Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)

Total Page:16

File Type:pdf, Size:1020Kb

Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document) Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Arobaini na Mbili – Tarehe 14 Agosti, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI: Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. MUSTAFA H. MKULLO): Hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2006/2007. MWENYEKITI WA KAMATI YA FEDHA NA UCHUMI: Maoni ya Kamati ya Fedha Kuhusu Utekelezaji wa Wizara ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha Uliopita, Pamoja na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2006/2007. SPIKA: Ahsante sana Mwenyekiti, kwa taarifa ya wageni wetu huyo ni Dr. Abdallah Omar Kigoda, Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Uchumi. Oh leo naona mambo ni mazito kidogo wanakuja wazito watupu. MHE. HAMAD RASHID MOHAMED - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI –WIZARA YA FEDHA, MIPANGO NA UWEZESHAJI: Maoni ya Kambi ya Upinzani Kuhusu Utekelezaji wa Wizara ya Fedha kwa Mwaka wa Fedha Uliopita, Pamoja na Maoni Kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka 2006/2007. SPIKA: Kwa taarifa ya wageni pia aliyewasilisha taarifa sasa hivi ni Mheshimiwa Hamad Rashid Mohamed, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani ndani ya Bunge. (Makofi) MASWALI NA MAJIBU Na. 395 1 Uharibifu wa Mazingira na Kampuni ya Placer Dome MHE ALI KHAMIS SEIF (K.n.y. MHE. CHACHA Z. WANGWE) aliuliza:- Kwa kuwa, Kampuni ya Placer Dome ina mwaga maji na takataka zenye sumu aina ya cynide na mercury kwenye mto Tigithe, ambapo wananchi wa maeneo hayo wanayatumia maji ya Mto huu kwa shughuli mbalimbali na tayari watu kadhaa na mifugo imeathirika na kemikali hizo:- (a) Je, Serikali inaweza kufanya Environmental Impact Assessment ya mgodi huo ili kuwanusuru watumiaji wa maji ya Mto huo kutokana na kemikali hizo? (b) Kwa kuwa, Mto Tigithe humwaga maji yake kwenye Mto Mara na Mto Mara humwaga maji yake Ziwa Victoria. Je, Serikali haioni kwamba, samaki wanaovuliwa ziwani hawafai kwa matumizi ya binadamu kutokana na kemikali hizo na itafanyaje? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS – MAZINGIRA alijibu:- Mheshimiwa Spika, kabla sijajibu swali la Mheshimiwa Wangwe, Mbunge wa Tarime, lenye sehemu (a) na (b) napenda kutoa maelezo mafupi kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Mgodi wa Dhahabu wa Placer Dome huko katika eneo la Gokoni Nyabigena karibu na Mto Tigithe, Wilaya ya Tarime. Shughuli inayofanyika katika eneo la Gokona ni uchimbaji udongo (Malighafi) ambao husafirishwa Nyabirama umbali wa kilomita saba. Eneo hili ni kilomita 100 Mashariki ya Ziwa Victoria. Mheshimiwa Spika, cyanide kemikali ambayo kiasi chake kikiwa kikubwa katika mchanganyiko wa vimilika huwa ni sumu kali hutumia viwandani katika kutengeneza dawa za kuulia wadudu, plastiki, rangi, nailoni na katika uchimbaji wa madini. Kiasi kidogo cha cyanide upatikana kiasilia katika vyakula kama vile mihogo, ulezi, kabeji na mchicha. Hata hivyo hakuna matatizo ya muda mrefu ya kiafya kuwepo na kiasi hiki kidogo cha cyanide. Mheshimiwa Spika, Placer Dome hutumika sana katika uchenguaji wa dhahabu (Gold Processing) uchenguaji hufanyika Nyabirama na mabaki ya uchafu wa uchenguaji yenye cyanide huwekwa kwenye kwenye bwawa maalum (tailing storage facility) ili kudhibiti uvujaji unaoweza kuathiri mazingira, maji yenye kiasi kidogo ya cyanide yanayotokana na uchafu huo nayo huhifadhiwa katika bwawa maalum kabla ya kurejeleshwa kiwandani. Bwawa limewekewa kinga madhubuti. Uangalizi wa kila mara (Environmental Monitoring) hufanywa ili kudhitibi uvujaji wa aina yoyote ile unaoweza kupenya chini kwa chini hadi Mto Tigithe au Mto Mara. Kampuni ina maabara ambayo inafanya uchunguzi wa sampuli mbalimbali ili hatua za haraka zichukuliwe endapo panatokea matatizo. Uchunguzi wa muda mrefu wa 2 sampuli kutoka Mto Mara na Mto Tigithe umeonyesha hakuna dalili za kuwepo kwa chembe chembe (traces) za ‘cyanide’. Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo, sasa napenda kujibu swali la Mheshimiwa Wangwe, Mbunge wa Tarime, kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Spika, tathmini ya Athari kwa Mazingira (Environmental Impact Assessment) ya mgogi wa Placer Dome ilifanyika mwaka 2000 kabla ya kuanza rasmi shughuli za uzalishaji na iliwasilishwa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Wizara ya Nishati na Madini. Ripoti na Mpango wa Usimamizi wa Mazingira (Environmental Management Plan) ilijadiliwa na kukubaliwa na wadau wote toka sekta husika. Mwaka 2002 NEMC ilishauri Kampuni ya Placer Dome kufanya uchunguzi wa kina ili kubainisha athari kwa mazingira, wafanyakazi, na jamii inayozunguka mgodi, zinazoweza kutokea kutokana na shughuli za uchimbaji. Matokeo ya uchunguzi huo yaliiwezesha Kampuni hiyo kuboresha Mpango wa Usimamizi wa Mazingira (EMP) ya kutengeneza Mpango wa Nyongeza uliozingatia ushauri huo. Mwaka huo huo ulifanyika utafiti ili kujua hali ya viumbe hai katika Mto Mara na Mto Tigithe. Matokeo ya utafiti huo hayakubainisha madhara yanayotokana na shughuli za uchimbaji yanayohatarisha maisha ya viumbe hai katika mito hiyo. Hata hivyo Serikali inawataka wenye migodi kwa kushirikiana na wataalamu toka NEMC na Wizara ya Nishati na Madini, kuendelea kufanya Ukaguzi wa Mazingira environment audit na kubaini kama kuna athari zote, ili hatua za haraka zichukuliwe inapobidi. Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mgodi wa Placer Dome hautumii zebaki (mercury) katika uchenguaji wa dhahabu hakuna uwezekano wa kuwepo kemikali hiyo katika maji taka yanayotokana na shughuli za mgodi huo. (b) Mheshimiwa Spika, mwaka 2005 kupitia Mradi wa Hifadhi ya Mazingira ya Ziwa Victoria kwa kushirikiana na Shirika Lisilo la Kiserikali la Kimataifa la Hifadhi ya Mazingira na Wanyamapori na Kampuni ya Placer Dome ilifanya utafiti wa hali ya samaki katika Ziwa Victoria na Mto Mara. Matokeo ya utafiti huo yalionyesha kuwa vipimo vya ubora wa samaki wa Ziwa Victoria kwa matumizi ya binadamu vipo juu ya viwango vya Kimataifa. Aidha, maabara za kisasa zilizo kwenye viwanda vya minofu na Taasisi za Kiserikali zinatumika kupima ubora wa minofu ya samaki. Kwa kuzingatia hayo samaki wanaovuliwa toka Ziwa Victoria huuzwa kwenye masoko ya Ulaya ambako viwango vya ubora vinapewa kipaumbele. Hakuna malalamiko toka kwenye masoko ya ndani na nje ya Tanzania ndiyo maana uuzaji wa minofu ya samaki nje ya nchi bado unaendelea. 3 Mheshimiwa Spika, kutokana na maelezo haya, napenda kuwahakikishia wananchi wanunuzi wa samaki kutoka nje ya Tanzania vile vile napenda kumhakikishia huyo Bwana Hubert Sauper kwamba samaki wanaovuliwa toka Ziwa Victoria ni salama kabisa hawana chembechembe cha aina yoyote zenye kuhatarisha afya ya binadamu. MHE. ALI KHAMIS SEIF: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa sababu Mheshimiwa waziri amekiri kuwa cyanide kwa kiwango kikubwa inaweza ikaleta athari. Na amekiri kuwa huko kunakochimbwa madini ni kuwa kuna hifadhi ya cyanide katika mabwawa. Je, Mheshimiwa Waziri hakuna njia nyingine ya kuhifadhi cyanide isipokuwa kuwekwa katika bwawa? SPIKA: Halikusikika Mheshimiwa Mbunge. Ebu tafadhali rudia swali. MHE. ALI KHAMIS SEIF: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa sababu Mheshimiwa Waziri amekiri kuwa iko cyanide ambayo inatumiwa kwa kuhifadhia dhahabu. Na amekiri kuwa cyanide inahifadhiwa katika mabwawa na cyanide ikiwa nyingi inakuwa ni sumu, je, hakuna njia nyingine ya kuhifadhi cyanide isipokuwa katika mabwawa? SPIKA: Yaani Waziri cyanide lazima itupwe kwenye mabwawa tu hakuna njia nyingine ya kuweza kuyatokomeza? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS – MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, cyanide ni kemikali ambayo kiasilia inakuwa na carbon na nitrate. Kuweza kuharibika haraka yaani ikapoteza nguvu yake ya kemikali kwa kukutana na mionzi ya jua ndiyo maana huwekwa kwenye mabwawa ambayo moja kwa moja inakutana na mionzi ya jua na kuharibika. WAZIRI WA KAZI, AJIRA NA MAENDELEO YA VIJANA: Mheshimiwa Spika, kuweka cyanide kwenye mabwawa ni katika hatua muhimu ya detoxification yaani kuifanya cyanide isiwe nafuu. Mheshimiwa Spika, cyanide ni madini ambayo ni sumu sana na yakiwepo katika kiwango kidogo sana yanaweza kuleta maafa. Kwa hivi kiasi ambacho kinakuwa pale kikiingia kwenye ziwa na kuwa detoxified hakina madhara yoyote. (Makofi) Na. 396 Uchafuzi wa Mazingira MHE. RIZIKI OMAR JUMA (K.n.y.MHE. SUSAN A. J. LYIMO) aliuliza:- Kwa kuwa, mazingira ni suala mtambuka na kwamba, Serikali imejitahidi sana kudhibiti hali ya uchafu wa mazingira ikiwa ni pamoja na kuongeza ushuru kwenye mifuko ya plastiki lakini pamoja na juhudi hizo bado mifuko ya plastiki maarufu kama 4 Rambo inaendelea kuzagaa kwenye sehemu nyingi hasa za mijini na kuhatarisha afya za watu na wanyama wachungwao:- (a) Kwa kuwa, historia inaonyesha kuwa, mifuko hiyo haikuwepo katika miaka ya nyuma na badala yake ilitumika mifuko ya karatasi za khaki na magazeti. Je, Serikali haioni hoja ya kuzuia kabisa mifuko ya Rambo isitumike tena hapa nchini na kurudia utaratibu wa nyuma? (b) Kama Serikali haiwezi kuzuia bidhaa hizo za plastiki, kwa nini isinunue kinu ili mifuko hiyo pamoja na bidhaa za aina hiyo zifanyiwe recycling? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS – MAZINGIRA alijibu:- Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Susan Lyimo, Mbunge Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mwezi April 2006 Serikali ilitoa tamko la kupiga marufuku utengenezaji, uagizaji, ununuzi na matumizi ya mifuko ya plastiki laini na ile ya kufungia maji na maji ya matunda. Serikali imeongeza kodi kwenye mifuko mingine ya plastiki kwa asilimia 120. Aidha, Shirika la Viwango liko katika hatua za mwisho katika kuweka viwango vya plastiki vinavyokubalika
Recommended publications
  • 1458125471-Hs-6-8-20
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _________________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________________ MKUTANO WA KUMI Kikao cha Saba – Tarehe 6 Februari, 2008 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita Katibu kwa orodha ya shughuli za leo, ninapenda kwanza nimpongeze Corporal Fauster. Napenda niwafahamisheni, ni mara ya kwanza katika historia ya Bunge letu Spika kutanguliwa na Sergeant-At-Arms ambaye ni mwanamke. Tulikwishasema awali Bunge hili litaendeshwa kwa viwango na viwango ni pamoja na kuzingatia jinsia. Hakuna kazi ambazo ni za wanaume tu peke yao. Ahsante sana Corporal Fauster. (Makofi) Waheshimiwa Wabunge, nimerejea, nimesitisha safari ya Marekani. Nalazimika kutoa maelezo kwa sababu ya maneno mengi tu. Safari ile kwenda kule ilipangwa kwa kuzingatia mambo mawili :- Moja, ni umuhimu tu wake. Wenzetu Amerika, wiki ya pili ya Mwezi Februari kila mwaka mihimili yote mitatu ya Dola wanakaa pamoja kwa mlo wa asubuhi, inaitwa National Prayer Breakfast. Pamoja na mambo mengi yatakayofanyika, Rais wao ataongea pale kwenye Prayers Breakfast. Lakini wanawatambua baadhi ya viongozi mashuhuri ambao wana ushirikiano mwema nao. Mimi kama Spika wa Bunge hili, nilialikwa kwa msingi huo. Kwa hiyo, hoja kwamba labda ningeweza kumtuma mtu mwingine, haipo kwa sababu ni mwaliko wa heshima kwa jina. (Makofi) La pili ni kwamba, nikitazama ratiba na Kanuni ya 24 ya Bunge, ilikuwa ni kwamba Miswada inaendelea na kwa hiyo, nilidhani mambo mengine kama vile taarifa za Kamati yangekuja kama ilivyo kawaida katika wiki ya mwisho, na mimi nilikuwa narudi Ijumaa asubuhi. Kwa hiyo, yote yangewezekana. Sasa hilo lilishindikana, niliwaarifu wenyeji wetu kule Marekani na wamesikitika, lakini wamesema kama wanasiasa, wameelewa,kwa sababu niliwaeleza mazingira ambayo yalinifanya nisiende.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge Mkutano Wa Kumi Na Nane
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Tatu - Tarehe 28 Januari, 2010 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI KWA WAZIRI MKUU SPIKA: Muuliza swali wa kwanza ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani. MHE. HAMAD RASHID MOHAMED : Mheshimiwa Spika, ahsante. Mheshimiwa Waziri Mkuu nafikiri unakumbuka tarehe 5 Novemba, 2009 Dr. Aman Abeid Karume na Maalim Seif Sharif Hamad, walikutana na hatimaye chama cha CUF kikamtambua na kuitambua Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Ni nini position ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya maridhiano haya? WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, wako watu watatu au wanne wakisimama najua ni yaleyale tu. (Kicheko) Mheshimiwa Spika, sina hakika kama nitakuwa na jibu zuri sana, lakini niseme kwamba tunao mfumo mzuri sana wa namna ya kufanya maamuzi makubwa kama haya. Sasa ni kweli jambo hili limetokea pale Zanzibar lakini mimi imani yangu ni kwamba katika kutekeleza ule mfumo wa namna ya kufanya maamuzi yafikie ukomo wake naamini ndani ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na kwa kutumia Kamati maalumu ya Chama cha Mapinduzi ndani ya Zanzibar bila shaka jambo hili litakuwa tayari limeshazungumzwa, ndiyo imani yangu mimi. (Makofi) Naamini vilevile kwamba baada ya hapo hatua itakayofuata ni kulileta jambo hili sasa formally kwenye Chama cha Mapinduzi kupitia Kamati Kuu pamoja na Halmashauri Kuu ya Taifa. Kwa hiyo, kama ni jibu sahihi juu ya nini mtazamo wa Serikali itakuwa ni baada ya chama kuwa kimefanya maamuzi na kuielekeza Serikali ifanye nini katika jambo hili.
    [Show full text]
  • Bunge La Tanzania
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Kwanza – Tarehe 9 Juni, 2009 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) WIMBO WA TAIFA (Hapa Wabunge Waliimba Wimbo wa Taifa) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta ) Alisoma Dua KIAPO CHA UAMINIFU Mbunge afuataye aliapa Kiapo cha Uaminifu na kukaa katika nafasi yake Bungeni:- Mheshimiwa Lolensia Jeremiah Maselle Bukwimba SPIKA: Ahsante sana, leo shamrashamra zimepita kiasi; nimetafuta ushauri wa sheria bado sijapewa kuhusu shamrashamra hizi kwa kiwango hiki kama inaruhusiwa kwa kanuni lakini hayo sasa ni ya baadaye. (Kicheko) T A A R I F A Y A S P I K A SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, katika Mkutano wa Kumi na Tano wa Bunge hili, tulipitisha Miswada mitano ya sheria iitwayo The Human DNA Regulation Bill, 2009, The Fertilizers Bill, 2009, The Insurance Bill, 2009, The Water Resources Management Bill, 2009 na The Water Supply and Sanitation Bill, 2009. Mara baada ya kupitishwa na Bunge na baadae kupita katika hatua zake zote za uchapishaji, Miswada hiyo ilipelekwa kwa Mheshimiwa Rais ili kupata kibali chake kwa mujibu wa Katiba. Kwa taarifa hii, nafurahi kuwaarifu Wabunge wote na Bunge hili Tukufu kwamba, tayari Mheshimiwa Rais amekwishatoa kibali kwa Miswada yote hiyo mitano na sasa ni sheria za nchi, ambapo The Human DNA Regulation Act, 2009 inakuwa ni Sheria Namba Nane ya Mwaka 2009; The Fertilizers Act, 2009 ni Sheria Namba Tisa ya 1 Mwaka 2009; The Insurance Act, 2009 ni Namba Kumi ya Mwaka 2009; The Water Resources Management, Act 2009 ni Namba Kumi na Moja ya Mwaka 2009; na Sheria Namba Kumi na Mbili ya Mwaka 2009 ni ile ya Water Supply and Sanitation Act, 2009.
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE _________________ MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 10 Februari, 2010 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI (MHE. OMAR YUSSUF MZEE): Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Benki ya Posta Tanzania, kwa Mwaka 2008 [The Annual Report and Accounts of The Tanzania Postal Bank for the Year 2008]. The Mid-Term Review of the Monetary Policy Statement of The Bank of Tanzania for the Year 2009/2010. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini juu ya Taarifa ya Serikali Kuhusu Ubinafsishwaji wa Mgodi wa Kiwira. Taarifa ya Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Mchakato wa Zabuni ya Kuzalisha Umeme wa Dharura Ulioipa Ushindi Kampuni ya Richmond Development Company LLC. Houston Texas - Marekani Mwaka 2006. MWENYEKITI WA KAMATI YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelzaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Uendeshaji Usioridhisha wa Shirika la Reli Tanzania uliofanywa na Kampuni ya RITES ya India. 1 Taarifa ya Kamati ya Miundombinu Kuhusu Taarifa ya Serikali ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge Kuhusu Utendaji wa Kazi Usioridhisha wa Kampuni ya TICTS. MASWALI NA MAJIBU Na. 145 Usimamizi wa Ukaguzi wa Fedha za Halmashauri MHE. HERBERT J. MNTANGI aliuliza:- Kwa kuwa, kiasi cha fedha kinachopelekwa katika Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Jiji ni kikubwa na kinahitaji usimamizi wa ziada:- Kwa kuwa kitengo cha ukaguzi wa ndani kipo chini ya Mkurugenzi Mtendaji.
    [Show full text]
  • Coversheet for Thesis in Sussex Research Online
    A University of Sussex DPhil thesis Available online via Sussex Research Online: http://sro.sussex.ac.uk/ This thesis is protected by copyright which belongs to the author. This thesis cannot be reproduced or quoted extensively from without first obtaining permission in writing from the Author The content must not be changed in any way or sold commercially in any format or medium without the formal permission of the Author When referring to this work, full bibliographic details including the author, title, awarding institution and date of the thesis must be given Please visit Sussex Research Online for more information and further details Accountability and Clientelism in Dominant Party Politics: The Case of a Constituency Development Fund in Tanzania Machiko Tsubura Submitted for the Degree of Doctor of Philosophy in Development Studies University of Sussex January 2014 - ii - I hereby declare that this thesis has not been and will not be submitted in whole or in part to another University for the award of any other degree. Signature: ……………………………………… - iii - UNIVERSITY OF SUSSEX MACHIKO TSUBURA DOCTOR OF PHILOSOPHY IN DEVELOPMENT STUDIES ACCOUNTABILITY AND CLIENTELISM IN DOMINANT PARTY POLITICS: THE CASE OF A CONSTITUENCY DEVELOPMENT FUND IN TANZANIA SUMMARY This thesis examines the shifting nature of accountability and clientelism in dominant party politics in Tanzania through the analysis of the introduction of a Constituency Development Fund (CDF) in 2009. A CDF is a distinctive mechanism that channels a specific portion of the government budget to the constituencies of Members of Parliament (MPs) to finance local small-scale development projects which are primarily selected by MPs.
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Ishirini na Nne – Tarehe 18 Julai, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita muuliza swali la kwanza nina matangazo kuhusu wageni, kwanza wale vijana wanafunzi kutoka shule ya sekondari, naona tangazo halisomeki vizuri, naomba tu wanafunzi na walimu msimame ili Waheshimiwa Wabunge waweze kuwatambua. Tunafurahi sana walimu na wanafunzi wa shule zetu za hapa nchini Tanzania mnapokuja hapa Bungeni kujionea wenyewe demokrasia ya nchi yetu inavyofanya kazi. Karibuni sana. Wapo Makatibu 26 wa UWT, ambao wamekuja kwenye Semina ya Utetezi na Ushawishi kwa Harakati za Wanawake inayofanyika Dodoma CCT wale pale mkono wangu wakulia karibuni sana kina mama tunawatakia mema katika semina yenu, ili ilete mafanikio na ipige hatua mbele katika kumkomboa mwanamke wa Tanzania, ahsanteni sana. Hawa ni wageni ambao tumetaarifiwa na Mheshimiwa Shamsa Selengia Mwangunga, Naibu Waziri wa Maji. Wageni wengine nitawatamka kadri nitakavyopata taarifa, kwa sababu wamechelewa kuleta taarifa. Na. 223 Barabara Toka KIA – Mererani MHE. DORA H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa, Mererani ni Controlled Area na ipo kwenye mpango wa Special Economic Zone na kwa kuwa Tanzanite ni madini pekee duniani yanayochimbwa huko Mererani na inajulikana kote ulimwenguni kutokana na madini hayo, lakini barabara inayotoka KIA kwenda Mererani ni mbaya sana
    [Show full text]
  • Hii Ni Nakala Ya Mtandao (Online Document)
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA NNE Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 30 Juni, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua MASWALI NA MAJIBU SPIKA:- Waheshimiwa Wabunge kwenye Jukwaa la Spika naomba nimtambulishe Mzee wetu Mzee Rajani kwa mikoa mingi sana hapa Tanzania amefanya kazi nyingi sana za biashara lakini pia za huduma ya jamii. Ninavyofahamu huko Wilaya ya Kahama alijenga sekondari wa fedha yake mwenyewe na watoto wanapata elimu, namshukuru sana. Karibu sana Mzee Rajani. Na. 117 Ujenzi wa Daraja la Munguri MHE. PASCHAL C. DEGERA aliuliza:- Kwa kuwa, Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, iliahidi kuchangia gharama za ujenzi wa Daraja la Munguri Wilayani Kondoa lakini hadi sasa haijatekeleza ahadi yake:- (a) Je, kwa nini Serikali haitekelezi ahadi yake hiyo? (b) Je, ni lini sasa Serikali itaitekeleza ahadi hiyo? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Paschal Constantine Degera, Mbunge wa Kondoa Kusini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- 1 (a) Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa iliahidi kuchangia gharama za ujenzi wa daraja la Munguri Wilaya ya Kondoa kwa kiasi cha Shilingi 122,000,000/=. Napenda kumfahamisha Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imetimiza ahadi yake kwa kutoa jumla ya shilingi milioni 122 kama ilivyoahidi.
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NANE Kikao Cha
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________ MKUTANO WA NANE Kikao cha Kumi na Tatu – Tarehe 29 Juni, 2007 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kabla sijamwita Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii kwa Kuwasilisha Hati. Naomba niwashukuru nyote jinsi tulivyoshirikiana kwa pamoja kuweza kumsindikiza mwenzetu Marehemu Amina Chifupa Mpakanjia, katika safari yake ya mwisho. Waheshimiwa Wabunge, napenda niwashukuru Kamati ya Uongozi na Tume ya Huduma za Bunge, lakini pia TWPG kwa kushirikiana vizuri sana kuweza kumsindikiza mwenzetu kwa heshima; na kipekee naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu atutolee salamu za shukrani kwa Mheshimiwa Rais kwa jinsi ambavyo Mheshimiwa Rais alivyokuwa karibu nasi kila dakika kwa mawasiliano hadi hapo jana kule Njombe. Waheshimiwa Wabunge, narejea tena Mungu ailaze roho ya Marehemu Mheshimiwa Amina Chifupa Mpakanjia, mahali pema peponi. Amin. Hati ifuatayo iliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Taarifa ya Mwaka na Hesabu za Shirika la Hifadhi ya Taifa (TANAPA) kwa mwaka 2005/2006 (The Annual Report and Accounts of the Tanzania National Parks for the Year 2005/2006). MASWALI NA MAJIBU Na. 106 Ubovu wa Barabara za Jiji la Dar es Salaam MHE. MUSSA A. ZUNGU aliuliza:- 1 Kwa kuwa sura ya nchi yetu iko katika Jimbo la Ilala; na kwa kuwa barabara nyingi za Jiji la Dar es Salaam ni mbovu sana hali inayosababisha msongamano wa magari na
    [Show full text]
  • Majadiliano Ya Bunge ______
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA ___________ MAJADILIANO YA BUNGE ____________ MKUTANO WA TISA Kikao cha Saba – Tarehe 7 Novemba, 2007 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua HATI ILIYOWASILISHWA MEZANI Hati ifuatayo iliwasilishwa Mezani na:- MHE. MOHAMED H. MISSANGA - MWENYEKITI WA KAMATI YA MIUNDOMBINU: Taarifa ya Kamati ya Miundombinu kwa Mwaka 2006. MASWALI NA MAJIBU Na. 86 Ufanisi wa Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali MHE. ESTHERINA J. KILASI aliuliza:- Kwa kuwa, Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali, imekuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na ufanisi unaonekana kuwa si mzuri sana:- Je, ni lini ofisi hiyo itakuwa wakala ili iweze kufanya kazi zake kwa ufanisi zaidi? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa idhini yako kabla ya kujibu swali la Mheshimiwa Estherina Kilasi naomba kutoa pongezi zangu za dhati kwa Chama cha Mapinduzi, kwa kukamilisha chaguzi zake. Nikupongeze wewe Mheshimiwa Spika, kwa kuongoza vizuri Kamati ile ya usimamizi kwa kufanyakazi kwa kasi na viwango inavyotakiwa. Nawapongeza wote waliopita katika sekretarieti na wajumbe wa Kamati.Kwa niaba ya 1 Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Estherina Kilasi, Mbunge wa Mbarali, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Idara ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali, ina dhamana ya kuchapa Nyaraka muhimu zote za Serikali Kuu, Serikali za Mitaa na Taasisi za Serikali za Mitaa na Taasisi za Serikali. Idara hiyo bado haijawa Wakala wa Serikali kwa kuwa ushauri huo ulikuwa bado tunaufanyia kazi. Kwa hivi sasa Serikali imekamilisha uchambuzi wake na kukubalika kwamba Idara ya Mpigachapa wa Serikali, haiwezi kuingia kwenye mfumo wa uwakala mpaka ukamilike mpango wa kuipatia mitambo na vitendea kazi ambavyo vitawezesha kukifanya kifanye kazi kwa ufanisi.
    [Show full text]
  • Tarehe 6 Aprili, 2006
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA __________ MAJADILIANO YA BUNGE _________ MKUTANO WA TATU Kikao cha Nane - Tarehe 6 Aprili, 2006 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta) Alisoma Dua SPIKA: Kabla hatujaingia kwenye shughuli za leo asubuhi nakuombeni Waheshimiwa Wabunge tuwatambue Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu wakiongozwa na Mwenyekiti wao wa Halmashauri hiyo. Ni wale wamesimama pale. Ahsante sana. (Makofi) HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Taarifa ya mwaka na Hesabu zilizokaguliwa za Serikali za Mitaa kwa kipindi cha mwaka kinachoishia tarehe 30 Juni, 2005 (The Annual Report and Audited Accounts of the Local Authorities for the year ended 30th June, 2005) NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. MUSTAFA H. MKULO): The Statutory Report of the Controller and Auditor General on the Audit of the Financial Statements of Ministries Independent Departments and Affiliated Bodies for the Financial year ended 30th June, 2005. MASWALI NA MAJIBU Na. 105 Madawa ya Kulevya MHE. PETER J. SERUKAMBA (k.n.y. MHE. ANNE K. MALECELA) aliuliza:- 1 Kwa kuwa tatizo la vijana na baadhi ya watu wazima kutumia dawa za kulevya katika nchi yetu sasa hivi limekuwa kubwa sana na kwa kuwa dawa hizo zimekuwa ni chanzo kikuu cha kuathiri akili za watumiaji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukomesha biashara hii haramu? NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, MAAFA NA KAMPENI DHIDI YA UKIMWI (MHE. DR. LUKA J. SIYAME) alijibu:- Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, Mbunge wa Same Mashariki, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwepo kwa tatizo la baadhi ya vijana na watu wazima kutumia dawa za kulevya hapa nchini na kwamba baadhi yao wameathirika kutokana na matumizi ya dawa hizo.
    [Show full text]
  • MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao Cha
    Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE _______________ MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Ishirini na Tatu – Tarehe 8 Julai, 2009 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:- Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2009/2010. MHE. MUSSA A. ZUNGU (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA): Taarifa ya Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka 2008/2010 pamoja na maoni ya Kamati kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2009/2010. MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM - MSEMAJI WA KAMBI YA UPINZANI KUHUSU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2009/2010. NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO Randama za makadirio ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa mwaka wa fedha 2009/2010. 1 MASWALI NA MAJIBU Na. 171 Kutangazwa kwa Miji Midogo MHE. DORAH H. MUSHI aliuliza:- Kwa kuwa tarehe 17/09/2004 Miji midogo ipatato 90 ilitangazwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 353 ambapo Mji wa Mererani ni miongoni mwa Miji iliyotangazwa ukiwa na wakazi wapatao 48,000. (a) Je, miongoni mwa Miji iliyotangazwa ni Miji mingapi imekwishaanza? (b) Je, ni Miji mingapi iliyopata ruzuku moja kwa moja ya kujiendesha toka Serikali Kuu? WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:- Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dora Mushi, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:- (a) Mheshimiwa Naibu Spika, Mamlaka ya miji midogo ni Mamlaka ya Serikali za Mitaa iliyopo kwenye Mamlaka ya Wilaya.
    [Show full text]