1 BUNGE LA TANZANIA ___MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA TANO Kikao Cha Tisa – Tarehe 10 Novemba, 2016

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

1 BUNGE LA TANZANIA ___MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA TANO Kikao Cha Tisa – Tarehe 10 Novemba, 2016 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA _____________ MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA TANO Kikao cha Tisa – Tarehe 10 Novemba, 2016 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Tunaendelea na Mkutano wa Tano, Kikao cha Tisa, kama mlivyoona Waheshimiwa Wabunge Order Paper ilivyo, kile kipindi maarufu hatutakuwa nacho kwa udhuru maalum wa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Katibu! NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH- KATIBU MEZANI: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI ,VIJANA, AJIRA NA WALEMAVU: Taarifa ya Hali ya Dawa za Kulevya nchini ya mwaka 2015. MHE. ANDREW J. CHENGE - MWENYEKITI WA KAMATI YA BUNGE YA SHERIA NDOGO: Taarifa ya Kamati ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo. 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH - KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU Na. 94 Kuipanua Hospitali ya Wilaya ya Lushoto MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Wilaya ya Lushoto ina hospitali moja ya Wilaya ndani ya Halmashauri mbili na Majimbo matatu, hospitali hii inategemewa na watu zaidi ya 500,000. Je, ni lini Serikali itaifanyia upanuzi hospitali hiyo hasa wodi ya akina mama wajawazito? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Omar Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto imepanga kufanya upanuzi wa miundombinu ya Hospitali ya Wilaya katika mwaka wa fedha 2016/2017 ambapo zimetengwa shilingi milioni 50 kwa awamu ya kwanza. Fedha hizo zitatumika kujenga jengo ambalo litakuwa kwa huduma za mama na mtoto, zikiwemo wodi za wajawazito. Hadi kukamilika jengo hilo linatarajiwa kugharimu shilingi milioni 350. Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali ni kuimarisha vituo vya afya vilivyopo ili viweze kuwa na uwezo wa kufanya upasuaji mdogo wa dharura hasa kwa mama wajawazito ili kupunguza msongamano katika Hospitali ya Wilaya. MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Kwa kuwa Jimbo la Lushoto lina kituo kimoja tu cha afya, ambacho kinahudumia takribani Kata saba; je, Serikali haioni sasa kuwa umefikia wakati wa kujenga vituo vya afya hasa katika Kata ya Makanya, Ngwelo, Kilole, Gare, Ubiri, Magamba, Malibwi pamoja na Kwai? 2 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Swali la pili, kwa kuwa wananchi wa Lushoto wamejitolea kujenga zahanati katika vijiji vya Mzalagembei, Bombo, Mavului, Mbwei, Mazumbai, Ilente, Mbelei, Makanka na Kwemachai, lakini zahanati hizi zimebakia kukamilika tu. Je, Serikali inatoa tamko gani sasa la kumalizia zahanati hizi pamoja na kupeleka watumishi ili wananchi wa Jimbo la Lushoto waondokane na usumbufu wa kutembea umbali mrefu hasa kwa mama zetu na dada zetu? SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa sijui kama vijiji hivyo Mheshimiwa Jafo toka Kisarawe mpaka Lushoto huko. Majibu Mheshimiwa Naibu Waziri. NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza katika kumbukumbu yangu Mheshimiwa Shekilindi amekuwa akiuliza maswali mengi sana ya sekta ya afya, ofisi yetu inakiri mchango mkubwa wa Mheshimiwa Shekilindi katika Jimbo lake na wananchi wake. Mheshimiwa Spika, katika kulifanikisha suala hili, Serikali tumeelekeza mpango wetu wa sasa tunaondoka nao, jinsi gani tutafanya katika mwaka huu wa fedha, kuhakikisha kwamba tunajenga vituo vya afya. Mheshimiwa Shekilindi kwa sababu jana nilikujibu hapa kwamba nina mpango wa kuanzia katika Mkoa wako wa Tanga, tena ratiba nimeibadilisha nitaanza siku ya tarehe 21, na Mheshimiwa Shangazi, nitakuwa naye hiyo tarehe 21, tutaangalia jinsi gani tutafanya baada ya kuwa kule site, kutembelea hivyo vituo. Katika mpango wa bajeti inaokuja lengo kubwa ni kuimarisha vituo vya afya, katika ujenzi kwenye maeneo yetu, tumelenga kwamba angalau kila Halmashauri katika mwaka wa fedha tunaoondoka nao tujenge kituo kimoja cha afya. Mheshimiwa Spika, hali kadhalika katika suala zima la maboma nimesema, tulifanya assessment katika Halmashauri zote, na hili ni agizo la Kamati ya Bajeti, maboma yote ambayo hayajakamilika, tumepata idadi ya maboma. Ndiyo maana nimesema katika bajeti ya mwaka huu unaokuja sasa, ninaomba Waheshimiwa Wabunge, tuungane pamoja kwamba jinsi gani tutafanya mpango mkakati wa kibajeti tuweze kumaliza maboma yale ambayo Mheshimiwa Shekilindi umeyazungumza katika maeneo yako, tukimaliza yale tutakuwa tumesogeza kwa ukaribu zaidi huduma za afya kwa wananchi wetu. Kwa hiyo, nakuunga mkono katika hilo na Serikali imesikiliza kilio chako. MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi, niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Wilaya ya Longido imeanzishwa mwaka 2007, takribani miaka tisa mpaka leo Wilaya ile haina hospitali ya Wilaya, matokeo yake wagonjwa wakipewa 3 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) rufaa, wanapelekwa, Mount Meru - Arusha, kiasi cha kilometa 94 na Serikali imekuwa ikiahidi itajenga Hospitali ya Wilaya. Tunataka majibu ya uhakika, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ya Longido? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Wilaya ya Longido haina Hospitali ya Wilaya kama zilivyo Wilaya nyingine nyingi tu hapa nchini. Niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge kwamba miradi ya Halmashauri, inaanzia kwenye mipango ya Halmashauri na baadaye bajeti ya Halmashauri. Kwa hiyo, niwasihi sana Waheshimiwa Wabunge kwamba kule kwenye mipango ya Halmashauri ndiko vitu hivyo vionekane ili baadaye vikija huku Bungeni tuweze kuvitengea bajeti kwa mujibu wa taratibu za kibajeti. Mheshimiwa Spika, imekuwa ni kawaida mimi kupata wageni wanaoomba vitu nje ya bajeti. Uwezo huo sina na hata Waziri wa Fedha, nadhani hana. Bajeti ikishapitishwa ndicho kitakachofanyika. Hivyo, Wilaya ipange mipango yake, mipango hiyo iwemo kwenye bajeti za Halmashuari zao. Jambo kubwa litakalobakia sasa ni kwa Wabunge ku-demand utekelezaji wa bajeti ili tufikie yale malengo hilo la kwanza. Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kuwasihi Waheshimiwa Wabunge, kwamba kwa sera ya Serikali ni kuweka kituo cha afya kila kata, lakini Serikali tumeamua na tumepanga na Wizara ya Afya kuhakikisha kwamba kila Halmashauri basi angalau ijenge kituo kimoja. Katika Halmashauri 185 tulizonazo, tukifanya tutapata vituo karibu zaidi ya 400, wakati toka uhuru tuna vituo kama 600 tu. Mheshimiwa Spika, nadhani hii itatusaidia sana, wa-dedicate maeneo, indication kulingana na maeneo ambako kuna problem kubwa. Jambo lingine ni kwamba kwenye zahanati wananiomba ramani, ramani ile iliyotolewa na Wizara ya Afya tumekubaliana na Waziri wa Afya kwamba ni kubwa mno kwa zahanati kila kijiji na haitekelezeki kwa sababu ya gharama kubwa karibu ya 1.8 billion ili iweze kutekeleza ule mradi. (Makofi) Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tumekubaliana ku-review ile bajeti, kwa sababu tuna zahanati ambazo zilijengwa wakati tulipopata uhuru tu, zilitosha kutuhudumia mpaka leo tupo. Kwa hiyo, tunadhani zisiwe kubwa kiasi cha kushindwa ku-manage uchumi wa kijiji kwa sababu sehemu kubwa ni michango ya wananchi itatumika pamoja na kwamba Serikali itaweka mkono wake, lakini lazima ramani iwe ya kawaida inayoweza kuwa manageable. (Makofi) 4 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) SPIKA: Nakushukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Nchi TAMISEMI, kwa majibu yako nisisitize kwamba Wizara iendelee kujiandaa kwa ajili ya ile semina kwa Wabunge ambayo itafanyika kwenye kikao kijacho cha Bunge, kwa sababu ni ukweli kabisa usiyopingika kwamba maswali mengi yanayoulizwa kuhusu TAMISEMI, ni maswali ambayo katika mazingira ya kawaida tusingeweza kuyaruhusu hapa. Ni maswali ambayo yanatakiwa wewe mwenyewe kama Diwani uwe umeingiza vitu vyako kwenye bajeti badala ya kuja kuuliza hewa hapa. Kwa hiyo, huko mbele baada ya hiyo semina maswali mengi ya aina hiyo tutakuwa hatuyaweki kwenye Order Paper ya siku hiyo. Mheshimiwa Hawa ghasia! MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi napenda niulize swali la nyongeza. Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Vijijini tayari imeshapanua kituo chake cha afya cha Nanguruwe, ambapo pia kinacho chumba cha upasuaji cha kisasa, chenye vifaa na kimeanza kutoa huduma kwa lengo la kuifanya iwe hospitali ya Wilaya, ambapo majengo yote yanayotakiwa yamekamilika. Je, ni lini Serikali itaibadilishia hadhi kutoka kituo cha afya na kuwa hospitali ya Wilaya baada ya kuwa kila kitu kimekamilika? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli katika mpango wa bajeti tulipokuwa tunajadili na watu wa Mtwara kule Nanguruwe, mwaka huu kwamba wameonesha demand ya kituo hiki, na ni kweli walihakikisha kituo hiki kimekamilisha vitu vyote vya msingi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Hawa Ghasia, tutawasiliana na wenzetu wa Wizara ya Afya kuangalia zile taratibu za kikawaida kuhakikisha kituo hiki sasa kinapandishwa hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya, tukijua wazi kwamba ikiwa hospitali ya Wilaya hata kasma ya bajeti itabadilika eneo hilo na wananchi wataendelea kupata huduma nzuri baada ya kituo hicho kupanda kuwa Hospitali ya Wilaya. (Makofi) SPIKA: Tunaendelea na Wizara inayofuata ambayo ni Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, swali linaulizwa na Mheshimiwa Ester Mmasi. 5 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Na. 95 Uteuzi wa Watumishi Taasisi za Elimu ya Juu MHE. ESTER M. MMASI aliuliza:- Changamoto nyingi kwa upande wa kada za waendeshaji Vyuo Vikuu unatokana na uteuzi
Recommended publications
  • Ruaha Journal of Business, Economics and Management Sciences, Vol.1, Issue 1, 2018  Ms Hadija Matimbwa , Faculty of Business and Management Science, RUCU Iii
    RUAHA JOURNAL of Business, Economics and Management Sciences Faculty of Business and Management Sciences Vol 1, Issue 1, 2018 A. Editorial Board i. Executive Secretarial Members Chairman: Dr. Alex Juma Ochumbo, Dean Faculty of Business and Management Sciences, RUCU Chief Editor: Prof. Robert Mabele, Faculty of Business and Management Sciences, RUCU Managing Editor: Dr.Venance Ndalichako, Faculty of Business and Management Sciences, RUCU Business Manager: Dr. Alberto Gabriel Ndekwa, Faculty of Business and Management Science, RUCU Secretary to the Board: Ms. Hawa Jumanne,Faculty of Business and Management Science, RUCU ii. Members of the Editorial Board Dr. Dominicus Kasilo, Faculty of Business and Management Science, RUCU Bishop Dr. Edward Johnson Mwaikali,Bishop of Mbeya, Formerly with RUCU Dr. Theobard Kipilimba, Faculty of Business and Management Science, RUCU Dr. Esther Ikasu, Faculty of Business and Management Science, RUCU ii Ruaha Journal of Business, Economics and Management Sciences, Vol.1, Issue 1, 2018 Ms Hadija Matimbwa , Faculty of Business and Management Science, RUCU iii. Associate Editors Prof. Enock Wicketye Iringa University,Tanzania. Dr. Enery Challu University of Dar es Dr. Ernest Abayo Makerere University, Uganda. Dr. Vicent Leyaro University of Dar es Salaam Dr. Hawa Tundui Mzumbe University, Tanzania. B. Editorial Note Ruaha Journal of Business, Economics and Management Sciences would like to wish all our esteemed readers on this first appearance A HAPPY NEW YEAR. We shall be appearing twice a year January and July. We hope you will be able to help us fulfill this pledge by feeding us with journal articles, book reviews and other such journal writings and stand ready to read from cover to cover all our issues.
    [Show full text]
  • TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who Will Benefit from the Gas Economy, If It Happens?
    TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who will benefit from the gas economy, if it happens? TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who will benefit from the gas economy, if it happens? TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013 Who will benefit from the gas economy, if it happens? Supported by: 2 TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2013: Who will benefit from the gas economy, if it happens? ACKNOWLEDGEMENTS Policy Forum would like to thank the Foundation for Civil Society for the generous grant that financed Tanzania Governance Review 2013. The review was drafted by Tanzania Development Research Group and edited by Policy Forum. The cartoons were drawn by Adam Lutta (Adamu). Tanzania Governance Reviews for 2006-7, 2008-9, 2010-11, 2012 and 2013 can be downloaded from the Policy Forum website. The views expressed and conclusions drawn on the basis of data and analysis presented in this review do not necessarily reflect those of Policy Forum. TGRs review published and unpublished materials from official sources, civil society and academia, and from the media. Policy Forum has made every effort to verify the accuracy of the information contained in TGR2013, particularly with media sources. However, Policy Forum cannot guarantee the accuracy of all reported claims, statements, and statistics. Whereas any part of this review can be reproduced provided it is duly sourced, Policy Forum cannot accept responsibility for the consequences of its use for other purposes or in other contexts. ISBN:978-9987-708-19-2 For more information and to order copies of the report please contact: Policy Forum P.O. Box 38486 Dar es Salaam Tel +255 22 2780200 Website: www.policyforum.or.tz Email: [email protected] Suggested citation: Policy Forum 2015.
    [Show full text]
  • Issued by the Britain-Tanzania Society No 105 May - Aug 2013
    Tanzanian Affairs Text 1 Issued by the Britain-Tanzania Society No 105 May - Aug 2013 Even More Gas Discovered Exam Results Bombshell Rising Religious Tensions The Maasai & the Foreign Hunters Volunteering Changed my Life EVEN MORE GAS DISCOVERED Roger Nellist, the latest volunteer to join our panel of contributors reports as follows on an announcement by Statoil of their third big gas discovery offshore Tanzania: On 18 March 2013 Statoil and its co-venturer ExxonMobil gave details of their third high-impact gas discovery in licence Block 2 in a year. The new discovery (known as Tangawizi-1) is located 10 kilometres from their first two discoveries (Lavani and Zafarani) made in 2012, and is located in water depth of 2,300 metres. The consortium will drill further wells later this year. The Tangawizi-1 discovery brings the estimated total volume of natural gas in-place in Block 2 to between 15 and 17 trillion cubic feet (Tcf). Depending on reservoir characteristics and field development plans, this could result in recoverable gas volumes in the range of 10-13 Tcf from just this one Block. These are large reserves by international stand- ards. By comparison, Tanzania’s first gas field at Songo Songo island has volumes of about 1 Tcf. Statoil has been in Tanzania since 2007 and has an office in Dar es Salaam. It operates the licence on Block 2 on behalf of the Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) and has a 65% working interest, with ExxonMobil Exploration and Production Tanzania Limited holding the remaining 35%. It is understood that under the Production Sharing Agreement that governs the operations, TPDC has the right to a 10% working participation interest in case of a development phase.
    [Show full text]
  • TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity?
    TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? With Partial Support from a TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? ACKNOWLEDGEMENTS This review was compiled and edited by Tanzania Development Research Group (TADREG) under the supervision of the Steering Group of Policy Forum members, and has been financially supported in part by Water Aid in Tanzania and Policy Forum core funders. The cartoons were drawn by Adam Lutta Published 2013 For more information and to order copies of the review please contact: Policy Forum P.O Box 38486 Dar es Salaam Tel: +255 22 2780200 Website: www.policyforum.or.tz Email: [email protected] ISBN: 978-9987 -708-09-3 © Policy Forum The conclusions drawn and views expressed on the basis of the data and analysis presented in this review do not necessarily reflect those of Policy Forum. Every effort has been made to verify the accuracy of the information contained in this review, including allegations. Nevertheless, Policy Forum cannot guarantee the accuracy and completeness of the contents. Whereas any part of this review may be reproduced providing it is properly sourced, Policy Forum cannot accept responsibility for the consequences of its use for other purposes or in other contexts. Designed by: Jamana Printers b TANZANIA GOVERNANCE REVIEW 2012: Transparency with Impunity? TABLE OF CONTENTS POLICY FORUM’s OBJECTIVES .............................................................................................................
    [Show full text]
  • Kitabu Cha Kumbukumbu Za Wabunge
    BUNGE LA TANZANIA ____________ KITABU CHA KUMBUKUMBU ZA WABUNGE BUNGE LA KUMI NA MBILI Toleo la Nne - Agosti, 2021 1 SEHEMU YA KWANZA UTANGULIZI Bunge limekuwepo toka tupate Uhuru mwaka 1961 na kabla ya Uhuru kuanzia mwaka 1926. Wabunge nao wameendelea kuwepo kwa vipindi tofauti na kwa idadi inayobadilika kila wakati wakitekeleza wajibu wao muhimu wa kutunga sheria na kuisimamia Serikali kwa niaba ya wananchi kwa mujibu wa Katiba ya nchi. Bunge lilipoanza mwaka 1926, Wabunge walikuwa ishirini na moja (21) na mwaka 1961 ulipopatikana Uhuru Wabunge waliongezeka kufikia themanini (80) na baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 idadi ya Wabunge iliongezeka na kufikia Wabunge 357. Hata hivyo, baada ya Tume ya Uchaguzi kuona umuhimu wa kuongeza idadi ya majimbo kutokana na sababu mbalimbali sasa hivi idadi ya Wabunge ni 393. Kitabu hiki cha Kumbukumbu za Wabunge kimegawanyika katika Sehemu kuu Kumi na Nne. Katika sehemu hizo, kitabu kimeorodhesha Wabunge wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na anuani zao, namba zao simu za mkononi na majimbo au aina ya uwakilishi wao Bungeni chini ya picha zao ili kurahisisha mawasiliano. Katika mchanganuo wa kila sehemu, Sehemu ya Kwanza ni Utangulizi. Aidha, Wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Bunge ambao ndio wasimamizi wa shughuli za Bunge wameorodheshwa katika Sehemu ya Pili ya kitabu hiki ikifuatiwa na Uongozi wa Ofisi ya Bunge katika Sehemu ya Tatu. 2 Sehemu ya Nne imeorodhesha Wabunge wote wa Majimbo wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Mikoa ikifuatiwa na Sehemu ya Tano ambayo imeorodhesha Wabunge wote wa Viti Maalum kulingana na uwakilishi wa vyama vyao Bungeni ikianzia na Chama cha Mapinduzi (CCM) na ikifuatiwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Sehemu ya Sita imeorodhesha Wabunge kupitia nafasi ya Kuteuliwa na Rais na Sehemu ya Saba itaorodhesha Wabunge kutoka Baraza la Wawakilishi.
    [Show full text]
  • Meda Economic Development Associates (Meda)
    0 YALIYOMO Contents YALIYOMO .............................................................................................................. 0 1. UTANGULIZI ....................................................................................................... 5 2. SEKTA YA ELIMU .............................................................................................. 6 2.1. KUFUNGULIWA KWA SEKONDARI MPYA ............................................... 6 2.2. SEKONDARI MPYA ZINAZOJENGWA ........................................................ 8 2.3. VYUMBA VIPYA VYA MADARASA .......................................................... 10 2.4. UJENZI WA MAKTABA ................................................................................ 12 2.5. UJENZI WA SHULE SHIKIZI ........................................................................ 13 2.6. MIRADI YA SERIKALI KWENYE SEKTA YA ELIMU ............................. 15 2.6.1. EDUCATION QUALITY IMPROVEMENT PROGRAMME (EQUIP) .... 15 2.6.2. EDUCATION PROGRAMME FOR RESULTS (EP4R) ............................. 15 2.6.3. UGAWAJI WA VITABU VYA SAYANSI NA KIINGEREZA ................. 15 3. SEKTA YA AFYA .............................................................................................. 16 3.1. ZAHANATI ZINAZOTOA HUDUMA ZA AFYA ........................................ 16 3.2. ZAHANATI MPYA ZINAZOJENGWA NA WANAVIJIJI .......................... 17 3.3. UJENZI WA WODI ZA MAMA NA MTOTO ............................................... 18 3.4. VITUO VYA AFYA ........................................................................................
    [Show full text]
  • Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA SITA (DAILY SUMMARY RECORD OF PROCEEDINGS) 11 NOVEMBA, 2014 MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA KIKAO CHA SITA – 11 NOVEMBA, 2014 I. DUA Saa 3.00 Asubuhi kikao kilianza kikiongozwa na Mhe. Naibu Spika (Mhe Job Y. Ndugai) na alisoma Dua. Makatibu Mezani 1. Ramadhani Abdallah Issa 2. Asia Minja 3. Hellen Mbeba II. MASWALI Maswali yafuatayo yaliulizwa na yalijibiwa:- 1. OFISI YA WAZIRI MKUU Swali . 67 – Mhe. Charles J.P. Mwijage Nyongeza (i) Mhe. Charles Mwijage (ii) Mhe. Joshua Nassari Swali. 68- Mhe. Hezekiah Chibulunje (K.n.y – Mhe. David Mallole) Nyongeza (i) Mhe. Hezekiah Chibulunje Swali. 69 – Mhe. Josephat Sinkamba Kandege Nyongeza (i) Mhe. Josephat Kandege 2. OFISI YA RAIS (UTAWALA BORA) Swali. 70 – Mhe. Amina Abdulla Amour 2 Nyongeza (i) Mhe. Amina Abdullah Amour 3. OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA URATIBU) Swali. 71 – Mhe. Leticia Mageni Nyerere Nyongeza i. Mhe. Leticia Nyerere ii. Mhe. Mohammed Habib Mnyaa 4. OFISI YA MAKAMU WA RIAS (MAZINGIRA) Swali. 72 – Mhe. Victor Kilasile Mwambalaswa Nyongeza i. Mhe. Victor Kilasile Mwambalaswa. 5. WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Swali. 73 – Mhe. Diana Mkumbo Chilolo Nyongeza i. Mhe. Diana Mkumbo Chilolo 6. WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA Swali. 74 – Mhe. Sylvestry Francis Koka Nyongeza i. Mhe. Sylvestry Koka ii. Mhe. Salim Masoud 7. WIZARA YA UCHUKUZI Swali. 75 – Mhe. Prof. David Mwakyusa (k.n.y Mhe. Luckson Mwanjale). Nyongeza i. Mhe. Prof. David Mwakyusa. 3 Swali. 76 – Mhe.
    [Show full text]
  • Tarehe 7 Februari, 2017
    NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA SITA Kikao cha Saba – Tarehe 7 Februari, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Tukae. Katibu. NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na: MHE. PROF. NORMAN A. S. KING – MWENYEKITI WA KAMATI YA BUNGE YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kwa kipindi cha kuanzia Januari, 2016 hadi Januari, 2017. MHE. DOTO M. BITEKO -MWENYEKITI WA KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwa kipindi cha kuanzia Januari 2016 hadi Januari 2017. NAIBU SPIKA: Ahsante. Katibu! NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI: MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na maswali, Ofisi ya Rais - TAMISEMI. Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge wa Viti Maalum, sasa aulize swali lake. Na. 69 Tatizo la Ulevi MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza:- 1 NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT) Ulevi wa kupita kiasi hasa wa pombe za kienyeji umekuwa na athari kubwa za kiafya na kiakili kwa Watanzania wenye tabia ya ulevi wa kukithiri:- Je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na tatizo hilo hasa ikizingatiwa kuwa Sheria ya Vileo ya mwaka 1969 ni ya zamani sana kiasi kwamba inawezekana kabisa haikidhi mabadiliko ya hali halisi ya vileo kwa wakati huu. NAIBUWAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, pombe za kienyeji zimeainishwa katika Kifungu cha pili (2) cha tafsiri katika Sheria ya Vileo, Sura ya 77.
    [Show full text]
  • Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bunge La Tanzania
    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA KUMI NA TISA (DAILY SUMMARY RECORD OF PROCEEDINGS) 28 NOVEMBA, 2014 MKUTANO WA KUMI NA SITA NA KUMI NA SABA YATOKANAYO NA KIKAO CHA KUMI NA TISA (SUMMARY RECORD OF PROCEEDINGS – NINETEENTH SITTING) TAREHE 28 NOVEMBA, 2014 I. DUA: Mhe. Spika Anne S. Makinda alisoma Dua saa 3.00 asubuhi na Kikao kiliendelea. MAKATIBU MEZANI: 1. Ndg. Theonest Ruhilabake 2. Ndg. Lawrence Makigi 3. Ndg. Neema Msangi II. MASWALI Maswali yafuatayo yaliulizwa na kujibiwa; 1. OFISI YA WAZIRI MKUU Swali Na. 229: Mhe. Hamoud Abuu Jumaa Nyongeza: (i) Mhe. Hamoud Abuu Jumaa (ii) Mhe. Murtaza Ally Mangungu Swali Na. 230: Mhe. Suzan A. J. Lyimo Nyongeza: (i) Mhe. Suzan A. J. Lyimo (ii) Mhe. Michael L. Laizer (iii) Mhe. Mch. Peter Msigwa Swali Na. 231: Mhe. Ismail Aden Rage [kny: Mhe. Dkt. Hamis Kigwangalla] Nyongeza: (i) Mhe. Ismail Aden Rage (ii) Mhe. Ezekia Dibogo Wenje 2 2. WIZARA YA NISHATI NA MADINI Swali Na. 232: Mhe. Faith Mohammed Mitambo [kny: Mhe. Fatma Mikidadi] Nyongeza: (i) Mhe. Faith Mohammed Mitambo Swali Na. 233: Mhe. John Paul Lwanji Nyongeza: (i) Mhe. John Paul Lwanji (ii) Mhe. Joseph Osmund Mbilinyi Swali Na. 234: Mhe. John Damiano Komba [kny. Mhe.Juma Abdallah Njwayo] Nyongeza: (i) Mhe. John Damiano Komba (ii) Mhe. Mtutura Abdallah Mtutura (iii) Mhe. Moshi Selemani Kakoso 3. WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI Swali Na. 235: Mhe. AnnaMaryStella John Mallac Nyongeza: (i) Mhe. AnnaMaryStella John Mallac (ii) Mhe. Rukia Kassim Ahmed Swali Na.
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE ___MKUTANO WA TATU Kikao Cha
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Arobaini na Tatu – Tarehe 3 Juni, 2021 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naomba tukae. Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Mkutano wetu wa Tatu, leo ni Kikao cha Arobaini na Tatu. Katibu NDG. NENELWA MWIHAMBI, ndc – KATIBU WA BUNGE: HATI ZA KUWASILISHA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022. SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, aah sasa hivi unavaa sketi ndefu, hataki ugomvi na Mgogo. (Kicheko) Tunaendelea, Katibu. 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) NDG. NENELWA MWIHAMBI, ndc – KATIBU WA BUNGE: MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Maswali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Waziri Mkuu karibu sana. (Makofi) Waheshimiwa Wabunge, nawakumbusha tena kuhusu maswali ya kisera sio matukio, sio nini, ni ya kisera. Tunaanza na Mheshimiwa Mbunge wa Liwale, Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, maswali kwa kifupi. MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kwanza kuuliza swali kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Mheshimiwa Spika, swali langu litahusu sekta ya korosho. Mwaka huu tumepata taarifa kwamba Serikali ilijipanga kutupatia pembejeo wakulima wa zao la korosho kwa maana kwamba waje kuzilipa baadaye kwenye mjengeko wa bei. Hata hivyo, kuna taharuki kubwa kwa wakulima wetu wa korosho baada ya Bodi ya Korosho kuleta waraka kwenye Halmashauri zetu, wakiwaambia kila mkulima akipeleka zao lile kwenye mnada kila kilo moja itakatwa shilingi 110 bila kujali kwamba mkulima yule amechukua pembejeo kwa kiwango gani.
    [Show full text]
  • Nakala Ya Mtandao (Online Document) 1 MAJADILIANO YA BUNGE
    Nakala ya Mtandao (Online Document) MAJADILIANO YA BUNGE __________ MKUTANO WA ISHIRINI __________ Kikao cha Ishirini na Moja - Tarehe 5 Juni, 2015 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, napenda kuchukua nafasi hii kuwapa pole wote kwa msiba uliotupata, msiba ulitokea wakati nikiwa Geneva ambapo tulikuwa na kikao cha Kamati Ndogo ya maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Maspika wote duniani utakaofanyika mwezi wa Nane, sasa kuna Maspika kumi ndiyo tupo kwenye maandalizi ya mkutano huo na kilikuwa ni kikao chetu cha mwisho kabla ya mkutano huo. Kwa hiyo, wakati msiba unatokea nilikuwa huko, nilipewa taarifa na nilisikitika sana. Kwa hiyo, tutatangaza baadaye mchana, ni akina nani watakaokwenda kuzika kesho. Katibu! HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI (MHE. CHARLES M. KITWANGA): Randama za Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016. NAIBU WAZIRI WA MAJI: Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Maji kwa mwaka wa Fedha, 2015/2016. MHE. DAVID H. MWAKYUSA (k.n.y. MHE. PROF. PETER M. MSOLLA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015, pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa Fedha 2015/2016. MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED (k.n.y. MHE. MAGDALENA H. SAKAYA - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI KWA WIZARA YA MAJI): Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Fedha kwa Wizara ya Maji kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016.
    [Show full text]
  • MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao Cha Ishirini Na Tano
    NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) BUNGE LA TANZANIA ________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Tano – Tarehe 10 Mei, 2019 (Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA: Tukae, Katibu. NDG. RUTH MAKUNGU – KATIBU MEZANI: Maswali. MASWALI NA MAJIBU NAIBU SPIKA: Maswali, Waheshimiwa Wabunge tutaanza na Ofisi ya Rais TAMISEMI. Mheshimiwa Joel Mwaka Makanyaga Mbunge wa Chilonwa, sasa aulize swali lake. Na. 200 Kukamilisha Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji – Chilonwa MHE. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Chilonwa iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ambayo kwa sasa imefikia kwenye linta? NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:- 1 NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joel Mwaka Makanyaga, Mbunge wa Chilonwa, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Chilonwa ni miongoni mwa Kata 36 za Wilaya ya Chamwino, ina vijiji viwili vya Nzali na Mahama, Kata ina huduma za Zahanati moja iliyopo katika Kijiji cha Nzali. Wananchi wa kijiji cha Mahama walianzisha ujenzi wa Zahanati ya Kijiji ambayo kwa sasa jengo limefikia hatua ya lInta. Katika kuunga mkono juhudi za wananchi, Halmashauri ya Chamwino katika mwaka wa fedha 2019/2020 kupitia mapato yake ya ndani imetenga shilingi milioni 30 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa zahanati hiyo katika Kijiji cha Mahama. Ahsante. NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Joel Makanyaga, swali la nyongeza.
    [Show full text]