2.00 40.000 Mikumi - Kidatu - Mahenge 6.70 1,001.000 Morogoro - Bigwa - Bigwa JCT 1.80 246.000 Sub-total 20.80 2,828.000 MTWARA Mtwara - Mtegu 6.85 650.000 Mkungu - Masasi 12.00 980.050 Sub-total 18.85 1,630.050 MWANZA Mwanza - Mara bdr (Overlay Igoma Area) 2.00 400.000 Mwanza - Shinyanga bdr 16.00 3,200.000 Sub-total 18.00 3,600.000 RUVUMA Songea -Lukumbulu 15.00 2,290.000 Songea - Mbinga - Mbambabay 2.00 300.000 Songea Urban roads 1.00 200.000 Sub-total 18.00 2,790.000 205

TABORA Singida/Tabora brd - Nzega 2.00 350.000 Tabora (Isike NBC) - Urambo 0.60 54.600 Sub-total 2.60 404.600 GRAND TOTAL 319.35 32,361.520

206

DETAILS OF PERIODIC MAINTENANCE KIAMBATANISHO 5C(iii)

PAVED REGIONAL ROADS Estimate (Tshs Region Road Name Length (km) mio) ARUSHA Monduli - Engaruka 2.80 178.000 Mbauda - Losinyai 6.30 398.000 Usa river - Oldonyosambu 1.80 114.000 Sub-total 10.90 690.000 COAST Mkurunga - Kisiju 0.50 120.000 Pugu - Vikumburu 4.10 94.000 Sub-total 4.60 214.000 DAR ES Tabata Jct (Mandela rd) - Kinyerezi - SALAAM Banana 2.00 600.000 Ukonga jct - G/Mboto - Chanika (widening) 2.00 1,600.000 Buyuni - Ununio - Boko upgradding to bituminous 2.00 1,600.000

Kivukoni - Tungi 1.50 1,000.000

207

Mwenge - Mlalakuwa (drainage) 2.00 600.000 Moroco - Kawe jct - TPDF Range - Afrikana (Old Bagamoyo road) 2.00 450.000 Mbweni Jct - Mbweni upgradding to bituminous 3.00 2,400.000 Kawe Jnt - Lugalo 1.50 200.000 Sub-total 16.00 8,450.000 DODOMA Bahi rd - Airport R.A 0.86 155.600 Sub-total 0.86 155.600 IRINGA Iringa - Idete 4.00 800.000 Kikondo - Makete - Njombe 5.00 500.000 Sub-total 9.00 1,300.000 KAGERA Kanazi - Bulila 1.60 120.000 Muhutwe - Kamachumu - Muleba 140.000 200 Sub-total 3.60 260.000 KILIMANJARO KMT - Machame 1.00 170.000 Sub-total 1.00 170.000 LINDI K/Masoko - Nangurukuru 1.00 100.000 Sub-total 1.00 100.000 208

MANYARA Mbulu town (Kilimapunda - Kidarafa) 1.60 800.000 Dareda - Dongobeshi (Darbil escarp.) Section 1 1.00 500.000 Sub-total 1,300.000 Musoma - Makoko (Musoma Town 260 MARA roads) 2.00 400.000 Sub-total 400.000 200 MOROGORO Morogoro - Old Dar es salaam road 1.00 100.000 Sub-total 1.00 100.000 MTWARA Mbuyuni - Nambunga 1.00 110.000 Nanyamba - Mangamba - Magomeni 0.80 95.500 Sub-total 1.80 205.500 MWANZA Magu - Ngudu - Jojiro (Ngudu Town) 2.20 600.000 Sub-total 2.20 600.000 RUKWA Sumbawanga Town (Regional Block) 1.00 100.000 Sub-total 1.00 100.000 SHINYANGA Shinyanga - Bubiki 1.00 200.000 Sub-total 1.00 200.000 SINGIDA Misigiri - Kiomboi 6.20 1,800.000 209

Sub-total 6.20 1,800.000 TANGA Mombo - Lushoto 3.00 177.000 Sub-total 3.00 177.000 GRAND TOTAL 67.760 16,222.100

210

DETAILS OF PERIODIC MAINTENANCE KIAMBATANISHO 5C(iv)

UNPAVED REGIONAL ROADS

Region Road Name Length (km) Estimate (Tshs mio) ARUSHA Monduri - Engaruka 7.00 106.100 Mto wa Mbu - Loliondo 30.00 450.000 T/Packers - Losinyai 5.00 76.000 Mbauda - Losinyai 5.50 83.700 Tengeru - Mererani 9.70 145.300 Longindo - Oldonyolengai Jct 0.30 4.200 Monduli Jnct - Lolkisale 2.00 30.200 Usa river - Oldonyosambu 15.40 231.600 Karatu - Kilimapunda 19.00 284.000 Sub-total 93.90 1,411.100

COAST Mbwewe - Lukigura bridge 2.00 30.000 Makurunge - Saadani 9.00 132.800 Mandera - Saadani 2.00 30.000

211

Chalinze - Magindu 9.00 103.000 Makofia - Mlandizi - 10.00 122.500 M Kiluvya - Mpuyani 4.00 38.000 Pugu - Vikumburu 35.00 355.000 Mkuranga - Kisiju 2.00 20.000

Kibiti - Utete - Nyamwage 15.00 300.000

TAMCO - Vikawa - Mapinga 15.00 200.000

Kilindoni - Utende 6.00 157.000

Kilindoni - Utende - Rasmkumbi 15.00 300.000

Sub-total 124.00 1,788.300

DAR ES SALAAM Mbweni jct - Mbweni - Bunju 4.00 100.000

Victoria - Magoe Mpiji - Bunju 5.00 120.000

Mbezi -M/Mawili - Kinyerezi 4.00 100.000

Goba - Wazo hill 5.00 170.000

212

Kunduchi - Ununio - Boko 3.00 90.000

Mbezi Mwisho - Samaki wabichi 5.00 200.000

Temboni - Matosa - Goba 3.00 90.000

Mvuti - Mbande 3.00 90.000

Mjimwema - Pembamnazi 6.00 130.000

Kibada - T/Songani - C/Boarder 5.00 150.000

Vijibweni Jnct - Kibada 3.00 90.000

Sub-total 46.00 1,330.000

DODOMA Dosidosi - Hogoro Jct 29.40 382.700

Olbolot - Dalai - Kolo 0.90 11.200 Ntyuka Jnct - Mvumi - Kikombo Jct 5.00 65.000 Machali - Ng'ambi - Kongwa Jct Hogoro Jct 13.00 169.000

213

Mpwapwa - Gulwe - Kibakwe - Chipogoro 12.00 156.000

Mbande - Kongwa - Suguta 13.80 179.800

Pandambili - Mpwapwa - Ng'ambi 15.00 195.000 Mkonze - Chidilo Jnct - Chipanga - Chali Igogo 6.00 47.400

Sub-total 95.10 1,206.100 IRINGA Iringa - Msembe 7.00 140.000 Iringa - Pawaga 4.00 80.000 Kitulo - Mfumbi 5.00 100.000 Kandamija - Kipingu 3.00 70.000 Iringa - Idete 7.00 140.000 Nyololo - Kibaoni 5.00 100.000

Kikondo - Makete - Njombe 15.00 300.000

Ndulamo - Nkenja - Kitulo 6.00 120.000

Njombe (Ramadhani) - Iyayi 7.00 149.000 Kibena - Lupembe 10.00 200.000 214

Mkiwu - Mavanga (Ruv Brd) 5.00 100.000

Igowole - Kasanga - Nyigo 5.00 100.000 Ilula - Kilolo 5.00 100.000 Ihawaga - Mgololo 10.00 200.000 Sub-total 94.00 1,899.000 Bugene - Nkwenda - Kaisho - KAGERA Murongo 22.00 286.000

Kakunyu - Kagera sugarJct 33.70 138.000

Kyaka - 2 - Kanazi - Kyetema 13.50 100.000

Muhutwe - Kamachumu - Muleba 5.00 93.000

Katoke - Nyamirembe Port 1.50 19.500

Rusumo Custom - Ngara 5.00 55.000 Murugarama - Rulenge - Nyakahura 6.70 87.200 Rulenge - Musurugamba - Kamubuga 17.00 210.000

215

Nyamwirorelwa - Uyovu 2.00 20.000

Nyabihanga - Kasambya -Minziro 5.00 65.000

Mwogo - Makonge - Ruhija 1.00 15.000

Kigusha - Ntoma - Kalembe 2.00 20.000

Maugulu - Mwogo 1.00 10.000

Kamukumbwa - Nagetageta 5.00 50.000

Rutenge - Rubale - Kishoju 6.00 80.000

Mukungo - Kabindi - Nyantakara 12.00 46.500

Sub-total 138.40 1,295.200

KIGOMA Simbo - Ilagala - Kalya 15.43 277.700

Nyaronga - Biharamulo Brd 12.21 219.800

Kakonko - Nyaronga - Ngara bdr 15.12 272.200

Mabamba - Kichananga - Kifura 15.00 300.000 216

Kasulu - Manyovu 2.00 50.000 Kalela - Munzeze - Janda 13.33 240.000 73.09 1,359.700 KILIMANJARO Kware - Lemira 3.00 79.600

Tarakea Jct - Tarakea Nayemi 8.00 200.000 Sanya juu - Kamwanga 13.00 393.890 TPC - Kikuletwa Bridge 7.00 191.500

Same - Kisiwani - Mkomazi 7.35 221.015 Sub-total 38.35 1,086.005 LINDI Tingi - Kipatimu 2.30 28.000 Liwale - Nachingwea 15.10 196.000

Nachingwea - Ruangwa Jct 37.00 426.000 Ngongo - Mandawa - Ruangwa Jct 13.60 28.600

Nachingwea - K/Rondo 26.00 207.000

Sub-total 94.00 885.600 MANYARA Kilimapunda - Kidarafa 40.00 450.000 217

Dareda - Dongobesh 12.00 156.000 Mogitu - Haydom 60.60 787.000 Mbuyu wa mjerumani - Mbulu 43.00 262.000 Mirerani - Landanai - 9.00 95.000 Ok t Cairo - Mererani 1.49 19.300 Kibaya - Kibereshi 18.00 169.000 Sub-total 184.09 1,938.300 MARA Kuruya - Utegi 10.00 130.000 Shirati - Kubiterere 15.00 180.000

Nyankanga - Rung'abure 15.00 180.000 Sirori simba - Majimoto 1.50 14.000 Musoma - Makojo 5.00 65.000

Manyamanyama - Nyambui 14.60 138.300 Nyamuswa - Kisorya 15.00 195.000 Sub-total 76.10 902.300

MBEYA Mbalizi - Shigamba - Isongole 23.00 298.800

Mbalizi - Makongolosi 38.00 493.600 218

Katumba - Lwangwa - Mbambo 4.70 60.800

Tukuyu - Mbambo - Ipinda 10.80 140.900

Kikusya - Ipinda - Mateme 17.50 227.300 Majombe (Madibira Jct) - Mbalali/Mufindi) 8.00 126.400

Kiwira - Isangati 11.60 150.400

Kilambo - Njugilo 2.10 89.000

Sub-total 115.70 1,587.200

MOROGORO Mziha - Magole 7.40 121.400

Sangasanga - Langali 9.40 157.400

Bigwa - Kisaki 14.30 241.600

Sub-total 31.10 520.400

MTWARA Lukuledi - Masasi - Newala 15.70 161.000

Newala - Mahuta 34.00 404.700 219

Madimba - Msingati 6.40 83.200

56.10 648.900 Bukongo - M.tunguru - Bulamba - MWANZA Bukonyo 13.00 193.000 Rugenzi - Bukongo - Bukondo - Masonga 18.00 252.000

Geita (Mugusu) - Port Nungwe 5.00 65.000

Magu - Kabila - Mahaha 2.00 26.000

Geita - Bukoli - Buyange 6.00 91.000 Mwanza - Airport (Kayenze Jct) - Nyanguge 2.50 30.200

Mwanangwa - Misasi - Salawe 22.00 356.400 Sub-total 68.50 1,013.600 RUKWA Kizitwe - Mkina 8.10 82.684 Sitalike - Kibaoni 6.60 67.752 Kibaoni - Mamba 6.80 68.902 Kaengesa - Mwimbi 5.40 55.122 220

Laela - Mwimbi - Kizombwe 4.20 42.263 Kibo - Mwese - Lugonesi 4.90 50.041 Lyazumbi - Kabwe 4.50 45.729 Nkundi - Kate - Namanyere 5.40 55.122

Mtimbwa - Ntalamila 5.40 55.122

Kawajense(Mpanda) - Ugalla 4.20 42.263

Sub-total 55.50 565.000

RUVUMA Mbambabay - Liuli - Lituhi 4.50 75.700

Tunduru - Nalasi/Chamba 2.00 48.600 Nangombo - Chiwindi 1.20 30.000 Azimio - Lukumbule 2.00 52.000

Mtwarapachani - Lingusenguse 3.80 91.000 Sub-total 13.50 297.300 SHINYANGA Buyange - Busoka 15.00 90.000 Nyikonga - Ushirombo 11.00 143.000

221

Maswa Niapanda - Lalago 11.00 66.000

Malya - Malampaka - Ikungu 5.00 65.000

Luguru - Kadoto - Malya 7.00 66.500

Sola Jnct - Sakasaka 15.00 195.000

Mwandete - Mwamanoni 12.00 157.000

Kabondo -Semu 10.00 130.000

Kanawa - Mihama 5.00 30.000

Mwamashele - Kalitu 5.00 47.500

Shinyanga - Bubiki 5.00 47.500 Nyandekwa Jnct - Nyandekwa - Butibu 5.00 47.500

Salawe - Old Shinyanga 16.50 211.000

Bariadi - Salama (Magu Boarder) 12.60 119.800

Bariadi - Kisesa (Meatu Boarder) 5.00 47.500 222

Kahama - Chambo 10.00 99.000 Kanawa Jnct - Manonga River (Tbr Brd) 15.00 110.000

Sub-total 165.10 1,672.300

SINGIDA Sekenke - Shelui 5.00 75.500

Misigiri - Kiomboi 3.00 39.000 Kizaga - Sepuka - Mlandala - Mgungira 10.00 103.900

Ulemo - Gumanga - Sibiti 5.00 61.500 Iguguno Shamba - Nduguti - Gumanga 5.00 84.000

Ikungi - Londoni - Kilimatinde 7.00 107.500

Heka - Sasilo - Iluma 2.00 30.000

Manyoni - Heka - Ikasi 18.00 293.000

Njuki - Ilongero - Ngamu 5.00 82.200

223

Sabasaba (Singida) - Sepuka 4.00 60.000

Kidarafa - Nkungi 5.00 75.500

Kititimo - Kinyamshindo 3.00 45.000

Sub-total 72.00 1,057.100

TABORA Bukene - Itobo 5.00 47.500

Kahama Brd - Nzega 37.00 481.000

42.00 528.500

TANGA Malindi - Mtae 2.80 56.600

Magamba - Mlola 8.20 163.000

Mlingano Jct - Kiomoni Jct 15.00 400.000

Tanga - Pangani - Buyuni 7.90 158.000

Mkalamo Jct - Mkalamo 17.20 344.600

Bombani - Kimbe 4.80 96.000 224

Manyara Brd - Kibershi - Handeni 3.30 65.500

Umba - Mkomazi Jct 7.60 151.000

Silabi - Dindira 1.20 24.000

Vibaoni - Mziha 1.20 24.000

Kwarugulu - Kibereshi 14.20 284.000 Mbaramo - Maramba - Kwasongoro 7.80 156.000

Sub-total 91.20 1,922.700

GRAND TOTAL 1,767.73 24,914.605

225

KIAMBATANISHO 5D(i)

SPOT IMPROVEMENT DETAILS - TRUNK ROADS

REGIO N PAVED UNPAVED Targ

Target et Amount Amount Road Name Length Road Name Leng (Tshs (Tshs (Km) th mio.) mio.) (Km) Coast Kongowe - Kibiti (T7) 1.00 50.541 Sub total 1.00 50.541 - - DSM New Bagamoyo Road 1.00 150.000 Sub total 1.00 150.000 - - Dodom Mtera - Dodoma - Bereko 1.97 226

a 32.800

Sub total - - 1.97 32.800 Kigoma Kigoma - Kanyani 1.54 19.700 Rukwa/Kigoma bdr - Kanyani - Kasulu 4.31 63.170

Kasulu - Kibondo 1.30 17.000 Tabora brd - Nkwaza - Kibaoni - Kidawe 0.75 11.500 Sub total - - 7.90 111.370 Lindi Mtama - Mkungu 1.69 10.980

Lindi - Ngongo 1.68 48.040 Tingi- Nangurukuru 0.56 5.010 Sub total 3.93 64.030 - - Mbeya Mbeya - Rungwa (Singida 0.20 227

Border) 2.248

Sub total - - 0.20 2.248 Mtwara Mtwara-Mtegu & Mangaka - Mkungu - Masasi 2.50 386.650 Lumesule(Ruvuma brd) 1.35 22.000 Sub total 2.50 386.650 1.35 22.000 Rukwa Matai - Kasesya 1.00 17.000

Mpanda - Tabora brd 0.50 8.500

Mpanda - Kigoma brd 1.00 17.000 Sub total - - 2.50 42.500 Ruvum a Songea - Mitomoni 10.00 100.000 Mbinga - Mbambay (Ambrose Escarp.) 8.00 120.000 Sub total - - 18.00 220.000 Shinya nga - - Bariadi - Maswa 0.60 9.00 228

Kolandoto - Lalago 0.20 2.00

Lalago - Mwanhuzi 0.40 6.00 Sub total - - 1.20 17.00 Singida Manyoni - Itigi - Chaya 6.00 90.500

Rungwa - Itigi - Mkiwa 5.40 80.929 Sub total - - 11.40 171.429 Tabora Rungwa (Mbeya Brd) - Ipole 0.30 3.680

Ipole - Tabora (Isike NBC) 1.60 23.770

Tabora (Isike NBC) - Nzega 3.80 59.910

Chaya - Kigwa - Tabora 1.10 15.750

Tabora - Urambo 1.10 16.110

Urambo - Kaliua - Chagu 11.6 179.03

229

Sub total - - 19.50 298.250

64.02 GRAND TOTAL 8.43 651.221 0 917.597

230

231

KIAMBATANISHO 5D(ii) SPOT IMPROVEMENT DETAILS - REGIONAL ROADS

PAVED UNPAVED REGIO Target Amount Target Amount N Road Name Road Name Length (Tshs Length (Tshs (Km) mio.) (Km) mio.) Coast Bungu - Nyamisati 2.00 30.000 Makurunge - Saadan 3.00 60.000 232

Mbwewe - Lukigura Bridge 1.50 62.372

Chalinze - Magindu 0.20 2.300

Pugu - Vikumburu 3.00 45.000 Sub Total 9.70 199.672 DSM Ukonga Jct - G/mboto - Kibamba Shule - Chanika 1.500 150.000 Magoe Mpiji 0.50 17.000 Makabe Jct. - Mbezi Kawe - Lugalo 0.500 70.000 Msakuzi 1.00 35.000 Moroko - Mlalakuwa - Victoria - Magoe Kawe jct - Mpiji - Bunju Sports Africana 1.000 150.000 Motel 1.00 20.000

Kibamba- Kwembe 1.80 45.000 Mbezi-M/Mawili- Kinyerezi 2.50 20.000 Kunduchi - Ununio - Boko 1.00 30.000

233

Mbezi Mwisho - S/Wabichi 1.20 36.000

Mvuti - Mbande 1.50 22.500 Kivukoni - Tungi- Vijibweni 1.00 25.000

Dege - Gomvu 1.51 25.000 Kibada - T/Songani- C/Boarder 1.03 22.000 Buyuni - Tundwisongani 3.00 30.000

Chekeni - Kimbiji 1.50 20.000 Vijibweni jct - Kibada 1.00 20.000 Pugu - Kajiungeni A -KILTEX 0.60 9.000

Kibo - Msewe 1.00 20.000 Sub Total 3.000 370.000 21.14 396.500 Dodom Pandambili - a Ng'ambi 0.75 14.250 234

Chimwaga Jct - Chimwaga - Ihumwa 0.25 3.750 Ntyuka - Mvumi - Kikombo 0.39 5.600 Mbande - Kongwa - Suguta 0.80 15.500 Machali - Ng'ambi - Kongwa 1.42 26.650 Mpwapwa - Gulwe - Kibakwe 1.50 25.250 Chamwino Ikulu - Chamwino 2.50 47.850 Mkoze - ChidiloJct - Chipanga 0.21 3.150 Hogoro Jct - Dosidosi 0.05 0.750 Kibaigwa - Ngomai - lugine 0.85 13.500

Olbolot - Kolo 0.50 7.500 Mpwapwa - Pwaga - Lumuma 0.05 0.750

235

Zamahero - Kinyamshindo 1.59 27.130 Sub Total 10.86 191.630 Kagera Kyaka - 1 - Rutenge - Rubale - Kanazi - Kyetema 2.00 10.000 Kishoji 35.00 149.250 Kanazi - Mukungo - Kabindi - Kanyinya 1.00 12.600 Nyantakara 12.00 50.000 Magoti - Makonge- Kanyangereko 1.00 17.400 Sub Total 4.00 40.000 47.00 199.250 Kigoma Kakonko - Nyaronga - Ngara brd 2.30 31.500 Simbo - Ilagala - Kalya 2.02 26.450 Sub Total 4.32 57.950 Kilimanj Gunge Bridge - aro Hedaru 2.00 51.250

Kifaru - Butu - 2.00 50.000 236

Ng'ombe

Mwembe - Vuchama 11.00 258.000

Bangalala - Ndolwa 1.50 35.500 Sub Total 16.50 394.750 Lindi K/Masoko - Liwale 2.82 43.030 Liwale - Newala (Liwale - Kiangara) 16.24 358.950 Liwale - Newala (Kiangara - Luponda) 27.19 228.500 Sub Total 46.25 630.480 Manyar Kilimapunda - a Kidarafa 2.04 24.980

Losinyai - Njoro 11.63 155.450 Mbuyu wa Mjerumani - Mbulu 0.80 8.550

237

Cairo - Mererani 0.05 0.500

Lolksale - Sukuro 0.20 3.250 Dareda - Dongobesh 2.85 37.200

Mogitu - Haydom 3.17 39.250 Babati - Kuta - Mburu 1.40 24.250

Singe - Naberera 1.57 17.380

Kimotorok - Ngopito 5.58 62.030 Kijungu - Sunya - Dongo 4.13 72.450

Orkesumet - Gunge 2.70 45.250 KIA - Landanai - Orkesumet 3.66 61.100 Kibaya - Kiberashi 0.48 4.800 Sub Total 40.26 556.440 Mara Nyamuswa - Bunda 3.00 - Kisorya 50.000 238

Kuruya - Utegi 0.50 3.370 Sub Total 3.50 53.370 Mbeya Mbalizi - Makongolosi 3.80 50.500 Igawa - Mbarali 0.05 0.500 Kikusya - Matema 0.90 11.000 Katumba - Mbambo 2.15 25.500 Tukuyu - Mbambo - Ipinda 1.25 15.000

Mbalizi - Isongole 2.30 25.500 Majombe - Mbarali/Mufindi brd 0.10 1.500 Igurusi - Utengule 0.70 7.000 Saza - Kapalala 3.37 43.950 Mahenje - Hansamba - Vyawa 0.20 2.000 Katumba - Lutengano - Kyimbila 0.20 3.500 Bujesi - Itete 0.10 1.230

239

Sub Total 15.12 187.180 Morogo Mvomero - Ndole - ro Kibati - Lusanga 5.80 115.228 Bigwa - Kisaki 2.00 38.546 Msomvinzi - Mikese 2.00 33.541 Ifakara - Taweta 19.20 384.943 Mahenge - Ilonga 3.00 59.190 Sub Total 31.80 631.448 Mtwara Lukuledi - Masasi Lukuledi - Masasi - - Newala 1.80 21.000 Newala 7.55 115.750 Mbuyuni - Makong'onda 1.05 16.000 Mkwiti - Kitangari 12.30 244.500 Matipa - Litehu 10.25 181.750 Mpapura - Mikao 4.20 83.000 Msijute - Mnina 2.80 52.000 Newala - Magamba 3.38 50.700 Mahuta jct - 1.45 27.000 Nik Madimba - 1.25 19.750 N ik 240

Madimba - Msimbati 1.40 21.000 Likwachu - Mwema 1.20 24.000 Sub Total 1.80 21.00 46.83 835.450 Mwanza Rugezi - Bukongo - Masonga 0.44 7.850 Geita - Bukoli - Buyange 0.35 6.750 Busisi - Nyang'holongo 0.25 4.130 Nyashimo - Ngasamo 2.00 40.000

Magu - Mahaha 0.20 3.000 Fulo - Nyambiti 0.05 0.750 Bukwimba - Kabila 0.70 17.500 Ngudu - Malya 0.07 1.400 Mwanangwa - Salawe 0.70 11.900 Sub Total 4.76 93.280 Rukwa Kagwira - Karema 1.00 17.000 Kibaoni - Mamba 1.00 17.000 241

Ilomba - Kaoza 1.00 17.000 Laela - Mwimbi - Kozombwe 1.00 17.000 Kibo - Msewe (R753) 0.50 8.500 Nkundi - Kate - Namanyere 1.00 17.000 Msishindwe - Mambwekenya 1.00 17.000 Mtimbwa - Ntalamla 0.50 8.500 Lyazumbi - Kabwe 1.00 17.000 Kizwite - Mkima 1.00 17.000 Sub Total 9.00 153.000 Ruvum Mbamba Bay - Liuli a - Lituhi (R821) 7.60 128.270 Namtumbu - Likuyu (R830) 1.09 25.000

Luhuhu Ferry Ramp 1.00 150.000 Nangombo - Chiwindi (R837) 1.39 25.000

242

Sub Total 11.08 328.270 Shinyan ga Buyange - Busoka 0.55 8.250 Luguru - Kadoto - Malya 1.75 17.500

Sola jct - Sakasaka 1.35 14.250 Mwandete - Mwamanoni 1.16 13.100

Kishapu - Buzinza 1.15 13.000

Kanawa - Mihama 0.30 3.000 Mwamashele - Kalitu 0.90 9.000

Shinyanga - Bubiki 0.60 9.500 Salawe - Oild Shinyanga 0.90 13.500 Nyandekwa jct - Butibu 1.46 16.100

Bariadi - Kisesa 0.05 0.500

243

Kanawa Jct - Manonga River 0.15 2.250 Masabi - Mega (R360) 0.40 4.000 Sub Total 10.72 123.950 Singida Kidarafa - Nkungi 3.00 43.987

Sekenke - Shelui 3.00 43.987 Kizaga - Sepuka - Mgungira 5.00 42.278

Ulemo - Sibiti 0.10 0.750 Iguguno - Nduguti - Gumanga 0.30 4.500 Ilongero - Mtinko - Ndunguti 4.00 60.000 Ikungi - Londoni - Kilimatinde 5.00 75.000 Heka - Sasilo - Iluma 0.80 12.000 Manyoni - Heka - Ikasi 10.00 150.500 244

Kinyamshindo - Kititimo 0.10 0.500

Sabasaba - Sepuka 0.10 1.500 Sub Total 31.40 435.002 Tabora Tabora - Ulyankulu 3.30 49.050

Mambali - Bukumbi 1.30 19.950

Tabora - Mambali 3.30 42.510

Bukene - Itobo 0.20 9.670

Igurubi - Iborogero 4.00 59.920

Ziba - Choma 2.00 30.750

Puge - Ziba 5.30 87.200

2.60 40.650 Sub Total 22.00 339.700 Tanga Vuga - Vuga - 0.60 12.750 245

Mission

Tanga - Pangani - Buyuni 3.30 66.750

Mheza - Kwamkoro 0.20 3.000

Silabu - Dindira 0.10 2.250 Mbaramo - Kwasongoro 0.80 15.000 Sub Total 5.00 99.750

GRAND TOTAL 8.800 431.000 387.24 5,907.072

246

KIAMBATANISHO 5D(ii) SPOT IMPROVEMENT DETAILS - REGIONAL ROADS

PAVED UNPAVED REGIO Target Amount Target Amount N Road Name Road Name Lengt (Tshs Length (Tshs h (Km) mio.) (Km) mio.) Coast Bungu - Nyamisati 2.00 30.000 Makurunge - Saadan 3.00 60.000 Mbwewe - Lukigura Bridge 1.50 62.372 Chalinze - Magindu 0.20 2.300 247

Pugu - Vikumburu 3.00 45.000 Sub Total 9.70 199.672 DSM Ukonga Jct - Kibamba Shule - G/mboto - Chanika 1.500 150.000 Magoe Mpiji 0.50 17.000 Makabe Jct. - Mbezi Kawe - Lugalo 0.500 70.000 Msakuzi 1.00 35.000 Victoria - Magoe Moroko - Mlalakuwa Mpiji - Bunju Sports - Kawe jct - Africana 1.000 150.000 Motel 1.00 20.000 Kibamba- Kwembe 1.80 45.000 Mbezi-M/Mawili- 2.50 20.000 Ki i Kunduchi - Ununio - 1.00 30.000 MbeziBk Mwisho - S/Wabichi 1.20 36.000 Mvuti - Mbande 1.50 22.500 Kivukoni - Tungi- 1.00 25.000 Vijib i Dege - Gomvu 1.51 25.000 Kibada - T/Songani- C/Boarder 1.03 22.000 Buyuni - 3.00 30.000 Tdi i 248

Chekeni - Kimbiji 1.50 20.000 Vijibweni jct - Kibada 1.00 20.000 Pugu - Kajiungeni A -KILTEX 0.60 9.000

Kibo - Msewe 1.00 20.000 Sub Total 3.000 370.000 21.14 396.500 Dodom Pandambili - a Ng'ambi 0.75 14.250 Chimwaga Jct - Chimwaga - Ihumwa 0.25 3.750 Ntyuka - Mvumi - Kikombo 0.39 5.600 Mbande - Kongwa - Suguta 0.80 15.500 Machali - Ng'ambi - Kongwa 1.42 26.650 Mpwapwa - Gulwe - Kibakwe 1.50 25.250 Chamwino Ikulu - Chamwino 2.50 47.850

249

Mkoze - ChidiloJct - Chipanga 0.21 3.150 Hogoro Jct - Dosidosi 0.05 0.750 Kibaigwa - Ngomai - lugine 0.85 13.500

Olbolot - Kolo 0.50 7.500 Mpwapwa - Pwaga - Lumuma 0.05 0.750 Zamahero - Kinyamshindo 1.59 27.130 Sub Total 10.86 191.630 Kagera Kyaka - 1 - Kanazi - Rutenge - Rubale - Kyetema 2.00 10.000 Kishoji 35.00 149.250 Mukungo - Kabindi - Kanazi - Kanyinya 1.00 12.600 Nyantakara 12.00 50.000 Magoti - Makonge- Kanyangereko 1.00 17.400 Sub Total 4.00 40.000 47.00 199.250 Kigoma Kakonko - Nyaronga 2.30 31.500 250

- Ngara brd

Simbo - Ilagala - Kalya 2.02 26.450 Sub Total 4.32 57.950 Kiliman Gunge Bridge - jaro Hedaru 2.00 51.250 Kifaru - Butu - Ng'ombe 2.00 50.000

Mwembe - Vuchama 11.00 258.000

Bangalala - Ndolwa 1.50 35.500 Sub Total 16.50 394.750 Lindi K/Masoko - Liwale 2.82 43.030 Liwale - Newala (Liwale - Kiangara) 16.24 358.950 Liwale - Newala (Kiangara - Luponda) 27.19 228.500

251

Sub Total 46.25 630.480 Manyar Kilimapunda - a Kidarafa 2.04 24.980

Losinyai - Njoro 11.63 155.450 Mbuyu wa Mjerumani - Mbulu 0.80 8.550

Cairo - Mererani 0.05 0.500

Lolksale - Sukuro 0.20 3.250

Dareda - Dongobesh 2.85 37.200

Mogitu - Haydom 3.17 39.250 Babati - Kuta - Mburu 1.40 24.250

Singe - Naberera 1.57 17.380

Kimotorok - Ngopito 5.58 62.030 Kijungu - Sunya - Dongo 4.13 72.450

252

Orkesumet - Gunge 2.70 45.250 KIA - Landanai - Orkesumet 3.66 61.100

Kibaya - Kiberashi 0.48 4.800 Sub Total 40.26 556.440 Mara Nyamuswa - Bunda - 3.00 Kisorya 50.000 0.50 Kuruya - Utegi 3.370 Sub Total 3.50 53.370 Mbeya Mbalizi - Makongolosi 3.80 50.500

Igawa - Mbarali 0.05 0.500

Kikusya - Matema 0.90 11.000

Katumba - Mbambo 2.15 25.500 Tukuyu - Mbambo - Ipinda 1.25 15.000

253

Mbalizi - Isongole 2.30 25.500 Majombe - Mbarali/Mufindi brd 0.10 1.500

Igurusi - Utengule 0.70 7.000

Saza - Kapalala 3.37 43.950 Mahenje - Hansamba - Vyawa 0.20 2.000 Katumba - Lutengano - Kyimbila 0.20 3.500

Bujesi - Itete 0.10 1.230 Sub Total 15.12 187.180 Morogo Mvomero - Ndole - ro Kibati - Lusanga 5.80 115.228

Bigwa - Kisaki 2.00 38.546

Msomvinzi - Mikese 2.00 33.541

Ifakara - Taweta 19.20 384.943 254

Mahenge - Ilonga 3.00 59.190 Sub Total 31.80 631.448 Mtwara Lukuledi - Masasi - Lukuledi - Masasi - Newala 1.80 21.000 Newala 7.55 115.750 Mbuyuni - Makong'onda 1.05 16.000

Mkwiti - Kitangari 12.30 244.500

Matipa - Litehu 10.25 181.750

Mpapura - Mikao 4.20 83.000

Msijute - Mnina 2.80 52.000

Newala - Magamba 3.38 50.700 Mahuta jct - Namikupa 1.45 27.000 Madimba - Namikupa 1.25 19.750

Madimba - Msimbati 1.40 21.000

255

Likwachu - Mwema 1.20 24.000 Sub Total 1.80 21.00 46.83 835.450 Mwanza Rugezi - Bukongo - Masonga 0.44 7.850 Geita - Bukoli - Buyange 0.35 6.750 Busisi - Nyang'holongo 0.25 4.130 Nyashimo - Ngasamo 2.00 40.000

Magu - Mahaha 0.20 3.000

Fulo - Nyambiti 0.05 0.750

Bukwimba - Kabila 0.70 17.500

Ngudu - Malya 0.07 1.400 Mwanangwa - Salawe 0.70 11.900 Sub Total 4.76 93.280

256

Rukwa Kagwira - Karema 1.00 17.000

Kibaoni - Mamba 1.00 17.000

Ilomba - Kaoza 1.00 17.000 Laela - Mwimbi - Kozombwe 1.00 17.000 Kibo - Msewe (R753) 0.50 8.500 Nkundi - Kate - Namanyere 1.00 17.000 Msishindwe - Mambwekenya 1.00 17.000

Mtimbwa - Ntalamla 0.50 8.500

Lyazumbi - Kabwe 1.00 17.000

Kizwite - Mkima 1.00 17.000 Sub Total 9.00 153.000 Ruvum Mbamba Bay - Liuli - a Lituhi (R821) 7.60 128.270

257

Namtumbu - Likuyu (R830) 1.09 25.000

Luhuhu Ferry Ramp 1.00 150.000 Nangombo - Chiwindi (R837) 1.39 25.000 Sub Total 11.08 328.270 Shinya nga Buyange - Busoka 0.55 8.250 Luguru - Kadoto - Malya 1.75 17.500

Sola jct - Sakasaka 1.35 14.250 Mwandete - Mwamanoni 1.16 13.100

Kishapu - Buzinza 1.15 13.000

Kanawa - Mihama 0.30 3.000

Mwamashele - Kalitu 0.90 9.000

Shinyanga - Bubiki 0.60 9.500

258

Salawe - Oild Shinyanga 0.90 13.500 Nyandekwa jct - Butibu 1.46 16.100

Bariadi - Kisesa 0.05 0.500 Kanawa Jct - Manonga River 0.15 2.250 Masabi - Mega (R360) 0.40 4.000 Sub Total 10.72 123.950 Singida Kidarafa - Nkungi 3.00 43.987

Sekenke - Shelui 3.00 43.987 Kizaga - Sepuka - Mgungira 5.00 42.278

Ulemo - Sibiti 0.10 0.750 Iguguno - Nduguti - Gumanga 0.30 4.500 Ilongero - Mtinko - Ndunguti 4.00 60.000 259

Ikungi - Londoni - Kilimatinde 5.00 75.000

Heka - Sasilo - Iluma 0.80 12.000 Manyoni - Heka - Ikasi 10.00 150.500 Kinyamshindo - Kititimo 0.10 0.500

Sabasaba - Sepuka 0.10 1.500 Sub Total 31.40 435.002 Tabora Tabora - Ulyankulu 3.30 49.050

Mambali - Bukumbi 1.30 19.950

Tabora - Mambali 3.30 42.510

Bukene - Itobo 0.20 9.670

Igurubi - Iborogero 4.00 59.920

Ziba - Choma 2.00 30.750

260

Puge - Ziba 5.30 87.200

2.60 40.650 Sub Total 22.00 339.700 Tanga Vuga - Vuga - Mission 0.60 12.750 Tanga - Pangani - Buyuni 3.30 66.750

Mheza - Kwamkoro 0.20 3.000

Silabu - Dindira 0.10 2.250 Mbaramo - Kwasongoro 0.80 15.000 Sub Total 5.00 99.750

GRAND TOTAL 8.800 431.000 387.24 5,907.072

261

KIAMBATANISHO 5E(i) BRIDGE PREVENTIVE MAINTENANCE: Trunk and Regional Roads

FY 2010/11 Estimated Expenditure Tshs mio. TOTAL ESTIMATED NUMBER BRIDGES TO GET PREVENTIVE AMOUNT (TShs.) OF MTCE TOTAL (ROAD FUND) S/N REGION BRIDGES AMOUNT (Tshs mio.) TR TR RR TOTAL TR RR

1 Arusha 70 33 103 26.512 59.078 85.590

2 Coast 13 30 43 14.663 21.522 36.185

262

3 DSM 15 37 52 28.125 18.500 46.625

4 Dodoma 89 156 245 145.437 210.894 356.331

5 Iringa 99 59 158 56.400 77.400 133.800

6 Kagera 159 49 208 25.840 7.190 33.030

7 Kigoma 38 19 57 35.316 32.412 67.728

8 K’manjaro 30 40 70 90.000 120.000 210.000

9 Lindi 40 30 70 150.000 100.000 250.000

10 Manyara 3 30 33 4.200 33.600 37.800

263

11 Mara 120 134 254 46.475 203.470 249.945

12 Mbeya 202 190 392 102.300 52.250 154.550

13 Morogoro 75 91 166 75.000 91.000 166.000

14 Mtwara 50 9 59 50.000 30.000 80.000

15 Mwanza 40 14 54 190.237 92.033 282.270

16 Rukwa 26 72 98 20.800 56.000 76.800

17 Ruvuma 30 49 79 33.460 108.860 142.320

18 Shinyanga 10 23 33 97.346 252.679 350.025

264

19 Singida 7 13 20 16.500 27.300 43.800

20 Tabora 40 40 80 44.000 24.000 68.000

21 Tanga 12 14 26 55.770 66.000 121.770

1,308.38 1,684.18 TOTAL 1,168 1,132 2,300 2,992.569 1 8

265

KIAMBATANISHO 5E(ii) TRUNK ROADS BRIDGES: Major Repairs FY 2010/11 Major Repairs of Bridges & Drainage Structures Estimated Expenditure in Tshs mio.

FY 2010/11 Total Total RF No. of Roads Foreig for Region Name of Bridge Estimate bridges Fund n Region

Arusha TCA Junction - Minjingu 1 31.460 - 31.460

Makuyuni Ngorongoro gate 1 100.000 - 100.000

266

KIA Jct - TCA Jjct 1 200.000 - 200.000

Matala - Njia Panda 1 100.000 - 100.000 431.460

DSM Morogoro road 1 40.000 - 40.000 Kilwa road 1 40.000 40.000

New Bagamoyo road 4 150.000 - 150.000 230.000

Dodoma Mtera - Dodoma - Bereko 1 42.800 - 42.800

Gairo - Dodoma - Kintinku 1 287.435 - 287.435 330.235

Iringa TANZAM Highway 4 57.000 - 57.000

Itoni - Ludewa - Manda 1 45.000 - 45.000 Iringa - Dodoma border 1 20.000 20.000 Mafinga - Mgololo 1 15.000 15.000 137.000 Mutukula - Bukoba - Kagoma - Kagera Kalebezo 1 229.790 - 229.790 267

Kobero - Ngara - Nyakasanza 1 114.900 - 114.900 344.690

Kigoma Kanyani - Kidahwe (Jordan) 1 40.848 - 40.848

Kasulu - Kibondo (Ngalaganza) 1 60.000 - 60.000

Kasulu - Kibondo (Kanyanga) 1 114.000 - 114.000 214.848 Kilimanj Same - Himo Jct aro 1 300.000 - 300.000 300.000

Mara Musoma - Nabi Hill Gate 1 88.000 - 88.000

Sirari Jct - Sirari (Kirumi ) 1 50.000 - 50.000 138.000

Mbeya TANZAM Highway 1 100.000 - 100.000 100.000 Morogor Tanzam (Mgoda II & V) o 2 53.200 - 53.200

Mikumi-Mahenge/Londo) 7 90.404 - 90.404 143.604 Magomeni - Msijute (Magomeni Mtwara I) 1 59.259 - 59.259 59.259

268

Rukwa Matai - Kasesya 1 45.000 - 45.000 45.000

Ruvuma Songea - Tunduru - Lumesule 4 40.049 - 40.049

Songea - Mbinga - Mbambabay 2 58.444 - 58.444

Songea - Mtomoni 1 35.288 - 35.288 133.781

Singida Rungwa - Itigi - Mkiwa 1 40.000 - 40.000 40.000

Tabora Tabora - Ipole (Chabutwa) 1 65.155 - 65.155

Ipole - Rungwa (Kapumpa) 1 57.167 - 57.167

Nzega - Tabora/Singida brd 4 42.600 - 42.600 164.922

Total (Trunk Roads Bridges) 53 2,812.799 - 2,812.799 2,812.799

269

REGIONAL ROADS BRIDGES: Major Repairs FY 2010/11 Major Repairs of Bridges & Drainage Structures KIAMBATANISHO 5E(iii) Estimated Expenditure in Tshs mio. FY 2010/11 Total RF No. of Total Region Name of Bridge for bridges Roads Foreig Estimate Fund n region

Arusha Usa river - Oldonyo Sambu 1 100.000 - 100.000

Monduli - Engaruka JCT 1 100.000 - 100.000 200.000

Coast Pugu Vikumburu 1 125.000 - 125.000 125.000 270

Mbezi mwisho - Tanki bovu DSM (Lobokwe) 1 120.000 - 120.000

Kibamba - Mpiji (Kibesa) 1 120.000 - 120.000

Victoria - Mpiji (Magoe) 1 500.000 - 500.000 Chanika - Mbande (Kitonga

B/Culvert) 1 120.000 - 120.000 860.000

Dodoma Kolo-Dalai-Olbolot 2 67.182 - 67.182 Zamahero - Kwamtoro -

Kinyamshindo 1 45.264 - 45.264 Mpwapwa - Makutano Jct -

Pwaga Jct - Ddm/Mor 1 90.528 - 90.528 Manchali - Ng'ambi - Kongwa

jct - Hogoro 1 61.019 - 61.019

Pandambili-Mpwapwa-Ngambi 1 45.264 - 45.264 309.257

Iringa Kitulo - Matamba - Mfumbi 1 20.000 - 20.000

Mkiu - Lugarawa - Mavanga 1 25.000 - 25.000 45.000

271

Muhutwe - Kamachumu - Kagera Muleba 1 120.000 - 120.000

Rutenge - Rubale - Kishoju 1 250.000 - 250.000 370.000 Simbo - Ilagala - Kalya Kigoma (KasigoIII ) 1 30.000 - 30.000 Simbo - Ilagala - Kalya

(Kangwena II ) 1 42.665 - 42.665 Kalela - Mzeze - Janda ( Mtaha

) 1 18.440 18.440 Simbo - Ilagala - Kalya

(Kangwena III ) 1 26.512 26.512 Simbo - Ilagala - Kalya

(Kaswegenya) 1 26.512 26.512 Simbo - Ilagala - Kalya (

Mungwe Mkuu ) 1 160.864 160.864 Simbo - Ilagala - Kalya (

Bahiganyi ) 1 138.000 138.000 442.993 Kilimanj Same - Kisiwani - Mkomazi aro 1 450.000 - 450.000

Mwembe - Ndungu 1 250.000 - 250.000 700.000

272

Nangurukuru - Liwale ( Njinjo & Kingwea) 2 199.040 - 199.040

Tingi - Kipatimu (Mbuyuni ) Lindi 1 90.040 - 90.040

Kiranjeranje - Namichiga (Ngaluchete & Kikundi) 3 413.420 - 413.420 702.500

Manyara Losinyai - Njoro (Ruketo) 1 270.000 - 270.000 Dareda - Dongobesh

(Bashinet) 1 100.075 - 100.075 370.075

Mara Tarime - Nata (') 1 150.000 - 150.000

Murangi - Bugwena (Bugwema) 1 71.000 - 71.000

Balili - Machimwelu (Kihumbi) 1 106.000 - 106.000 327.000

Mbeya Isongole II - Isoko 1 300.000 - 300.000

Kyimo - Ibungu 1 50.000 - 50.000 350.000 Morogor Ifakara - Taweta o 2 148.454 - 148.454 273

Magole - Mziha 3 35.072 - 35.072

Bigwa - Kisaki 5 206.340 - 206.340 389.866

Mtwara Lukuledi - Masasi (Lukuledi III) 1 87.650 - 87.650 Mbuyuni - Makong'onda -

Newala (Mbuyuni II) 1 42.222 - 42.222

Mpapura - Mikao (Chekeleni III) 1 63.372 - 63.372 193.244

Mwanza Buyogo- 1 1 40.882 - 40.882

Bugorola 1 43.531 - 43.531

Nyamazugo bridge 1 158.730 - 158.730 243.144 Ilembe - Kaoze (Nyombe Rukwa vented drift) 1 80.000 - 80.000

Mtowisa - Ilembe ( drifts) 4 180.000 - 180.000

Muze - Mtowisa (drifts) 2 90.000 - 90.000

274

Kibaoni - Mamba (Kanidi brdg.) 1 65.734 - 65.734

Mamba - Muze (Kapilula drift) 1 60.000 - 60.000 Kibo - Mwese ( Katuma A

brdg.) 1 85.000 - 85.000 560.734

Ruvuma Kigonsera - Mbaha 1 10.000 - 10.000

Kalulu bridge 1 200.000 - 200.000

Kitai - Lituhi 2 40.000 - 40.000 250.000 Shinyan Kadoto - Luguru (Kadoto) ga 1 180.000 - 180.000

Kanawa Jct - Manonga 1 780.000 - 780.000 960.000

Singida Sekenke - Shelui 1 150.000 - 150.000

Ikungi - Londoni - Kilimatinde 1 50.000 - 50.000 200.000

Tabora Puge - Ziba (Nkinga c ) 1 70.115 - 70.115

275

Puge - Ziba ( Kalemela ) 1 69.540 69.540 Puge - Ziba (Ulaya) 1 51.840 51.840 Ziba - Choma ( Makwengi ) 1 30.240 30.240 221.735 Umba - Mkomazi (Mkundi - Tanga Mbalu) 1 303.000 - 303.000 Kwaluguru - Kibirashi

(Sangasa) 1 278.740 - 278.740 581.740 Total (Regional Roads Bridges) 79.00 8,402.288 - 8,402.288 8,402.288

TRUNK & REGIONAL ROADS BRIDGES: Major repairs FY 2010/11 Roads Target Fund Foreign Total 132.00 11,215.086 - 11,215.086

276

KIAMBATANISHO 5F FINANCIAL REQUIREMENT FOR FY 2010/2011 - PMMR PROJECT

S/N PROJECT PACKAGES FUNDS REQUIRED Tshs mio.

Initial

Rehabilitation Maintenance Emergency Total

1 MWANZA REGION

1.1 Package 1 650.530 100.000 750.530

1.2 Package 2 510.000 100.000 610.000

1.3 Price adjustment for Package 1&2 350.000 80.000 430.000

277

Consultancy Package 1& 2 1.4 (Supervision) 408.000

2 RUKWA REGION

2.1 Package 3A 758.800 200.000 958.800

2.2 Package 3B 355.200 200.00 555.200 Price adjustment for Package 3A 2.3 & 3B

Consultancy Package 3A & 3B

2.4 (Supervision) 448.000

3 TANGA REGION

3.1 Package 4 3,380.000 614.556 200.000 4,194.56

3.2 Package 5 778.700 368.310 136.400 1,283.410

278

Price adjustment for Package 4 & 3.3 5 1,247.610 294.8598 100.920 1,643.390

Consultancy Package 4 & 5 3.4 (Supervision) 960.000

PMMR FACILITATOR & 4 TRAINING 890.000

GRAND TOTALS 13,131.886

279